hamna lolote ni coincidence tu! Siku moja nilikuwa ofisini kwangu nafanya kazi, nakumbuka siku hiyo nilikuwa busy kupita maelezo, mpaka mchana wa saa8 sijatia kitu mdomoni wala kukaa. Akaja bwana mmoja kuchukua pesa, zile pesa nilkuwa nimeshazipanga kabisa ziko pembeni kwenye bahasha ndani ya draw, nina uhakika wa asilimia mia kuwa zilikuwa zimetimia, basi yule jamaa alipoingia tu akakuta nina purukushani vibaya mno akabaki amesimama kama dk kadhaa maana hata viti vilikuwa vimejaa, baadaye akanigutusha tu akasema "mkuu"..nilivoinua macho nikasema "daah, sorry kaka nimekuweka" nikachukua bahasha na kumpa, hakuhesabu pale akaondoka, dk kadhaa akarudi mbiao "samahani kaka hazijatimia"...what?.."kweli kaka"...hiyo pesa nimehesabu kwa umakini sana haiwezekani ipingue (nadhani yeye alivonikuta busy vile alijua nitajichanganya, kumbe ile pesa mimi nimeiweka kitambo kabla hata kazi hazijanitinga), nikamuuliza sh ngapi, akataja....mo way, thats too much siwezi kuchanganya kiasi hicho! akakomaa, nikajikuta kitu kimenipanda kwenye nafsi kimenikaba, nikafungua droo nikachomoa pesa nikampa huku nasema kwa mzuka wa hali juu "KAMA HII PESA NAYOKUPA SIYO HAKI YAKO UTAPOTEZA PESA NYINGI NDUGU YANGU NAKWAMBIA", Jamaa akachukua pesa akaondoka. Baada ya siku kadhaa nikaambiwa na jamaa yangu mwingine, "mbona yule jamaa anakusema vibaya, umechukua pesa yake kimazingara"...dafuq!!!!!? coincidence
siku nyingine tena niko ugenini nikakodi taxi, nikazunguka kidogo nikaingia kwenye ofisi fulani nikamwambia aningoje, muda kama wa saa moja hivi, nilivotoka nikamwambia aniache sehem, karibu tu, nauliza bili akaniambia elfu50...khaaa! bei ya kukodi siku nzima mkoa ule naijua vizuri ni elfu 80 mizunguko ya kawaida na mafuta kwake, huyu nikihesabu haizidi kilometa tano, na muda tuliotumia ni kama saa moja na nusu kuwa naye (mostly waiting), kwa mzunguko ule nisingekuwa na mzigo ningekuwa nimefanya kwa miguu tu! Akakomaa, hasira zikanipanda, nikamwesabia 50 nikawa nimeropoka..."UNAFIKIRI UTATAJIRIKA NA HIYO 50, ITAKUTIA UMASKINI, NDIYO NIMEKWAMBIA HIVYO"!....Loh, kama sjui nini, kesho yake napita mitaa fulani nikamkuta yuko garage, nikamsalimia akaanza kulalamika "KWELI KAKA NDIYO TUNAFANYIANA HIVI KWA AJILI YA VITU VIDOGO TU".....LOH! coincidence.
kuna vitu vinaweza kukutia kwenye mazingira magumu sana bila kukusudia, na watu inakuwa ngumu sana kukuelewa, lakini basi tu inatokea kama bahati mbaya!