Tuwe wakweli,hivi zile traffic light pale Chato zimewekwa kwa kazi gani haswa?Hakukuwa na sababu za kuweka traffic light eneo ambalo zinaweza kupita hadi dk 20 bila kuona gari likipita hapo.Hata hivyo taa hizo haziwezi kuwa kitu cha kujivunia,Wilaya ya Chato kama zilivyo wilaya nyingine,ni moja ya wilaya zilizo na umaskini wa kutupwa.
Ukiiacha chato mjini ambako mh.amejitahidi kuwekeza kwa kujenga nyumba za wageni,mahiteli na bar,maeneo mengine ya wilaya hiyo yapo duni sana.Wakazi wengi wa wilaya ya Chato wanajishughulisha zaidi na Kilimo pamoja na uvuvi wa samaki katika mwambao wa Ziwa Victoria.Vijiji kama Bwanga,Bukiriguru,Busaka,Makurugusi,Nyakato,Musasa,Mabira,Buzirayombo,Kankanshe,Muganza,Nyabugera na maeneo yote yanayouzunguka meambao wa Ziwa,wakazi wake ni watu duni ambao kamwe hawawezi kujivunia uwepo wa Traffic light kama suluhisho la matatizo ya kiuchumi waliyonayo.
Unaonekana ni mtu unayeongozwa na mizuka zaidi kuliko uhalisia,kama wewe ni mwana Chato,ulipaswa kuguswa na hali duni ya maisha waliyinayo wanachato kuliko kushangilia mambo madogo ambayo hayajawahi kuwa suluhisho kwa wakazi wa Chato.
Au mwenzetu hujuwi uwekezaji wa mkubwa pale Chato?Unafikiri ni watu wa kawaida waliowekeza pale Chato?Pole sana.Wana Chato watabaki kujivunia "urahisi" wa mukulu tu,zaidi ya hapo watatakiwa wajikite zaidi katika Kilimo na uvuvi ili wapate mkate wao,kitu pekee ambacho wanaweza kukipata bure japo ni kwa msimu ni T-shirt,kofia,kanga na chumvi toka ccm.Kujivunia traffic light ni upumbavu wa kiwango kikubwa kinachoweza kutweza weledi wa jukwaa hili.Jaribu kuuficha upumbavu wako.
Je,mwananchi wa Chato anayekula kwa kukamata kambale kwenye majaruba ya mpunga wanaweza kujisifia eneo hili?
View attachment 341848
Au anahisa kiasi gani kwenye hotel ile iliyo pembezoni mwa jengo la halmashauri ya wilaya ya Chato?Acha kujisifia upumbavu,tajili na Mali zake,maskini na watoto wake,kukaa kijiweni kutwa nzima kujisifia ukwasi wa wakubwa ni upumbavu zaidi ya upumbavu wenyewe,au nawe ni miongoni wa wale vijana wanaochunga ng'ombe na farasi wa mheshimiwa? Maana wachungaji wale wanaishi ghorofani,yawezekana kitendo cha kuishi ghorofani na kutunza mifugo ya mzee kimekufanya nawe ujihesabie haki kuwa na wewe ni mwana wa mfalme.
Acha mahaba ya kipumbavu,jaribu kuwa na huruma ya kiutu,jenga hoja zako kwa kuzingatia mazingira yako(Chato),usijenge hoja kwa kuegemea kwa jirani yako,vya jirani siyo vyako.