Katika kikao cha leo asubuhi bungeni, katika kipindi kiliobakia kurushwa " live" nimeliona tukio kwa hofu ya kukiuka sheria ya mtandao, naomba wana bodi, moderators wanisaidie.
Katika majira kati ya saa nne na dakika thelathini mpaka na dakika thelathini na sita ( 10:30-10:36) Wabunge wawili wa chama tawala wa jinsia tofauti walipojitanua. Sasa sijui niliangalia kwa makengeza au sawa, naomba nisaidieni.
Ikiwa nilichokiona ni sahihi, basi kitendawili cha siri ya bunge kukataa kuoneshwa " live" kimeteguliwa