Wadau kwa muda sasa kumekuwa kunaendeshwa kampeni kali ya kusaka michango kwaajili ya kukusanya fedha za kugharamikia matibabu nchini India ya Msanii wa filamu nchi SAJUKI ambaye kiukweli anaumwa kweli kweli..
Tunashuhudia watu mbali mbali wakitoa mchango yao kwenye kampeni hii ya nguvu, lakini hapa kuna funzo kubwa kwa wasanii wetu. kuna watu wengi nchi hii wanaumwa hoi bin taabani wapo vitandani hawana hata pesa ya kununulia asprin wapo wanasubiri kudra za Mungu tu na hakuna hata mtu mmoja anayewaza kuwachangia zaidi ya ndugu zao wa karibu ambao nao wapo hio kiuchumi
Kwanini SAJUKI au kwanini KANUMBA wapate michango mikubwa kiasi hicho?
Je wanapokuwa kwenye peack pesa zao wanatumia vipi? Na hasa kwa jamii inayo wazunguka? Natamani basi kuanzia sasa niwe nawaona wasanii hawa wakipishana kwenye vituo vya watoto yatima kutoa misaada, kutembelea mahospitali kugawa vyadarua, kusimama kampeni za malaria, uzazi wa mpango,uzazi salama na mengineyo mengi kusaidia jamii kutokana na vipato vyao na umaarufu wao.
Pamoja na kuendelea na maisha yao ya kifahari kwa kupanga majumba ya kifahari, kujirusha sana, kubadili magari na vimwana/mabuzi na tegemea sasa watakumbuka pia jamii hii wanayoipa kisogo pindi wanapokuwa juu ndio hii hurudi kuja kuiomba msaada pindi mambo yanapokuwa magumu.
Mwisho namtakia mafanikio mema bwana SAJUKI afanikiwe kwenye mtihani huu mgumu
Tunashuhudia watu mbali mbali wakitoa mchango yao kwenye kampeni hii ya nguvu, lakini hapa kuna funzo kubwa kwa wasanii wetu. kuna watu wengi nchi hii wanaumwa hoi bin taabani wapo vitandani hawana hata pesa ya kununulia asprin wapo wanasubiri kudra za Mungu tu na hakuna hata mtu mmoja anayewaza kuwachangia zaidi ya ndugu zao wa karibu ambao nao wapo hio kiuchumi
Kwanini SAJUKI au kwanini KANUMBA wapate michango mikubwa kiasi hicho?
Je wanapokuwa kwenye peack pesa zao wanatumia vipi? Na hasa kwa jamii inayo wazunguka? Natamani basi kuanzia sasa niwe nawaona wasanii hawa wakipishana kwenye vituo vya watoto yatima kutoa misaada, kutembelea mahospitali kugawa vyadarua, kusimama kampeni za malaria, uzazi wa mpango,uzazi salama na mengineyo mengi kusaidia jamii kutokana na vipato vyao na umaarufu wao.
Pamoja na kuendelea na maisha yao ya kifahari kwa kupanga majumba ya kifahari, kujirusha sana, kubadili magari na vimwana/mabuzi na tegemea sasa watakumbuka pia jamii hii wanayoipa kisogo pindi wanapokuwa juu ndio hii hurudi kuja kuiomba msaada pindi mambo yanapokuwa magumu.
Mwisho namtakia mafanikio mema bwana SAJUKI afanikiwe kwenye mtihani huu mgumu