chongchung
JF-Expert Member
- Jun 23, 2013
- 14,303
- 45,098
Kuna makanisa ya Kweli na ya uongo sio kwamba yote matapeli and the Word is widely straight-out unabii unatimia wa nyakati za mwisho.
Kuna makanisa ya Kweli na ya uongo sio kwamba yote matapeli and the Word is widely straight-out unabii unatimia wa nyakati za mwisho.
mshana na wewe nahisi unataka kuwa mchungajiUp sahihi chongchung na post hii imelenga hayo ya uongo
Wajinga Ndiyo Waliwao.
Sasa hivi ni mwendo wa kurudisha nguvu za Kiume, kutafuta Mume/Kuolewa, utajiri, kusafisha nyota.....Hawana tofauti na waganga a kienyeji..
Naona yakhe umerukia mada nyingine !
Hii lugha imetumika mpaka ndani ya Biblia.
Soma kitabu cha 'Mwanzo' utakuta lugha kama: .......na tuumbe mtu kwa mfano wetu.
Yakheee upo ?
Na manabii na mitume wenyewe ni wajanja wanapeleka makanisa yao kwenye mzunguuko wa hela kama Dar,Mwanza na Arusha
Hiyo yakutuma sadaka niliona Kenya, nilikwenda kumuona rafiki yangu Nairobi akanambia wao wanatuma hela kwa njia ya simu halafu wanaambiwa kutakua na maombi saa kadha ukamate TV ufungemacho uombewe,nilishangaaa sana lakini sikutaka kumkera sababu alikua serious na wanamuamini sana huyu mchungaji,nikaishia kujiuliza maswali mwenyewe nikajijibu mwenyewe..
mzee wako alikuwaga kalumanzila?
Am I not supposed to respond to the accusation?
It is you who don't read the Bible, but people who are informed are doing it. Hereunder is the impeccable proof.
Matthew 10:8 Heal the sick, raise the dead, cleanse those who have leprosy, drive out demons. Freely you have received; freely give.
Hili jambo miaka mitatu nyuma lilikuwa maarufu sana, yaliibuka makanisa ya mitume na manabii kwa kasi ya ajabu yaliyokuwa kila wakati yakituonyesha picha za wafu waliokufa kimazingara na baadae kufufuliwa nao.
Karata hii isiyo na chembe ya haya wala soni ya udanganyifu ikawapatia waumini wengi na umaarufu mkubwa.
Gwajima bingwa wa haya mazingaombwe kwa kujiamini kabisa aliutangazia uma wa waumini wake kuwa angemfufua Marehemu Amina Chifupa RIP, watu wakausubiri kwa hamu muujiza huu, Chifupa mpaka leo hajafufuka.
Maumivu yalibaki kwa mtoto wake na ndugu zake ambao jina la ndugu yao lilitumika kwa malengo binafsi huku magazeti ya udaku yakiwa kichocheo kikuu
Watu wote tuliowaona wakifufuliwa hatujawahi kuonyeshwa ndugu zao na historia zao, sijawahi kuona mtu wa Dar akifufuliwa au mtu ninayemfahamu, bali mtu wa dar alifufukia Arusha, wa mwanza alifufukia dar nk.
Upofu wa imani ukawafanya wengi wakimbilie kwenye haya makanisa, lakini sasa mambo yamebadilika na uongo wao umejulikana! Siku hizi kufufua misukule sio dili tena, kilichopo ambacho nacho kinakufa ni kutoa mapepo! Hivi mapepo yanakaa kwa akina mama tuuu!?
Imani ni kitu kizuri pale tu unapojitambua kuwa unaamini nini na kwa nini! Hawa manabii na mitume wa uongo wamechuma Mali nyingi kwa waumini wapumbavu! Serikali iliangalie hili kwa makini yasije kutokea yaliyotokea Uganda, Kenya na ulaya kule watu waliojiuwa kwa maelfu kwa maagizo ya viongozi wao wakiamini kwa kufanya hivyo watakwenda peponi.