Nanyaro Ephata
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,237
- 1,828
Niliwahi kuandika kuhusu huyu Waziri wa Fedha anajiitaga mchumi wa daraja la kwanza! Huyu ni miongoni mwa mawaziri ambao ni mzigo kwa Watanzania!
Leo Bwana Mwigulu akiwa Bungeni amewatangaza watu watatu kuwa mabalozi wa kodi, Mobeto, Samata na Edo Kumwembe. Sasa twende taratibu, tatizo la kodi Tanzania ni tatizo la mfumo wa kodi wenyewe, tatizo ambalo waziri na timu yake walipaswa kulitatua kwanza!
Kodi haitalipika kwa HAMASA wala kuwa na MABALOZI bali kwa kuondoa kero kwa wafanyabiashara. Kodi italipika kwa kuongeza wigo wa walipa kodi. Kodi italipika kwa kuweka mazingira rafiki ya ulipaji kodi. Hapa lazima serikali itekeleze wajibu wake kimsingi Serikali imeacha wajibu wake wa kuongeza wigo wa walipa kodi badala yake hata wale wachache imeshindwa kuwalinda.
Kila kona machinga wanauza bidhaa na hawalipi kodi leo uniambie Samatta /Hamisa atawasihi waliofungiwa biashara zao na machinga walipe kodi?
Serikali inapaswa kuweka mazingira rafiki ya kuanzisha zaidi SMe ili kupanua wigo wa walipa kodi!pia ipunguze mlolongo na utitiri wa kodi ambazo hugeuka mzigo kwa mlipa kodi,badala yake kuwepo na kodi zinazolipika
Cosmetic solution haiwezi kuwa suluhisho,kuwa na mabalozi sio suluhisho unateua Balozi ambaye hajawahi kulipa hata milioni TRA au hajui hata huo mlango wa TRA unafananaje
Wizara ya fedha iache mzaha ndani ya TRA kuna kitengo cha elimu ya mlipa kodi,kitengo hiki kifanye kazi yake kitalaam,kiache kuishi zama za kale
Kama ni lazima sana kuwa na balozi wa kulipa kodi basi Waziri alipaswa kutafuta walipakodi wakubwa ndio wawe mabalozi
Leo Bwana Mwigulu akiwa Bungeni amewatangaza watu watatu kuwa mabalozi wa kodi, Mobeto, Samata na Edo Kumwembe. Sasa twende taratibu, tatizo la kodi Tanzania ni tatizo la mfumo wa kodi wenyewe, tatizo ambalo waziri na timu yake walipaswa kulitatua kwanza!
Kodi haitalipika kwa HAMASA wala kuwa na MABALOZI bali kwa kuondoa kero kwa wafanyabiashara. Kodi italipika kwa kuongeza wigo wa walipa kodi. Kodi italipika kwa kuweka mazingira rafiki ya ulipaji kodi. Hapa lazima serikali itekeleze wajibu wake kimsingi Serikali imeacha wajibu wake wa kuongeza wigo wa walipa kodi badala yake hata wale wachache imeshindwa kuwalinda.
Kila kona machinga wanauza bidhaa na hawalipi kodi leo uniambie Samatta /Hamisa atawasihi waliofungiwa biashara zao na machinga walipe kodi?
Serikali inapaswa kuweka mazingira rafiki ya kuanzisha zaidi SMe ili kupanua wigo wa walipa kodi!pia ipunguze mlolongo na utitiri wa kodi ambazo hugeuka mzigo kwa mlipa kodi,badala yake kuwepo na kodi zinazolipika
Cosmetic solution haiwezi kuwa suluhisho,kuwa na mabalozi sio suluhisho unateua Balozi ambaye hajawahi kulipa hata milioni TRA au hajui hata huo mlango wa TRA unafananaje
Wizara ya fedha iache mzaha ndani ya TRA kuna kitengo cha elimu ya mlipa kodi,kitengo hiki kifanye kazi yake kitalaam,kiache kuishi zama za kale
Kama ni lazima sana kuwa na balozi wa kulipa kodi basi Waziri alipaswa kutafuta walipakodi wakubwa ndio wawe mabalozi


