Yaliyojiri katika Maadhimisho ya Mei Mosi - Mbeya

KOMBAJR

JF-Expert Member
Nov 15, 2011
5,827
1,271
wanabodi heshima mbele ....

Naomba niwaletee update za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei Mosi ambayo kitaifa yanafanyika katika uwanja wa Sokoine jiji Mbeya.

Watu wameshaanza kuingia na viongozi mbali mbali wameshaingia nimemuona Hawa Ghasia,Mama Kabaka,Kinana,Kawambwa,Makongoro na mabalozi mbali mbali.

UPDATES:
- Kwa ufupi uwanja uko mtupu wazo la kupeleka mbeya linaweza kuleta tafsiri mbaya ya jamaa kukubalika kazi kweli kweli wanafuta muda ili watu wajae jae isijekuwa aibu kwa Mgeni rasmi. Hivi watoto wa shule nao ni wafanyakazi?

- Mgeni Rasmi Rais Kikwete ndo anaingia uwanja wa sokoine tayari kuongea na wafanyakazi akifuatiwa na maandamano ya wafanyakazi yalioyoanzia nzomve!

- Rais ameingia ila hamasa kwa wahuzuriaji siyo nzuri mpaka mshereheshaji akiwalazimisha wananchi kumshangilia kitu ambacho akijakubaliaka zaidi ya matarumbeta.....anadai eti wananchi wa mbeya wana historia ya kupokea wageni wapi!

- Rais ameshashuka kwenye gari lake amelakiwa na viongozi mbali mbali na kuelekea jukwaani, kwa ufupi watu wapo Doro sana Mshereheshaji anakazi ya ziada kuamasisha watu kushangilia kitu ambacho hakipo.

- Makundi ya wafanyakazi yanaingia kwa maandamano katika uwanja wa sokoine kulingana na sekta zao, Mshehereshaji anasema eti kujitokeza kwa wingi kwa walimu kutaongeza ufaulu wa wanafunzi wanabodi vinahusiano hivi?

- Ninachokiona kwenye maandamano haya ya wafanyakazi wa taasisi na sekta mbali mbali ni matabaka ya kiuwezo wa taasisi husika kuanzia kwenye mavazi mpaka vikorombwezo.................

- Boda Boda na Bajaji naona nao ndani ya nyumba ndizo ajira ambazo JK amezitengeneza

- Kudos ofisi ya bunge mmewakilisha vyema ............

- Wimbo wa taifa na wimbo wa wafanyakazi unatendewa haki

................................

Mkuu wa Mkoa anawakaribisha wageni mbali mbali katika jiji la mbeya na katika maadhimisho ya mei 2013 tayari kabisa kuanza maadhimisho........

Mgaya anatambulisha wageni walioalikwa katika sherehe hizi...........kinachofuata ni salamu za mkoa wa mbeya na zinatolewa na Mkuu wa Mkoa Bw. Kandoro....... ameambiwa atoe salamu za mkoa yeye anatambulisha

Kujipendekeza (Ukada) kubaya sana mtu hayupo kwenye ratiba yeye anataka aongee anataka Mama Salma atoe salaam amepotezewa!

Katika salaam za ATE wanasema maslai ya wafanyakazi hayaboreki kwa kasi ya mabadiliko ya kiuchumi,wanamtaka raisi waweke mgawanyo mzuri katika rasilimali za nchi hii

Waziri Kabaka - Mwenye mamlaka na wafanyakazi

  • Waziri kabaka mpaka sasa wameshindwa kutamka kima cha chini cha sekta binafsi changa la kwanza, amehahidi kabla ya mwezi huu kwisha watakuwa wametangaza kima cha chini cha mishahara kwa wafanyakazi wa sekta binafsi. Uanzishwaji wa mfuko wa wafanyakazi wanaoumia katika maeneo ya kazi upo kwenye mchakato na hatua za mwisho
Katibu Mkuu Tucta- Mgaya

  • Katiba Mpya izingatike haki kwa tabaka la wafanyakazi, mishahara iwe agenda ya kitaifa.
  • Serikali kukopa katika mifuko ya hifadhi ya jamii na kutorudisha kunazidi kuwaongezea majonzi wastaafu
  • Amezungumzia suala la udini pia
  • Hali ya elimu katika nchi pia TUCTA wanatakujua serikali imechukua hatua gani kukabiliana na wimbi kubwa watoto wengi kufeli.
  • Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi itakuwa na tija pale tu maagizo na makubaliano yatakapokuwa yanatekelezwa.
JK- Hotuba

  • Wameipokea hotuba ya Katibu wa TUCTA na wataifanyia kazi sababu imekamilika katika idara zote.
  • Serikali kutokuongeza mishahara kwa wafanyakazi kwa muda husika hakutokani na mtimanyongo bali ni hali halisi ya kipato cha serikali
  • serikali wataunda chombo cha kusimamia utekelezaji wa mambo mbali mbali kwa kuanza wataanza na sekta 6
  • Ajira 168,000 zimezalishwa kufikia mwisho wa mwaka jana
  • Kodi kwenye PAYE Kupunguzwa 13% mpaka.......... waziri wa fedha atatangaza kwenye bajeti
  • waligundua kasaro nyingi katika Mamilioni ya JK, watu wengi walipewa pesa bila kupewa mafunzo ila kwasasa watazingatia hilo katika kutoa mikopo kwa Vijana na wanawake.
  • Serikali wanaanzisha utaratibu wa kuwakopesha nyumba wafanyakazi ili kuwapunguzia ukali wa maisha
  • Kiwanja cha mbeya cha songwe Umekamilika hii inafungua biashara na kukuza uchumi kwa mikoa ya iranga,Njombe na Mbeya
  • Wanambeya wanapata fursa ya kupata historia ya Malkia wa Uholanzi na uhusiano na Tanzania.....Duh!
  • fursa za kilimo cha maua kutokana na miundo mbinu zilizopo katika mikoa tajwa, makampuni ya kigeni yatakuwa ila ndiyo mambo ya eeh!this one eeh dont worry hakuna
  • Mbeya kufikia mwaka 2018 hakutakuwa na tatizo la maji kabisa.
  • Anazungumzia Udini watanzania wajiepushe na migogoro inayotokana na imani
  • Turejee enzi za mababu za waislamu na wakiristo kushirikian
  • JK amezindua Gazeti la Mfanyakazi
Mwisho:
Kila lililozungumzwa serikali watalifanyia kazi ni wajibu wao kuwasikiliza na kutatua kero za wafanyakazi.

Wanabodi Asanteni kwa uvumilivu wenu katika kufuatilia updates, Mtaniwia Radhi kwa yale ambayo sijaweka ni mapungufu tu ya kibinadamu unaweza ongeza kwa faida ya wanabodi. Kazi kwenu sasa Je yote yaliyozungumzwa ya Tija? Picha zitawajia ASP.

8E9U2311.jpg images jk.jpg

Naomba Kuwasilisha
 
Kinana tena, yeye ni nani hadi kwenye mei mosi
Yeye ni mfanyabiashara maarufu sana hapa nchini na nje ya nchi kwa sababu hiyo ameajiri watu wengisana ambao leo wanaadhimisha siku yao ya wafanyakazi. Hasa biashara yake yake ya kuuza meno ya tembo a.k.a pembe za ndovu a.k.a nyara za serikali....Thubutu....sio mfanya biashara wa kimataifa ni Jangili wa Kimataifa na leo anawakilisha majangili wenzie kwenye sherehe za wafanyakazi.......WEKA MBALI NA TEMBO
 
Ile hotuba ya kihistoria ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Rest in Peace) Mei Mosi, 1995 ilikuwa Mbeya. Naona safari hii wameamua kukisafisha chama chao kwa kwenda tena Mbeya ili kufuata nyendo za Baba wa Taifa. Well, tusubiri tuone impact yake.
 
Wakuu, Kama mjuavyo leo ni holiday na nikiwa napitisha remote ili niangalie channel ya Ten Sport nikaona TBC 1 wanarusha moja kwa moja maadhimisho ya mei mosi moja kwa moja kutoka Sokoine Mbeya.Kwa mlio karibu na Runinga mnaweza kuendelea kutazama na wale mlio mbali nitakuwa nawapa updates.Awali kuna kwa sasa kikundi cha ngoma kinatumbuiza.
 
Wakuu, Kama mjuavyo leo ni holiday na nikiwa napitisha remote ili niangalie channel ya Ten Sport nikaona TBC 1 wanarusha moja kwa moja maadhimisho ya mei mosi moja kwa moja kutoka Sokoine Mbeya.Kwa mlio karibu na Runinga mnaweza kuendelea kutazama na wale mlio mbali nitakuwa nawapa updates.Awali kuna kwa sasa kikundi cha ngoma kinatumbuiza.
Makala umeamka na malaria nini? Hivi ni nani mwenye akili anayeweza kuangalia tbccm wakati kitakachoongelewa na zaifu ni taarabu tu
 
Naona kina Mama wakicheza kwa mbwebwe huku wakiwa wamevalia kanga na t-shirt zenye rangi nyekundu,sijui wanaimba kilugha gani hawa ndugu zetu.T-shirt zao zote zimeandikwa namba 10...nahisi ni watani wangu hawa!
 
Hakika ni burudani kwenda mbele, wacheza ngoma wamependeza kwa mavazi safi sana, imatia moyo kuwaangalia wananchi walivyo na raha katika sherehe. Hongera CCM na serikali yake kwa kuweka mazingira safi na slama hatimaye watanzania wanafuraka kuzidi kifani!
 
Hakika ni burudani kwenda mbele, wacheza ngoma wamependeza kwa mavazi safi sana, imatia moyo kuwaangalia wananchi walivyo na raha katika sherehe. Hongera CCM na serikali yake kwa kuweka mazingira safi na slama hatimaye watanzania wanafuraka kuzidi kifani!

Aseeeee....
ImageUploadedByJamiiForums1367395345.988734.jpg
 
Hakika ni burudani kwenda mbele, wacheza ngoma wamependeza kwa mavazi safi sana, imatia moyo kuwaangalia wananchi walivyo na raha katika sherehe. Hongera CCM na serikali yake kwa kuweka mazingira safi na slama hatimaye watanzania wanafuraka kuzidi kifani!

Ubarikiwe Mafilili mgeni rasmi atakuja saa ngapi watu wameshachoka aje hatubie hao waliopo hiyo ndiyo hali ya halisi
 
Jamani hii haki kukaguliwa kama naingia kwenye ndege, mbeya kunanini hadi watu wakaguliwe hivi??
 
Back
Top Bottom