Yah: Kuunga mkono CHADEMA kwa sasa

Kuna watu wanatisha humu duh ushauri wao ni kama sumu.
Watu wanaandika tu ila wahajuhi what is like to be in the battle field has kwenye inch yenye demokrasia changa kama bongo.
Watu hawa hatuna uhakika kama hata wata piga kura wakiwa ughaibuni....watu hawa ni hatari
 

Mkuu,another side of the story ni HUJUMA ZINAZOFANYWA NA CCM.Hivi kama Rostam,Lowassa na mafisadi wengine wanaweza kumwaga pesa dhidi ya wana-CCM wenzao (ambao hawana madhara makubwa kwao zaidi ya kukemea au pengine kupongeza ref kujiuzulu kwa Lowassa)kwa vile tu wanawaona kuwa kikwazo katika ufisadi wao,wanawekeza kiasi gani kuhakikisha type za watu kama Dkt Slaa ambaye hachelei to call a spade a spade (ref List of shame) hawaingii madarakani.

Natambua kuwa kuna mapungufu ndani ya vyama vyote vya siasa.Natambua pia kuwa miongoni mwa vyama vya upinzani kuwa "waharibifu" na wasindikizaji kama akina Mrema.Lakini naamini kabisa kwa namna Chadema ilivyoshikilia bango suala la ufisadi angalau wametuonyesha wanatambua kikwazo kikuu cha maendeleo yetu ni nini.Naamini pia kuwa kwa uelewa huo itakuwa rahisi kwao kuu-employ kukomesha ufisadi pindi wakiingia madarakani.

Hizo chaguzi ulizotolea mfano tatizo kubwa na mazingira yaliyopo ambapo CCM "inakaba hadi kona".Mkuu wa Mkoa ana waraka wa kuwabana wapinzani,DC na waraka kama huo...RSO,DSO,RPC,OCD...the list goes on...na hapo hatujajumuisha "wasimamizi wa uchaguzi",viumbe ambao ajira yao inategemea "baraka za CCM".

Natambua mkuu,hata kama tunatofautiana kimtizamo,una uchungu wa hali ya juu kuhusu hali ya mambo huko nyumbani.Binafsi naendelea kuamini kuwa pasipo kuondoa kansa hii inayotishia kuharibu mwili mzima,sio tu kuwa safari yetu itachukua muda mrefu bali pia kuna hatari ya kutumbukia kwenye korongo refu along the way.

I just hope Dkt Slaa atapitishwa na Chadema kisha Watanzania wote (wenye uchungu wa kweli kwa nchi yetu) watampa sapoti ya nguvu ili tuwape red card mafisadi.Penye nia pana njia.
 
Ni sumu tena kali Mutu lakini kwa JF haimwagiki kirahisi wataimba hadi wachoke wenyewe. Wanatuambia eti tusubiri kwanza tujifunze kutawala ndipo tuing'oe CCM, kwani CCM walijifunza kutawala wapi ndipo wakaingia.

Hawajui machungu waliyonayo watanzania, wao wako ughaibuni watoto wao wanasoma kwa benefits hawajui hata kuwa watoto wetu ni jana tu walifukuzwa shule kwa kukosa mchango wa tuisheni wa shilingi mia tano, wao wakikosa kazi wanalipwa Jobseekers allowance.

Ndio hao hao wanatuambia tusubiri hadi machungu yawe makali ndipo tumtafute mganga, je kama ni ugonjwa wa kansa si utakuwa sugu hautibiki tena, uzuri tumewajua na lengo lao tumelijua hawatupi tabu.
 

Uchambuzi mzuri Rev, mapambano yana stages, huwezi kutarajia kumng'oa adui bila kuwa na mipango na hatua madhubuti. Mwenye kusikia atasikia. Kama hili la Dr Slaa kugombea uraisi litawagharimu Chadema na Wtz kwa ujumla
 

Sasa hii imekaa kama kuna uchu na chuki za madaraka.....duh siasa za TZ at it's best, sio kwa faida ya wananchi
 
Mkuu nimekusoma ndani ya mistari yako.
Na jana wametupa chaguo sahihi la mgombea na siye kuwa na chembe ya uoga hasa linapokuja swala la kitaifa.Siyo huyu Dr.wa kikwere kila siku nina list ya wezi,walafi,wauza bwimbwi halafua anashindwa kuyataja majina.

mbele tunasonga na kura tutampigia na ninaimani hata mkuu MMKJJ atampigia pia DR.Slaa.

Ee Mungu tuongoze watz tupate mwanga bora wa kuyaona maisha katika mwanga bora zaidi,, Amen.
 
Kama wanaandika na wewe umepata kuyasoma waliyoandika,basi yatafakari kwa kina na chukua hatua sahii kutoka kwa kichwa yako.
Maana kuandika kwao ndiyo faida kwako kuyaona,soma na kufanya tafakuri sahihi ili kujua nni kifanyike inchi isonge mbele!
 
Mkuu kusema ukweli katika hili sinabudi kuunga nawe kwamba kuitoa CCM tu halafu mengine mbele kwa mbele haina tija kwa taifa na si Chadema tu na hivyo vingine pia kwa kukaa na fikra mgando kuwa mipango ya uongozi na maendeleo havifanyiki mpaka wameingia jumba jeupe.Hiyo ni dhana ya kuikimbia kabisa.
Utawala siyo jumba jeupe tu,mambo iko huku chini(TANISEMI)ambako ndo kila kitu.
Mfano mmoja na wa kweli kabisa pasipokwenda hata huko kunakoitwa vijijini.Uchaguzi ulofanyika 2009 wa hapa DAR jimbo la KAwe kata ya Mbweni viongozi wa CCM walirudi madarakani pasipo uchaguzi kufanyika kwani hakuna mgombea hata mmoja wa upinzani alikuwepo.
Sasa kwa mtindo huu ukiing'oa CCM unatwala vipi hapo???
Ifike mahali vyama vya upinzani vilitazame hili kwanza,na nina imani kwamba ndiyo chanzo cha kukosa madiwani na wabunge wengi ambao wangeweza kuvisaidia katika suala zima wa uongozi mzima.
 
Luteni

Nyerere alipouliza Watu wanakimbilia Ikulu kuna nini? Tulifurahia kauli hiyo kuwa lenga kina Kikwete, Lowassa na hata Malecela, Warioba na Msuya.

Sasa leo hii tukiuliza Lipumba n Chadema wanakimbilia nini Ikulu, tunaambiwa aah nyie roho korosho, mko majuu hamjui hali halisi!

Najua hali halisi zaidi yako, usifikiri kukaa nje basi ndio kuwa disconnected, kama niko disconnected as you think, nisingeling'amua la Richmond au Meremeta kuwa ni Uhujumu uchumi na kulipshikia bango!
 
Inavyoonekana hukumwelewa Nyerere au ulimwelewa ila unataka kupindisha kwa makusudi.
 
mimi mwenyewe kwa ukweli kutoka moyoni nahitaji mbadiliko haswa.lakini je?CHADEMA ndio chama mbadala kweli??!mpaka sasa sioni kitu kwenye upinzani zaidi ya blaah blaaah tu,usishangae hata huyo slaa katumwa kutulaghai tu kisha ccm inapiga mwendo kwa ushindi bwerere.sijui mi naona wapinzani watasindikiza tu na kuambulia ruzuku.
 
Nafikiri umefika wakati ambapo viongozi wa vyama vya upinzani wakaangalia alama za nyakati. Huu ni muda muafaka kwa vyama hivi kutoa ushirikiano wa pekee ili viweze kumuondoa SISIEMU na mafisadi wake kwenye UTAMU. Kwa mtazamo wangu, wakati huu unaruhusu kabisa chama cha upinzani kukamata madaraka Tanzania. Ingekuwa BUSARA kwa CUF na vyama vingine kuunga harakati za CHADEMA kuingia madarakani (MUUNGANO) kwa niaba ya wapenda maendeleo ya nchi yetu na vilevile vyama vingine pamoja na CHADEMA kui-support CUF upande wa Zanzibar. Sasa tuone SISIEMU watafanya nini kuwahadaa wananchi kuiba kura kurudi madarakani.
HUU NI MUDA MUAFAKA, TUACHE UBINAFSI...........Rangi za Mrema tulishaziona muda mrefu sana.
 
Je, Mwalimu aliposema upinzani wa kweli utapatikana tu mpasuko ndani ya CCM utakapotokea ina maana tuwe kama mafisi yanayokaa yakitokwa na mate yakisubiri siku mkono wa binadamu utakapodondoka. Shuhudia watu fulani fulani walivyoichangamkia CCJ eti tu kwa vile makapi yalikuwa yanasubiriwa yatoke CCM na kujiunga nayo na hapo CCJ ingekuwa imetakasika kiasi cha kuachiwa nchi. Sidhani kama tunataka kuiondoa CCM madarakani kwa sababu ya sera zake kwani nijuavyo CCM haina sera ya rushwa, CCM haina sera ya wizi, CCM haina sera ya ufisadi - la hasha. Tunataka kuiondoa CCM madarakani kwa vitendo vyake na viongozi wake ambao wameamua kutotenda yale wanayoyahubiri, kutotimiza yale wanayotuahidi na kutapanya rasilimali za taifa letu kama vile hazina mwenyewe.

Tunaelewa kabisa kuwa kuna msurururu mrefu wa wanaofaidika kutokana na kukaa kwao madarakani na watatumia kila mbinu kulinda hiyo hali hata ikibidi kudai kuwa hakuna mwananchi nje ya CCM anayeweza kuliongoza taifa. Mojawapo ya hizo mbinu ni kuanza kutukejeli kwa maswali kama tunataka kuiondoa CCM ili iweje huku wakijua fika kuwa bila CCM kuketishwa benchi hakuna mabadiliko yoyote yatakayowezekana kirahisi. Namshukuru Mwanamapinduzi Dr. Slaa ambaye pamoja na vizingiti vyote vinavyowekwa na vitakavyowekwa mbele yake na hawa chui waliovaa nguo za kondoo, ameamuru kuongoza haya mapambano ya kulinusuru taifa. Mrema wa JF wako wengi.
 



Nyerere alisema watu wasiende ikuli tusiwe na viongozi? usipindishe maneno either kwa makusudi au kwa uelewa wako mdogo.I'm afraid makusudi maana post zako zinyi nasoma anakuchukulia kuwa ni mwelewa vya kutosha.
 
Leo nina furaha kubwa sana na siwezi kuchangia kitu ktk mada hii. Na hakika hata Nyerere mwenyewe alipokuwa akiitangaza TANU walikutana na watu wenye kubeza chama kuwa hakikuwa tayari kuchukua uongozi kwa sababu hawakuona what next baada ya kumuondoa mkoloni.
Nachoweza kusema tu hapa ni kwamba Chadema hawawezi kuongoza kwa katiba yao isipokuwa kwa katiba ya nchi ambayo ndiyo mwongozo na dira ya Utawala. Kama dira hii ilipotoshwa kimazingara inarudishwa..

Ukifunga ndoa kuoa au kuolewa ni wazimu mtu akikuuliza what next kwani yeye alitaka iwe vipi?..
 

Yup ,thats whatsup brother.
 

Mkuu, naomba nikutaarifu tu kuwa, Kenya ni bora zaidi sasa kuliko wakati wa uongozi wa KANU. Hasa kipindi ambacho KANU iliondolewa madarakani. Hiyo ni kweli na dhahiri. Nimeishuhudia.

Zambia pia ni bora zaidi kuliko kipindi chochote cha ZANU. Na hasa kipindi ambacho ZANU iliondolewa madarakani. Hii pia ni kweli na nimeishuhudia.

Mkuu, ukweli unabaki kuwa, mabadiliko ndio njia pekee ya kupata nafuu yoyote. Tumeshaona nini CCM inachoweza kukifanya kwa kukijaribu kwa miaka 18 tangu kuanzishwa kwa chama hicho na miaka mingine 15 tangu kuanzishwa kwa mfumo wa siasa za vyama vingi. Ninaimani kabisa kuwa, kwa mtiririko wa siasa za TZ kama hakuna disciplinary actions zitakazochukuliwa kwa mfumo huu wa utawala wa chama kimoja pamoja na umasikini unaotumaliza, kuna jambo baya zaidi litakaloikumba nchi yetu kuliko kama tutabadili kwa sababu zozote ziwazo.

Tusiogope mabadiliko. Tuogope kutobadilika. Kwani hata mgonjwa mahututi hutamani aachiwe apumzike badala ya kupelekwa hospitali kama chaguo lake la kwanza. Wakati mwingine, ukikaa sana juani, unaweza kudhani kuwa hapo ndipo mahali pazuri zaidi kuliko kama ukiwa kivulini. Hakuna faida ya uoga wa mabadiliko.

Ni jambo jema kuwa sasa tumesikia kuwa Dr. Wilbroad Slaa ameteuliwa/amechaguliwa/amejitolea kugombea u-Rais kwa kupitia chama cha upinzani (CHADEMA). Hakuna kitu ambacho nimekuwa nikiombea kuwa busara, hekima, mapenzi na moyo wa ujasiri umjae Mheshimiwa huu ili aweze kuchukua hatua kama hiyo. Sasa kwa mara ya kwanza kabisa najua kuwa kura yangu ya uRais inakwenda wapi na niko tayari kushawishi na kuomba kila mpenda mema, mjali hali za watu wote kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa Rais wa Tz kuanzia muda Rais mpya anaotakiwa kutangazwa atakuwa Dr. W. Slaa.

Naamini kuwa Dr. Slaa hatakuwa na roho ya kutojali kama Rais wa CCM alieshika madaraka kwa miaka mitani akifanya mzaha na kutojali umasikini wa Taifa lake, heshima ya nchi na malengo ya wananchi wake ambao walimuamini na kumkabidhi madaraka makubwa kabisa ya uongozi wa nchi. Naamini pia kuwa endapo Dr. Slaa atashinda na kuwa Rais, ataheshimu na kuthamini madaraka ya cheo hicho kuliko Rais aliepo na anaetaka kugombea tena. Naamini kwa busara, hekima na uthabiti wa Dr. Slaa, nchi hii itakuwa bora zaidi kuliko inavyoenda sasa. Itaheshimika zaidi na itafikia malengo ya kweli kwa kasi zaidi kuliko sasa ama wakati mwingine wowote.

Sabau za imani yangu kwa Dr. Slaa ni nyingi. Ila baadhi tu, ni kama ifuatavyo:

1. Kwa kuwa ametoka chama cha upinzani atakuwa na changamoto nyingi zaidi kuweza kushawishi wananchi kuwa kuchagua upinzani ni jambo jema na linaloweza kuleta tija, maendeleo na ufanisi mkubwa kuliko kung'ang'ania CCM

2. Usomi, hekima, busara na heshima aliyonayo vinamuwezesha kutathmini na kutekeleza kwa imani na uaminifu ahadi zake nyingi kwa ufanisi zaidi

3. Uzoefu wake katika siasa za nchi na ufahamu wa siasa zisizofaa unamfanya afae zaidi kuongoza Taifa kwa ufanisi mkubwa. Nadhani Dr. SLaa ndie kiongozi/mwanachama wa upinzania aliekaa Bungeni kwa muda wote na kwa muda mrefu zaidi kuliko viongozi wengine na sia jabau kuliko viongozi wengi sana ndani ya CCM

4. Chama chake kikiweza kujipanga na kuamua kutekeleza matakwa ya wananchi kwa uwezo wao wote, kina nafasi kubwa ya kufanikiwa sana. Kwani ni chama ambacho kina wasomi wengi, vijana na wenye ari na nia ya kuona mabadiliko chanya.

Sababu ni nyingi, lakini niahisi hizi zinatosha kwa manufaa ya mjadala huu.
 
Recta,
Nimemsoma Mwanakijiji kule ktk mada yake mpya kuhusiana na hili, kazungumzia (CHUKI) na nimegundua kwamba Mwanakijiji anazungumzia what next ktk hatua ya kwanza ambayo inakitaka chama Chadema kuweka SABABU, NIA na hatimaye kupata UWEZO wa kukiondoa chama CCM. Na huo uwezo ndio tunauomba hapa pasipo sababu. nadhani sasa hivi nimempata vizuri sana.

Pasipo SABABU watu hawawezi kuunda UMOJA ili kumwondoa CCM, na ni kutokana na sababu hiyo ndipo NIA ya kumwondoa mtu au chama madarakani hutokea hivyo nadhani kosa dogo alilofanya hapa ni kuweka hili neno what next badala ya kuuliza SABABU ambayo itajenga NIA, kwani ikumbukwe tu kwamba hata Marekani walipoweka NIA ya kumwondoa Saadam Hussein walikuja na SABABU pamoja na kwamba ilikuwa ya uongo na uzushi, sababu ambayo iliwajaza watu (HOFU -Fear) kubwa inayoweza kuzaa CHUKI (Weapon of Mass Destruction). Ingawa hawakufanikiwa sana kupata UMOJA wa nchi za kimataifa, lakini ilikuwa na nguvu kubwa ya mvuto wakawapata wachache waliohofia na wakaweka NIA.

Na hata kabla ya kuvamia Afghanstan, Marekani tena walizua tena SABABU nyingine 9/11 (Hofu) ili kuivamia nchi hiyo, hivyo waliweza kujenga NIA ya kuwasaka Al Qaeda popote walipo duniani..Sasa tofauti na Marekani au hata mageuzi ya kisiasa, Chadema imeonyesha kukerwa na Ufisadi kama walivyochukia watanzania wengine, lakini chuki hii haikuzaa NIA isipokuwa walikaa pembeni na kukubali matokeo. Leo imefika wakati wa uchaguzi mkuu, Chadema wanaonyesha NIA ya kumwondoa CCM kwa kero zake na sii chuki inayolingana na sababu kubwa wananchi wanataka kuona CCM ikitokomezwa.

Sasa ndani ya mioyo ya watu wengi wanashindwa kuunganisha picha hizi mbili..Kwa nini Chadema inataka kumwondoa CCM madarakani? ni zipi haswa sababu au ndio kutokana na mfumo uliopo kwamba imefikia wakati wa Uchaguzi, basi chama hiki kama vyama vinginevyo hawana budi wala hila isipokuwa kugombea kwa sababu ni swala la demokrasia!.

Ikiwa ndivyo basi Chadema wanaiondoa CHUKI ya wananchi, wanaaondoa pia NIA ya wananchi kujiunga ktk mapambano haya kwani pasipo sababu ya dhati ni sawa na mtumwa kubebeshwa mzigo usijue alichobeba... Waswahili wanasema wanauziwa mbuzi ndani ya gunia. Hii ndio hofu ya wengi na pengine Mwanakijiji mwenyewe anasita kuchukua silaha na kusimama msitari wa mbele kwani pasipo sababu au sababu za kizushi siku zote haziwezi kushinda vita.

Ni kweli maneno yake Mwanakijiji kwamba Marekani wameshindwa vita ya Iraq kwa sababu ile sababu ya awali ilikuwa uongo na Uzushi hivyo umoja wa Mataifa walishindwa kuungana na uongo ule usokuwa na ushahidi wakutosha, na mimi katika imani yangu naamini kabisa ukimzushia mtu jambo ambalo sii la kweli, basi hata mafanikio yake hayawezi kudumu..Na ndio maana Marekani wamejikuta wakipigana vita visivyokwisha na hatimaye nina hakika Marekani watachoka na kushindwa..Iraq itabakia Somalia nyingine, nchi iliyoharibiwa kwa matakwa ya binadamu.

Kwa hiyo, Chadema wanatakiwa kuja na SABABU ambayo itajenga NIA ya wananchi kuungana nao kuiondoa CCM madarakani na sii swala la what next..Na hakika sababu yenyewe hakuna zaidi isipokuwa UFISADI.
 
KUDOS to CHADEMA.......................kwa kumchagua Dr Slaa kuwa mgombea wa Urais wa Tanzania..........ninasema.....hii ni BIG PLUS si kwa CHADEMA TU bali hata kwa vyama vingine vya upinzani.................once again hongereni sana Watanzania................sasa ni Watanzania na goli......tushindwe wenyewe.............
 
Na wewe tuwe pamoja, usiwatakie kila la kheri tafadhali unga mkono juhudi hizi, tulete mabadiliko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…