Kasie
Platinum Member
- Dec 29, 2013
- 21,234
- 36,261
Habari za jioni waungwana.
Leo mchana nilitoka kwenda ofisi flani hivi, ni eneo la kutembea kwa miguu, nikiwa kwenye hiyo ofisi hamadi nikakutana na huyu mbaba. .... tulifahamiana miaka hiyoo wakati tuko vijana.
Sasa huyu baba mie nilimpenda sana kipindi hicho tuko waschana, ila yeye akawa ananivalia miwani myeusi. Mie na aibu zangu nikawa namezea nisubiri siku anitongoze mweeh. Hapo kati nikiwa nasubiri anianze yeye akatokea mschana flani hivi huyo mschana ni mchangamfu wale ambao alienda mahali kama ni mgeni basi dakika 10 zinazokata anakuwa mwenyeji, ni muongeaji mnoo. Huyu mschana nae alimpenda mbaba niliyempenda wakati huo ila yeye hakulaza damu akamwambia kisha wakaanza kuwa karibu. Mie roho ikaniuma nikaondoka eneo nililokuwaa naishi ili nisiwaone.
Miaka chungu tele imepita leo ndo tumekutana tena yeye ndo alinikumbuka, Kasie habari yako.... hubadiliki uko Vilevile na sura yako tangu kaschana nikacheka kisha tukasalimiana. Baada ya salamu akaniomba tukishapata huduma hapo anahitaji kuongea na mimi. Nikamwambia sawa......
Kufika eneo la tukio ananikumbushia mambo ya miaka ile kuwa aliona vile nampenda ila akiwa anataka kuniambia akatokea yule mschana akambana. Hivo anaomba tuendeleze mahaba yetu maana hata yeye hadi sasa yuko singo.... looh
Nikamwambia mambo hayo.mie nshaacha. ... akasema tuwahi kurudi mahala pa kazi ila sikiliza huu wimbo tafadhali.
Kaomba kesho tuonane tuyajenge. .... hapa nautafakari huu wimbo.....
Hajui Kasie amekuwa jasusi wa mahaba hehehehee shauri yake looh.
Kasie Matata.
Leo mchana nilitoka kwenda ofisi flani hivi, ni eneo la kutembea kwa miguu, nikiwa kwenye hiyo ofisi hamadi nikakutana na huyu mbaba. .... tulifahamiana miaka hiyoo wakati tuko vijana.
Sasa huyu baba mie nilimpenda sana kipindi hicho tuko waschana, ila yeye akawa ananivalia miwani myeusi. Mie na aibu zangu nikawa namezea nisubiri siku anitongoze mweeh. Hapo kati nikiwa nasubiri anianze yeye akatokea mschana flani hivi huyo mschana ni mchangamfu wale ambao alienda mahali kama ni mgeni basi dakika 10 zinazokata anakuwa mwenyeji, ni muongeaji mnoo. Huyu mschana nae alimpenda mbaba niliyempenda wakati huo ila yeye hakulaza damu akamwambia kisha wakaanza kuwa karibu. Mie roho ikaniuma nikaondoka eneo nililokuwaa naishi ili nisiwaone.
Miaka chungu tele imepita leo ndo tumekutana tena yeye ndo alinikumbuka, Kasie habari yako.... hubadiliki uko Vilevile na sura yako tangu kaschana nikacheka kisha tukasalimiana. Baada ya salamu akaniomba tukishapata huduma hapo anahitaji kuongea na mimi. Nikamwambia sawa......
Kufika eneo la tukio ananikumbushia mambo ya miaka ile kuwa aliona vile nampenda ila akiwa anataka kuniambia akatokea yule mschana akambana. Hivo anaomba tuendeleze mahaba yetu maana hata yeye hadi sasa yuko singo.... looh
Nikamwambia mambo hayo.mie nshaacha. ... akasema tuwahi kurudi mahala pa kazi ila sikiliza huu wimbo tafadhali.
Kaomba kesho tuonane tuyajenge. .... hapa nautafakari huu wimbo.....
Hajui Kasie amekuwa jasusi wa mahaba hehehehee shauri yake looh.
Kasie Matata.