Namwona Mkuu wa mkoa wa Mbeya mhe.Abbas Kandoro anawakaribisha wageni.Pia anawataja baadhi ya wageni maalumu wakiwemo viongozi wa dini,wabunge n.k Naona ameanza kuzungumzia hali ya kilimo mkoani Mbeya huku akihusianisha wafanyakazi na wakulima.Amemaliza kuongea lakini hajapigiwa makofi.Mshereheshaji ameingilia kati, amewataka wafanyakazi kumpigia makofi matatu...kichekesho kwa kweli.Sasa anafuatia katibu wa TUCTA, naye pia anawatambulisha wageni maalumu walioalikwa akiwemo balozi wa China,Marekani,Italia,Msumbiji na wadau mbalimbali wa mashirika ya wafanyakazi. Mhe.Mgaya pia ametambua uwepo wa Mhe.Kinana,alisimama oa kupigiwa makofi kiduchu,huku Shukuru Kawambwa akipungiwa mkono na walimu wachache.