Ya Kikwete Yamkumba Rais Magufuli

Ya Kikwete Yamkumba Rais Magufuli

Mimi nawachukia sana hawa wanaojali sana processes (utaratibu) kuliko achievements. Wengi wao utakuta wanapenda kuendeleza uvivu, uzembe, rushwa na ufujaji. MAGU ndiye mtu tunayemhitaji as long as haamuru kuminywa mapu..u kwa wapinzani!
yeah right.....mtu ukipata mali/utajiri hata kwa mauaji hakuna tatizo kwa vile utakuwa ume-"achieve" siyo?

pathetic!
 
Utamu wa mkanasha ni kujibu hoja, kutumia nguvu ya hoja kumshinda unaye debate naye, kukimbia hoja si uungwana. Tunapobadilishana mawazo hapa wengine pia wananufaika. We sema tu, wala usiogope kama unachokijua ni ukweli na kama kimetokea. Onesha matendo pia onesha sheria iliyovunjwa. Maneno matupu yasiyo na ushahidi ni majungu yaliyotamalaki na yanaonesha chuki na husuda aliyonayo mtu moyoni. Sidhani kama wewe una chuki na kijiba. Haya jibu basi tuendelee kujadiliana
acha kijiparura nipo hapa kwa minajiri ya kujibu hoja tumesema Magufuli haiheshimu sheria ya bajeti ya mwaka 2015 na haeheshimu sheria ya fedha za umma ya mwaka 2015 MAGUFULI NI JIPU anapaswa kutumbuliwa kwa kukiuka sheria hizi muhimu katika kutuletea maendeleo ya nchi kipi usichokielewa wewe nyie ndio munamjaza pumzi hewa huyo mtu wenu mwambieni kwamba kinga yake yakutokushitakiwa isimfanye akawa dictator na mvunjaji wa sheria maana hata seriklali yake ni serikali magumashi haijawa gazetted hijatangazwa kwenye gazeti la serikali wala hajatengeneza mwongozo,wa kuongoza wizara ambazo ndio zinatekeleza matumizi ya fedha
 
Maamuzi mpaka ya Bunge yanafanywa na mtu moja au wawili alafu unayabariki?
Wote (Rais na Wabunge) ni wateule wa wananchi, Rais hakutumia hizo fedha kwa ajili yake na mke wake ila amezitumia kwenye hitaji la wananchi, mimi siishi Dar ila ninaona fahari fedha hizo zimetumika kwa ajili matumizi ya wananchi wote (ujenzi wa barabara za Dar na Mwanza).
Ningemuunga mkono Mbowe na wenzake endapo hizo pesa zingekuwa zimetumika kwa ajili ya pampers za watoto wake, kwa hili nawashauri wapinzani watulie, tunawacheka na hawatuwakilishi.
 
Sasa ukweli wa kinachoitwa 'upinzani' kinaonekana. Hawa wanataka kutuchelewesha tu. Hakuna aliyekuwa akijali vipengee hivi kama JK pamoja na maovu yote yaliyotokea mbona bunge halikuweza kumdhibiti. Haihitaji elimu kubwa kuona kwamba MAG anafanya kwa manufaa ya wananchi. Upinzani sasa ni wazi wanagombea mlo, kwani walikuwa wakinyofolewa kitu katika hivi vijisenti senti !
mkuu nchi haiendeshwi kwa Utashi wa mtu. Kiongozi lazima aeshimu katiba, sheria na taratibu zilizoko katika nchi ili kuondoa substandards.
 
Je utamtoa mwanapunda wako aliyetumbukia kisimani siku ya sabato? Kuna Muda ili mambo yaende busara inabidi itumike
 
hii issue ukiijadili kwa mizuka ila ukijadili bila kua biased upande wowote utagundua kua tunapoteza fedha nyingi kulipa wabunge ambao hawafanyi kazi yao inayowapasa kufanya kikatiba anachokifanya mbowe ni ukweli usiopingika ila kwa kua wananchi tuna mizuka acha twende ivi ivi
mwelewa atanielewa namaanisha nn ila kama sio mwelewa kula kona....
 
Kama wametoka nje kwa issue ya bunge kuwa live hapo Sawa lakini kwa hilo la ubanaji wa matumizi na fedha kuelekezwa kwenye shughuli za maendeleo naona upinzani wanajiharibia
 
Bunge kuwa ''live'' ni muhimu ili kuona kama wabunge wa CCM na ''Upinzani'' wanafanya kazi tuliyowatuma kuisimamia serikali kikamilifu.

Maana utendaji wa wabunge iwe ''utoto'' kama CCM wanavyosema kuhusu hatua za UKAWA kuibana serikali Bunge ni sisi wananchi tutawasaili wabunge kama wanatekeleza kazi zao wakati wa vikao vya Bunge au la.

Serikali haiwezi kuwachagulia wananchi ''kipi'' cha kilichotokea Bungeni wakione ktk TV usiku wa manane.
Hivi hizi habari umezipata live?
 
nyerere alituambia kiongozi yeyote anayevunja katiba hatufai. kama rais anaisaliti katiba nini zaidi atashindwa kukisaliti?
 
Leo ndio nimejiona nyumbu kabisa! Sitarudia tena kuzungusha mikono, hawa ndio niliwapa kura yangu? Mbowe unaona bora safari za kamati za bunge kuliko madawati?
GT wa sikuhizi ni hatari! unaelewa maana ya katiba ya nchi?
 
Wote (Rais na Wabunge) ni wateule wa wananchi, Rais hakutumia hizo fedha kwa ajili yake na mke wake ila amezitumia kwenye hitaji la wananchi, mimi siishi Dar ila ninaona fahari fedha hizo zimetumika kwa ajili matumizi ya wananchi wote (ujenzi wa barabara za Dar na Mwanza).
Ningemuunga mkono Mbowe na wenzake endapo hizo pesa zingekuwa zimetumika kwa ajili ya pampers za watoto wake, kwa hili nawashauri wapinzani watulie, tunawacheka na hawatuwakilishi.
Tunachosema mfumo upi wa sheria ulifuatwa ambao ni Bunge la bajeti
 
kuna hoja ya msingi hapa.

Hapa namsifu sana Mh Mbowe kwa kunukuu vifungu vya katiba na sheria vilivyovunjwa. Nilisikitika na ninaendelea kusikitika kuwa wakati yeye Mbowe na wenzaka wakimtaka Rais wa JMT JPM aingilie Zanzibar baada ya uchaguzi wa Oktoba hawakunukuu hata tone la kifungu cha katiba wala sheria inayomruhusu rais wa JMT kuingilia uchaguzi wa Zbar ambao kikatiba imeorodheshwa mioingoni mambo ya ndani ya Zenji.
 
Mimi nawachukia sana hawa wanaojali sana processes (utaratibu) kuliko achievements. Wengi wao utakuta wanapenda kuendeleza uvivu, uzembe, rushwa na ufujaji. MAGU ndiye mtu tunayemhitaji as long as haamuru kuminywa mapu..u kwa wapinzani!

Much of the reported achievements are just cosmetics. Wanayapamba sana kuliko uhalisia. Tuliona kwenye elimu na kilimo kwanza kwa mfano!
 
Mimi nawachukia sana hawa wanaojali sana processes (utaratibu) kuliko achievements. Wengi wao utakuta wanapenda kuendeleza uvivu, uzembe, rushwa na ufujaji. MAGU ndiye mtu tunayemhitaji as long as haamuru kuminywa mapu..u kwa wapinzani!
Kuna haja gana kufanya jambo sahihi in a wrong way wakati unaweza kulifanya kwa njia sahihi? Tujifundishe kufanya mambo in a civilized way kuliko anavyo fanya sasa.
 
JP akumbuke kwamba hao wengine ambao anawaita majipu au wezi sio kwamba walichukua pesa wakaweka mfukoni mwao bali walifanya vitu vya manufaa ya wananchi na vingine vinaonekana lakini kwa sababu hawakufuata kanuni au sheria za fedha CAG au mamlaka nyingine zilipokagua zikaona huo ukiukwaji, ndio hao akiletewa taarifa anawatumbua. Hivyo na yeye asifanye hayo ya kukiuka sheria za fedha kwa sababu yeye ni Rais hata kama nia yake ni njema

Mbona hausemi sheria gani zimekiukwa, unabaki kusema tu kakiuka sheria? Wewe hio sheria unazijua au unaishia kuambiwa tu wanasiasa? unawaamini vipi wanasiasa waliowahi kukuambia huyu ni fisadi na wakaitoalist of shame halafu wanasiasa wale wale leo wako na wale waliowataja kwenye list of shame huku waki wa endorse na kuwasifia nchi nzima? Usimtegemee mwanasiasa kukwambia ukweli.Utafute ukweli. Sheria zipo kwa kingereza na kiswahili. Jisomee sheria ya fedha za umma ya mwaka 2001,soma katiba,hautapata tabu kujua nani mkweli na nani laghai.Usiamini kuwa unajua, tafuta maarifa zaidi.
 
Haya Ndio matumizi mabaya ya madaraka. Watanzania ni wepesi kusahau tumesahau Meri, Nyumba za Serikali, Boti za Azam kwa kuwa yeye ni msema mkweli na mtumbuaji majipu.
 
Back
Top Bottom