X wangu kaniambia nimemroga!

X wangu kaniambia nimemroga!

Huyu alikuwa mchumba wangu ambaye nilimpenda sana na tulikubaliana kuoana. Nilipatwa na matatizo njiani mwenzangu akanambia anaolewa na mtu mwingine (tulikuwa tunaishi mikoa tofauti). Niliumia sana na kutokana na hasira nikamwambia `Tutaona kama utaishi na huyo mwanaume.' Toka hapo sijawahi kuwasiliana naye tena!

Siku za karibuni alinitumia message kwamba anaomba kuongea na mimi, nikamtajia muda ambao ntakuwa free.
Muda huo akanipigia simu na kuanza kunilaumu `@nyalotsi kwanini umenifanyia hivi?'
Nikamuuliza, nimfenyaje?(huku nikiwa na mshangao)
`Umeniroga kila nikipata mimba inatoka, tafadhali sana nisamehe kama nilikukosea! Familia yangu itavurugika.'

Nilikata simu na kuanza kutafakari mambo mengi sana. Ina maana huyu dada kaniona mi mchawi? Mbona hata mizizi ya dawa za kawaida tu siifahamu? Hii laana gani tena? Baadaye nikakumbuka niliwahi kumtishia kwamba hataishi kwa amani na mumewe. Nikampigia simu na kumhakikishia kwamba siwezi kufanya kitu hiyo na wala sio muumini wa mambo hayo.
Nikamshauri pia waende na mumewe hospitali kufanyiwa uchunguzi wa kiafya na wataalamu.!

Kweli duniani kuna mambo!!
Mkuu Nyalotsi,
  1. You have the powers!. Umezitumia negatively!. Nenda kanisome HAPA! ili ujue jinsi ya kuzitumia positively.
  2. Unaweza kujikuta ni kweli wewe ndie uliyemlaani!, kuna kitu kinaitwa "curse" laana!. Huyo dada amehangaika sana kutafuta mtoto, ana alikwenda kwa waganga fake, alipofika kwa mganga wa ukweli mwenye insight, akaangalia kwa jicho la tatu, jicho la ndani, jicho la roho, akaliona tatizo, akamwambia, dada akakutafuta!.
  3. Matatizo ya uzazi naturally huwa yapo, ila pia curse nazo huwa zipo, hivyo cha kufanya, ni kwa wewe kwanza riverse yale maneno mabaya uliyotamka, msamehe kwa dhati toka ndani ya moyo wako, wish her all the best, mtubie Mungu kuwa hukujua kilichotokea wala hukudhamiria kumdhuru ila ni powers zilizoko ndani yako ndizo zilizoyafanye hayo.
  4. Uatafunguka na atapata mtoto!.
Pasco.
 
coincidence! it happens.
Kwenye ulimwengu wa mwili, ndiko kwenye coincidence!, kwenye ulimwengu wa roho, hakuna coincidence!, kila kinachotokea, kilikuwa kitokee hivyo hivyo kitavyotokea!, every move, every action, every occorunce its all a pre meditated moves, kilikuwa kitokee!.

Pasco.
 
Mmm ngoja nikauze nyumba yangu ya gongolamboto kisha nije nipate hiyo ya mgando na pembeni.Lakini 7 utahimili? Naona msiba unautaka wewe maana nina guu la mtoto utaliweza???

hilo guu la mtoto liongeze kidogo halafu hizo saba kwani umesikia mimi mwanafunzi,fanya 10 na cha 11 cha kukuagia..uje tu umeshiba
 
hamna lolote ni coincidence tu! Siku moja nilikuwa ofisini kwangu nafanya kazi, nakumbuka siku hiyo nilikuwa busy kupita maelezo, mpaka mchana wa saa8 sijatia kitu mdomoni wala kukaa. Akaja bwana mmoja kuchukua pesa, zile pesa nilkuwa nimeshazipanga kabisa ziko pembeni kwenye bahasha ndani ya draw, nina uhakika wa asilimia mia kuwa zilikuwa zimetimia, basi yule jamaa alipoingia tu akakuta nina purukushani vibaya mno akabaki amesimama kama dk kadhaa maana hata viti vilikuwa vimejaa, baadaye akanigutusha tu akasema "mkuu"..nilivoinua macho nikasema "daah, sorry kaka nimekuweka" nikachukua bahasha na kumpa, hakuhesabu pale akaondoka, dk kadhaa akarudi mbiao "samahani kaka hazijatimia"...what?.."kweli kaka"...hiyo pesa nimehesabu kwa umakini sana haiwezekani ipingue (nadhani yeye alivonikuta busy vile alijua nitajichanganya, kumbe ile pesa mimi nimeiweka kitambo kabla hata kazi hazijanitinga), nikamuuliza sh ngapi, akataja....mo way, thats too much siwezi kuchanganya kiasi hicho! akakomaa, nikajikuta kitu kimenipanda kwenye nafsi kimenikaba, nikafungua droo nikachomoa pesa nikampa huku nasema kwa mzuka wa hali juu "KAMA HII PESA NAYOKUPA SIYO HAKI YAKO UTAPOTEZA PESA NYINGI NDUGU YANGU NAKWAMBIA", Jamaa akachukua pesa akaondoka. Baada ya siku kadhaa nikaambiwa na jamaa yangu mwingine, "mbona yule jamaa anakusema vibaya, umechukua pesa yake kimazingara"...dafuq!!!!!? coincidence

siku nyingine tena niko ugenini nikakodi taxi, nikazunguka kidogo nikaingia kwenye ofisi fulani nikamwambia aningoje, muda kama wa saa moja hivi, nilivotoka nikamwambia aniache sehem, karibu tu, nauliza bili akaniambia elfu50...khaaa! bei ya kukodi siku nzima mkoa ule naijua vizuri ni elfu 80 mizunguko ya kawaida na mafuta kwake, huyu nikihesabu haizidi kilometa tano, na muda tuliotumia ni kama saa moja na nusu kuwa naye (mostly waiting), kwa mzunguko ule nisingekuwa na mzigo ningekuwa nimefanya kwa miguu tu! Akakomaa, hasira zikanipanda, nikamwesabia 50 nikawa nimeropoka..."UNAFIKIRI UTATAJIRIKA NA HIYO 50, ITAKUTIA UMASKINI, NDIYO NIMEKWAMBIA HIVYO"!....Loh, kama sjui nini, kesho yake napita mitaa fulani nikamkuta yuko garage, nikamsalimia akaanza kulalamika "KWELI KAKA NDIYO TUNAFANYIANA HIVI KWA AJILI YA VITU VIDOGO TU".....LOH! coincidence.
kuna vitu vinaweza kukutia kwenye mazingira magumu sana bila kukusudia, na watu inakuwa ngumu sana kukuelewa, lakini basi tu inatokea kama bahati mbaya!
Mkuu Cyberteq!, you have the powers!.

Nenda kanisome HAPA ujue how to put them in a good use!.

Pasco
 
Hivi unajua maneno yanaumba? Hivi unajua shetani anatumia maneno ya binadamu kupitishia laana zake? Inawezekana havihusiani but inawezekana pia laana uliyoapiza kwake ndio inamuathiri...
Nakushauri tu ufanye utaratibu wa kuifuta hiyo laana kwa mwenzio. .. msaidie kwa hilo

Hilo nalijua aisee, hayo mambo niliyaongea nikiwa na hasira. Alinivuruga sana kipindi kile mpaka nikavurugika akili.
 
CYBERTEQ;9360206 siku nyingine tena niko ugenini nikakodi taxi said:
Kweli mkuu faida ya dhuruma Mungu huipiga kofi ogopa dhuruma na udanganyifu imewacost wengi.".......apandacho mtu ndicho atakachovuna"
 
Ndio umemloga kweli kwani maneno huumba.Mkuu acha uchawi kwa jina la YESU! Vipi na kuruka na ungo unaweza? kwa maana nataka niende London.

duh, mkuu hata dawa ya kujikinga sijawahi kuisikia. Mi nilisema tu kwa wakati na nilishasahau kwamba nilimwambia hivyo.
 
Kaka neno ulilolitumia lilikua ni kali sana...na kam unavyojua kuna viumbe wewe huwaoni akina mashetani...wakati wewe unoangea walilisikia ilo neno...wao wakaingia kati ili kukutengenea Fitna ya kuonekana kua wewe ni mchawi....ushauri uliowapa ni mzuri sana...kwa hio wache waende hospitali ili wajue kama ana tatizo la kiafya(biological problem)...ama kwa dawa za kiimani utawashauri kwa mujibu wa dini yao...kama ni waislam basi wanaweza kuchukua Maji atayasugulia majani ya mkunazi,majani ya mbaazi na mjani ya mpera na kuyasomea Surat-Mariam(7),Surat Raad(21),Surat Zilzala-Sura ya tetemeko(313),Surat-l-fiil=sura ya Tembo(313)...na takua anakunywa mara tatu kwa siku mara tu atakapojisikia amebeba uja uzito...Katuka mambo ambayo majini hufanya ni kuzila zite foetus zinapokua zinatunga kwenye tumbo la mama..
 
Kiukweli ulimlaani japo inaweza isiwe sababu ya masahibu yake. Muambie umemsamehe kabisa kwa kukuumiza, na utubu kwa Mungu na kukiri kwa sala kuwa umemsamehe. Hii mammbo ya kuumiza nyoyo za watu can be haunting.

Masaibu yake yana sababu zake bhana. Mimi huwa naamini ni mzazi wako tu ndiye anayeweza kukulaani. Mwingine atakuloga tuu!!
 
kaka umenena yaan ili mwanamke asepe kiroho safi ampe jamaa mpk aridhike ndo amruhusu vzr

Ha,ha itabidi nimwambie dawa ya uchawi niliomuwekea inabidi anipe kazi kwanza eti eeh!
 
Kaunga huwa hana comment za kitoto hivi, Kaunga eti hii ni ID yako nyingine mkuu?

Hahahah, kwamba ulikuwa unanijibu mimi eeh.
Duh hata kama ni usanii siwezi kumiliki personality tofauti hivi nisichemshe
 
Last edited by a moderator:
una "natural anciety witches in your body" "mtaje jina then zungumza kwa mkazo "fulani" sasa umepona"ninakuachia na sasa upo huru zaa watoto salama

sifanyi kazi hiyo aisee na sina nguvu hizo za Giza unazoamini wewe. Mimi naamini Mungu yupo na kila binadamu ana majaribu yake. Ukiamini uchawi na mwisho wako
 
Mmh pole umenikumbusha mbali Sana.
Nakumbuka nilikuwa na bf those years back. Nilimpenda kuliko hata nafsi yangu. Basi imeendaa akawa na mtu pembeni bila mi kujua. Kuna siku ikatokea huyo dada ajanitumia sms ya kunikashfu sana. Nikamwambia jamaa akabisha kuwa na uhusiano nae na hapo relationship ilikuwa imeshakuwa official kwao na kwetu.. nilikuwa nalia day and night. Nimejibembelezesha kwa jamaa wapi... baada ya miezi kibao ya kuumia nikasema enough is enough nikakata mawasiliano but kwa kumwambia maneno mabaya Sana like you will never be happy...hutafanikiwa etc etc.

Mmmmh baada ya two years nikasikia jamaa yupo vibaya mno kiuchumi...pia hana relationship stable kabisa.

Kuna siku bahati mbaya Sana si nikakutana nae bhana mahali....mmh nilichoka kabisa maana akaniambia kila anachofanya hajafanikiwa.La ajabu eti anasema eti ooh naomba ukubali nikuoe siwezi pata mtu kama ww.

I was like are you a nut case!!!
Sijaeleza yote asije akawa yupo humu akajua buure but no mengi na mabaya alinifanyia....
 
Hahahah, kwamba ulikuwa unanijibu mimi eeh.
Duh hata kama ni usanii siwezi kumiliki personality tofauti hivi nisichemshe

nilitaka kushangaa mkuu! lumbe siyo wewe ni mjusi tu anapita kwenye msafara wa mamba.
1 perfect love.
 
Mmh pole umenikumbusha mbali Sana.
Nakumbuka nilikuwa na bf those years back. Nilimpenda kuliko hata nafsi yangu. Basi imeendaa akawa na mtu pembeni bila mi kujua. Kuna siku ikatokea huyo dada ajanitumia sms ya kunikashfu sana. Nikamwambia jamaa akabisha kuwa na uhusiano nae na hapo relationship ilikuwa imeshakuwa official kwao na kwetu.. nilikuwa nalia day and night. Nimejibembelezesha kwa jamaa wapi... baada ya miezi kibao ya kuumia nikasema enough is enough nikakata mawasiliano but kwa kumwambia maneno mabaya Sana like you will never be happy...hutafanikiwa etc etc.

Mmmmh baada ya two years nikasikia jamaa yupo vibaya mno kiuchumi...pia hana relationship stable kabisa.

Kuna siku bahati mbaya Sana si nikakutana nae bhana mahali....mmh nilichoka kabisa maana akaniambia kila anachofanya hajafanikiwa.La ajabu eti anasema eti ooh naomba ukubali nikuoe siwezi pata mtu kama ww.

I was like are you a nut case!!!
Sijaeleza yote asije akawa yupo humu akajua buure but no mengi na mabaya alinifanyia....

Kwa hiyo unamaanisha kauli yako ndiyo ilibadilisha mkondo wa maisha yake?!!
 
Back
Top Bottom