Yaliyojiri katika Maadhimisho ya Mei Mosi - Mbeya

Yaliyojiri katika Maadhimisho ya Mei Mosi - Mbeya

Hawa wana Mbeya siyo wa kawaida, wanapita kimya hata hawampungi mkono mgeni rasmi Mhe.Rais Kikwete.Mshereheshaji anazidi kutia morali eti jamani shangilieni,chekeni mkipita mbele ya mgeni rasmi.Sura za waandamanaji zimenuna!
 
Wanajamvi. Nafuatilia yanayojiri Mbeya. Lakini Napata shida sana nikiangalia maandamano ya wafanyakazi naona wanawake ni wengi zaidi ya wanaume, hasa waalimu. Kwanini hasa gender imbalance kubwa hivi? Wanaume hawaoni umuhimu wa siku hii ya leo au ndo wamekata tamaa zaidi kuliko dada zetu na mama zetu? Tunaweza kujadili kuhusu uvumilivu na ustahimilivu hapa? Naomba mtiririke lakini tuache yale maneno makali na ya dharau. Nawasilisha.
 
Magamba tu wale mbao hawajitambui (Filikunjombe exclusively) ndio waliopungia humo!
 
Hao ni walimu, wapo hapo kwa sababu kuna rokoo iliyopitishwa pamoja na kuchimbwa mkwara "mwalimu asiyekuja atafukuzwa kazi"...
 
sio fair fair naona baadhi ya waandamanaji ktk sherehe za mei mosi mby wamenuna kinoma,sijui wana maana gani?mpk MC anawataka wawe na furaha na kuwave back kwa mkuu..
 
Naomba kuuliza hivi hakuna "wazee wa Mbeya" labda angezungumza nao kama wafanyakazi wamenuna?
 
Dah SUGU atakuwa ameharibu huko si bure.
 
mkuu mimi nafuatilia kupitia tbc naona watu wamehamasika sijui wewe upo uwanja gani au upo uwanja wa jamhuri mkuu.
 
Kaizer. Wazee wa Mbeya ni wabishi, hawawezi kukubali kukaa kimya na kusikiliza hata yale wasiyokubaliana nayo kama wafanyavyo wazee wa Dar es salaam!
 
Last edited by a moderator:
Naomba kuuliza hivi hakuna "wazee wa Mbeya" labda angezungumza nao kama wafanyakazi wamenuna?

Wapo Mkuu wameingia na Bango lao wakidai JK awasaidie wapate mafao yao kwa wakati
 
..unataka wachekecheke ? Kawatekenye basi,hujui hapa ni mbeya ?
 
Kuna nini sasa cha kuwachekesha! Unataka wajichekeshe kinafiki kama watu wa ccm!
 
Sasa sisi wafanyakazi hivi tulivyopigika unategemea tupunge mikono kweli , hizo nguvu tutapata wapi ?
 
mkuu mimi nafuatilia kupitia tbc naona watu wamehamasika sijui wewe upo uwanja gani au upo uwanja wa jamhuri mkuu.

Mimi nimeongelea jinsi watu walivyokuwa wamepooza tofauti kabisa na matarajio ya wengi na utofauti pia umeonekana ukilinganisha na mei mosi zilizopita
 
Back
Top Bottom