Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Mjadala wa BILIONI 1500 unazidi kushika kasi... Sasa watu wanaulizwa ni kweli zimepotea... Wanasema hapana hazijapotea.
Na ni kweli hakuna panaposema zimepotea ila zimeingizwa kwenye matumizi yasiyoonekana kwenye makaratasi ya kumbukumbu. Sasa baada ya hapo kila mtu anaweza kuchanganya na za kwake.
Mbunge mmoja kule Afrika kusini wakiwa bungeni akasema nusu ya wabunge wote humu ndani ni wapumbavu. Kauli hii ikawakera wengi mpaka supika akamwamuru jamaa afute kauli yake.
Hakubisha! Akakubali kufuta kauli yake kwa kusema nusu ya wabunge wote humu ndani sio wapumbavu!!
Hivi tofauti ya kupotea na kutojulikana kilipo kitu ni ipi!?
Tunaishi nchi ya wanoni... Ni nani akamfunge paka kengele!? Ili akija wote tumsikie?
Na ni kweli hakuna panaposema zimepotea ila zimeingizwa kwenye matumizi yasiyoonekana kwenye makaratasi ya kumbukumbu. Sasa baada ya hapo kila mtu anaweza kuchanganya na za kwake.
Mbunge mmoja kule Afrika kusini wakiwa bungeni akasema nusu ya wabunge wote humu ndani ni wapumbavu. Kauli hii ikawakera wengi mpaka supika akamwamuru jamaa afute kauli yake.
Hakubisha! Akakubali kufuta kauli yake kwa kusema nusu ya wabunge wote humu ndani sio wapumbavu!!
Hivi tofauti ya kupotea na kutojulikana kilipo kitu ni ipi!?
Tunaishi nchi ya wanoni... Ni nani akamfunge paka kengele!? Ili akija wote tumsikie?