Haya ndio yaliyokuwa maneno ya Slaa,baada ya kuombwa kutoa ufafanuzi na kijana wa CHADEMA kuhusu swala la Zitto:
"CHADEMA katka nidhamu haijaogopa,vinginevyo hatutakuwa tofauti na CCM.CHADEMA tunajiamin,Tukisimamia kitu tunajiamini tutakisimamia.Kama tusiposimamia maadili ndani ya chama hatuna sababu ya kwenda ikulu,kwa sababu tutakuwa wezi kama CCM.Kama tuliwaondoa madiwani watano,tukaumia sana nafsi zetu kwamba madiwan tunawatafuta kwa gharama kubwa,walipoasi wale madiwan watano,wakaingia kwenye mkataba na CCM,hatukuogopa madhara ya kuwaondowa watano,tuliwaondoa wote.Tofauti na CCM walioshindwa kumuondoa meya fisadi.Kama CHADEMA haitasimamia misingi yake,hatuna sababu ya kuchaguliwa na watanzania kwenda ikulu"
Wana jf naomba tujadili kwa moyo mweupe maneno haya ya kizalendo na ya kiwajibikaji bila ushabiki.