Yaliyojili jioni hii mahakamani kati ya Mnyika vs Hawa Ngh'umbi

huyu mama katafuta mashahidi wake wa kuungauunga hawaelewi hata kinachoendelea,yaani hii kesi ni kupoteza mda
 
Haya yote ni matatizo ya mzee Makamba wakati akiwa katibu wa CCM na kuwadanganya wabunge wa CCM walioshindwa wafungue kesi na chama kitawasaidia. Mwisho wa siku hata wale ambao hawajielewi kama kina Hawa nao wakafungua kesi wakiamini chama chao kinaweza kurubuni mahakama na ushindi ubatilishwe. Sasa hali imekua sio hali na aibu zinawakuta sasa. Dah, Makamba kweli kiboko.
 
Sasa CCM wameanza kuokota Vichaa waje kuwatolea ushahidi! Mwenye akili timamu hawezi kwenda kujiaibisha kwenye madai ya kijinga kama haya!
 
kweli ccm imeishiwa maana watu wenye akili nzuri wa kuitetea hawapo mpaka wanaokoteza hadi walevi

Tatizo la hizi kesi za magamba nyingi zilifunguliwa kwa shinikizo la Makamba. Yeye kasepa kiaina ngoma imebaki kwa wahusika maana sina uhakika kama magmaba wanawasaidia wahusika kama alivyoahidi Yusufu Makamba
 
Ningekua Jaji hakuna cha kusubiri huyo shahidi wala upuuzi mwingine wowote,
Bali hapohapo nafuta kesi watu waendelee na dili zao zingine!!!
 
Mashahidi wawili muhimu wa upande wa mlalamikaji Hawa Ng’umbi wamegoma kuja mahakamani kutoa ushahidi hali iliyomfanya mlalamikaji kufunga ghafla ushahidi wake hapo jana. Wakili wa Mlalamikaji Issa Mayige awali alisema kwamba wangeleta mashahidi wengine wawili hata hivyo muda wa mashahidi hao ulipofika alieza kuwa shahidi kutoka ITV ameshindwa kupata ruhusu ya mwajiri wake. Kutokana na hali hiyo Jaji Upendo Msuya alimtaka wakili wa mlalamikaji kufanya mawasiliano na mashahidi wake kupata uhakika iwapo watakuja mahakamani. Mlalamikaji Hawa Ng’umbi na wakili wake walipiga simu kwa mashahidi hao na kurejea mahakamani na kueleza kuwa mashahidi hao hawawezi kuja mahakamani hivyo wameamua kufunga ushahidi. Kesi hiyo itaendelea tarehe 29 Machi 2012 ambapo upande wa walalamikiwa utaanza kutoa ushahidi wake. Mlalamikiwa namba moja na namba mbili ambao ni ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali na tume ya uchaguzi wataanza kutoa ushahidi.
 
naona kuna wimbi la ''court abuse'' linalofanywa na wanachama wa ccm.
Hili linapaswa kukemewa kwa nguvu zote.
 
Sisi watu wa Iringa tuna msemo mmoja unasema "UWUDODI WAWIKALA" ubichi hukauka.

UWUDODI WA CCM WIKALA
Wamefirisika hoja.
Wamefirisika kisiasa.
Wamefirisika matusi.
Wamefirisika kifedha
Sasa wamefirisika mashahidi wa kununua.
 
mashahidi wawili muhimu wa upande wa mlalamikaji hawa ng’umbi wamegoma kuja mahakamani kutoa ushahidi hali iliyomfanya mlalamikaji kufunga ghafla ushahidi wake hapo jana. Wakili wa mlalamikaji issa mayige awali alisema kwamba wangeleta mashahidi wengine wawili hata hivyo muda wa mashahidi hao ulipofika alieza kuwa shahidi kutoka itv ameshindwa kupata ruhusu ya mwajiri wake. Kutokana na hali hiyo jaji upendo msuya alimtaka wakili wa mlalamikaji kufanya mawasiliano na mashahidi wake kupata uhakika iwapo watakuja mahakamani. Mlalamikaji hawa ng’umbi na wakili wake walipiga simu kwa mashahidi hao na kurejea mahakamani na kueleza kuwa mashahidi hao hawawezi kuja mahakamani hivyo wameamua kufunga ushahidi. Kesi hiyo itaendelea tarehe 29 machi 2012 ambapo upande wa walalamikiwa utaanza kutoa ushahidi wake. Mlalamikiwa namba moja na namba mbili ambao ni ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali na tume ya uchaguzi wataanza kutoa ushahidi.

ni kitu gani hawa ng'umbi analalamikia katika hii kesi?

 

ni kitu gani hawa ng'umbi analalamikia katika hii kesi?


Eti Joni kachakachua kura kisa aliingia na laptop zake 5 na watu zaidi ya nane ndani ya chumba cha kuhesabia kura kinyume cha taratibu..huyu mama alitaka kui drop hii case lakini akatakiwa atoe ten M.nafikiri alichemka

 
kwani JK hajampa madaraka huyu mama kama ukuu wa mkoa au hata wilaya au ubarozi??
hawa ng'umbi ni ************
alafu tukumbuke huyu mama alishapewa jukumu la ukuu wa wilaya ili asimamie sheria sasa unajiuliza hayo mazingira ya kazi huko alikokuwa yalikuwaje!!!
Hii inahusisha ujuzi kidogo tu wa sheria ambapo either kwa kutokujua kwake au kwa makusudi mazima ili kupoteza muda wa serikali na kuchelewesha maendeleo ya nchi yetu.

 
Kama mazingira ya kesi ndio hayo si ipelekwe mahakama ya mwanzo ikasikilizwe na wazee wa baraza wanamsumbua Jaji mzima kukaa hapo kusikiliza vituko vyao huu si udhalilishaji wa mahakama?
 
Back
Top Bottom