Wosia wa Ballali kuwaumbua wengi!

Jamani na wale dada zake je?watakuwa kweli hawana data kamili??mbona walisema watakapo tua tu toka US watamwaga kila kitu.....na hakuna mtu aliye karibu ambaye anaweza kuziibadoc. hizo na kuzimwaga hapa??
 
Kuna fununu kuwa Balali alifanya mahojiano na Tanzania Daima mwaka jana huko US.Tanzania Daima walikuwa tayari kuyaprint,wakaingiliwa na UWT...wakachimbwa mkwara mzito sana na matokeo yake it has gone mum till today.Lakini inasemekana ipo na kuna siku itaibuka tu.
 
Dada zake hawana kitu cha kusema kwani nina uhakika mkapa alipokwenda huko alihakikisha hakuna kitu kitakachosemwa baada ya balali kufa na walikuwa wanajua kuwa balali atakufa kwa muda walimpangia kabla kamati haijamaliza muda wake ili waseme hatukuweza kumuhoji balali kwani amekufa kabla hatujamtafuta.

Mkono hawezi kusema kweli hata kidogo kwani na yeye anamalipo aliyopokea yasilingana na sheria za BOT, ni mmoja wao, lakini kama uko mikononi mwa watu zaidi ya mmoja, one day and very soon tutaupata na kuubandika hapa.

Serikali bado inaendelea kufanya madudu yaleyale yaliyoanza wakati balali anaumwa, wamezuia watu kuingia kwa mama yake boko lakini wakiulizwa wanasema hawausiki lakini wale walinzi wasema clear kabisa kuwa BOT imewaweka pale na hakuna kuruhusu mtu yeyote mpaka awe na kibali cha BOT je kama haikuwaweka pale kwanini mtu akiwa na kibali cha BOT anarusiwa kuingia bila tatizo au familia ndo iliagiza kuwa watu wapewe kibali na BOT. Leo walinzi wanasema wameambiwa wasiseme kuwa wamewekwa na BOT bali familia, hata kampuni waliyotoka hawataki kusema.
 
Kuna fununu kuwa Balali alifanya mahojiano na Tanzania Daima mwaka jana huko US.Tanzania Daima walikuwa tayari kuyaprint,wakaingiliwa na UWT...wakachimbwa mkwara mzito sana na matokeo yake it has gone mum till today.Lakini inasemekana ipo na kuna siku itaibuka tu.

tehe tehe tehe Bw. Absolum Kibanda alitishiwa nyau na UWT? hii tena....
 
Hata hivyo, inaelezwa kwamba wapelelezi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) walikwisha kuchukua nyaraka zote muhimu ikiwa ni pamoja na kadi ya benki iliyotumika kufungulia akaunti tawi la Azikiwe, ikiwa na picha na saini za wahusika wote muhimu kwa uhakika zaidi

Yani kama naiona vile report ya EPA haita kuwa na maajabu kabisa, kama takukuru walichukua nyaraka zote, na hosea ni member wa kamati inayochunguza EPA na ndie yuleyule alie itetea richmond

Tusubiri kudanganywa tuu....
 
Waraka huo ambao kwa sasa unatafutwa kwa udi na uvumba unadhihirisha kuwapo kwa usiri mkubwa ndani ya Serikali kutokana na baadhi ya wahusika muhimu wanaotajwa na Ballali kutozungumzwa popote linapozungumzwa suala la EPA na hata katika vyombo vya habari

Mkulo alikwenda US kumtafuta Balali ingawa "alimkosa"

Mkono alikuwa na maongezi na mazito sana na Balali masaa 24 kabla ya kifo chake huko US

Pika SItta alitaka kwenda US, akaghairi baada ya kumtuhumu makinda kuwa ni mkurupukaji

Wakamalizia makachero walioenda US kumsaka Balali
 
Wanaendelea kutuzingua tu, si watoe huo waraka?

Kama waraka huo upo kweli naamini Mbowe ni mmoja kati ya watu walio nao.

CHADEMA mna kazi kweli na huyu mheshimiwa maana ni ngumu sana kwake kutofautisha mambo ya chama na familia. Mimi naamini hiyo ndio weakness kubwa ya Mbowe.

Hii mambo ya EPA na Ballali angewaachia CCM wajimalize wenyewe na Dr. Slaa akiwa upande wa sisi wanyonge.

Najiuliza hivi spinning yote hii ya nini? Kama waraka upo, basi utoeni vinginevyo kaeni kimya kama mlivyokaa kimya wakati Ballali alipokuwepo.

Story nzima hii haimweki Ballali vizuri maana kukaa miezi tisa na siri nzito na kusubiri mpaka afe ndio itoke ni cowardice ya hali ya juu mno.

Laiti angewakabili mafisadi, Ballali angelikufa kama shujaa wa Watanzania, lakini sasa kazidiwa hata na vijana kama akina Zitto wakati yeye alikuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kutusaidia kuitengeneza Tanzania yetu.

Kibaya eti anawaachia siri watu kama akina Mkono, hivi kweli Ballali alikuwa anasoma alama za nyakati?

Mimi ninashindwa kushangaa maana hii imezidi kiasi!
 
Mkuu kinachohitajika hapa ni waraka kwani hata waliouchukua ni MAFISADI?

Kama ni MAFISADI basi watwambie. Balali tayari kafariki kaacha maandishi kwa nini yasitoke?

Inawezekana labda waraka umeisha rudi ulikotoka(Kwa mafisadi)
 
Kama maandiko ya raia mwema ni sahihi, basi wosia wa Balali upo kwenye mikono salama, na huyo wakili atakuwa si Nimrod kwani wakili anayetajwa ni wakili ambaye hajawahi kuhusishwa na mambo ya BOT. Huu wosia unaonekana kuwa na mambo mazito sana. No wonder makachero walitumwa huko USA na mission haikuwa kumleta Balali bali ku block huo wosia.
 
Wanaendelea kutuzingua tu, si watoe huo waraka?

Kama waraka huo upo kweli naamini Mbowe ni mmoja kati ya watu walio nao.

CHADEMA mna kazi kweli na huyu mheshimiwa maana ni ngumu sana kwake kutofautisha mambo ya chama na familia. Mimi naamini hiyo ndio weakness kubwa ya Mbowe.

Hii mambo ya EPA na Ballali angewaachia CCM wajimalize wenyewe na Dr. Slaa akiwa upande wa sisi wanyonge.

Najiuliza hivi spinning yote hii ya nini? Kama waraka upo, basi utoeni vinginevyo kaeni kimya kama mlivyokaa kimya wakati Ballali alipokuwepo.

Story nzima hii haimweki Ballali vizuri maana kukaa miezi tisa na siri nzito na kusubiri mpaka afe ndio itoke ni cowardice ya hali ya juu mno.

Laiti angewakabili mafisadi, Ballali angelikufa kama shujaa wa Watanzania, lakini sasa kazidiwa hata na vijana kama akina Zitto wakati yeye alikuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kutusaidia kuitengeneza Tanzania yetu.

Kibaya eti anawaachia siri watu kama akina Mkono, hivi kweli Ballali alikuwa anasoma alama za nyakati?

Mimi ninashindwa kushangaa maana hii imezidi kiasi!

Alishindwa hata kumuiga mwenzie yule mkurugenzi wa TANESCO bwana Indrisa Rashidi
 
Yangu Macho.. Tumepiga keleee weee hakuna kitu bwana. JK yupo zake Japan anakula raha Mafisadi wengine wapo wanednelea kutanua tu hapa TZ tunawaona. Hakuna cha wosia wala nini Picha imeungua
 
Mtanzania,

sidhani kama ni sahihi kusema Balali alikuwa coward,tukumbuke kuwa yeye hakuwa na moyo wa chuma,na ikizingatiwa kuwa alikuwa amezungukwa na mbwa mwitu kila kona waliotaka nyama hapo BoT na mabo baada ya kula nyama wasingekubali kuona akiwa huru.Hata ingekuwa wewe sidhani ungekuwa na ujasiri wa kupambana,kwangu mimi ni nafuu ameacha maandishi ambayo angalau yatatupatia...tusimfanye Balali kuwa exceptional human being ambaye hatishiki na umafia na ujambazi wa mafisadi jamani,kuna wangapi ambao wameshindwa kuacha hata maandishi tu?Cha muhimu tusubiri hizo documents...

that said I can guess nani anaweza kuwa miongoni mwa wanasiasa wawili wenye ushawishi waliomlazimisha Balali kutoa hizo pesa ambao hawatajwi katika EPA,Kingunge Ngombale Mwiru lazima yumo tu maana anajulikana kwa umafia wake.
 
Hatimaye sasa imethibitishwa kuwa ni kweli Mkono, alikuwepo US katika kipindi fulani mwezi wa April, kwa sababu kuna mpaka interview ninayo sasa aliyoitoa kwa gazeti moja nchini kuhusu malipo yake aliyolipwa na BOT ya shillingi Billioni 7.9, aliifanya hiyo interview akiwa US, hii ni kubainisha habari kuwa alikwenda na kukutana na Marehemu kwa masaa karibu 24, ambako inasadikiwa alimkabidhi mikoba yote muhimu ya uporaji wa mapesa yetu wananchi, pole pole tutawafikia tu wote watinge kwenye sheria ya wananchi!

Huu mchezo ndio kwanza umeanza!

.....yaani FISADI Mkono kapewa fimbo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!........basi tena tuisahau hii EPA
 
Wosia wa nini tena? Hata kama kuna la maana humo tutaishia kuunda tume nyingine ya akina Hosea kuuchunguza. Kinachohitajika ni mafisadi kufikishwa mahakamani tu, maana wanajulikana. Kwanza inawezekana vipi ushahidi wenye manufaa kwa watanzania uandikwe na balali? Kana kwamba haitoshi, anao Mkono, na Huyo Mkono ndio aufikishe katika Hadhara ya watanzania? Tuendelee kudanganyika!
 
Waraka huo ambao kwa sasa unatafutwa kwa udi na uvumba unadhihirisha kuwapo kwa usiri mkubwa ndani ya Serikali

According to the dataz....ni kwamba Balali ameacha info nyingi sana licha tu ya makaratasi, kuna videos mpaka tape recorders ambazo mkono hakupewa, kwa hiyo kwenu mafisadi ni waste of time kujaribu kuyazima makaratasi,

Mkono alikuwa ni mwanasheria wa binafsi wa Balali, according to the info, sasa kama ni kweli hivi hakuna sheria ya taifa letu iliyovunjwa hapo, kwa sababu Mkono pia alikuwa akiifanyia kazi za ki sheria BOT, ambayo Balali alikuwa gavana?
 
Mtanzania,

sidhani kama ni sahihi kusema Balali alikuwa coward,tukumbuke kuwa yeye hakuwa na moyo wa chuma,na ikizingatiwa kuwa alikuwa amezungukwa na mbwa mwitu kila kona waliotaka nyama hapo BoT na mabo baada ya kula nyama wasingekubali kuona akiwa huru.Hata ingekuwa wewe sidhani ungekuwa na ujasiri wa kupambana,kwangu mimi ni nafuu ameacha maandishi ambayo angalau yatatupatia...tusimfanye Balali kuwa exceptional human being ambaye hatishiki na umafia na ujambazi wa mafisadi jamani,kuna wangapi ambao wameshindwa kuacha hata maandishi tu?Cha muhimu tusubiri hizo documents...

that said I can guess nani anaweza kuwa miongoni mwa wanasiasa wawili wenye ushawishi waliomlazimisha Balali kutoa hizo pesa ambao hawatajwi katika EPA,Kingunge Ngombale Mwiru lazima yumo tu maana anajulikana kwa umafia wake.

Ibambasi,

Kwangu mimi hilo wala nisingehitaji mshauri. Unitumie, uniruke, unichafue udhani nitaa kimya kukulinda, no way. Kifo ni safari ya kila mtu, kwanini niogope kifo ambacho kinaongozana na haki?

Nitaogopa kifo kinachoongozana na dhuluma maana hapo hakuna hata muda wa kujirekebisha.

Wewe uogope tena ukiwa nje ya nchi, eti unawaachia wengine mabomu ndio walipue kwa niaba yako kama hiyo sio cowardice ni nini?

Akina Dr. Mwakyembe wanawavaa akina Lowassa pale pale na bado wanapeta, yeye alikuwa anaogopa hata kivuli chake? Ameogopa na bado amekufa, sasa alikuwa analinda usalama upi?

Kwa kweli kila nikifikiria hili jambo linanichanganya mno, kama kuna ndugu walimwambia Ballali akae kimya naamini walifanya makosa makubwa sana.

Wote ni binadamu na wakati mwingine naionea huruma familia ya Ballali lakini pia inabidi hili jambo tuendelee kulijadili maana kilichofanywa na serikali na washirika wao wote ni kibaya mno. Tukiamua kukaa kimya yatatokea tena, hata kama hatuna nguvu za kisheria ni bora tuendelee kupiga kelele.
 
Kuna fununu kuwa Balali alifanya mahojiano na Tanzania Daima mwaka jana huko US.Tanzania Daima walikuwa tayari kuyaprint,wakaingiliwa na UWT...wakachimbwa mkwara mzito sana na matokeo yake it has gone mum till today.Lakini inasemekana ipo na kuna siku itaibuka tu.

Ilikuwaje Tanzania Daima wakaenda UWT kuomba ruhusa ya ku print mahojiano na Ballali?

Tunaomba maelezo ya uhusiano wa Ballali, UWT, Tanzania Daima na mpangilio mzima wa gazeti kukiambia chombo kingine nje ya chumba cha habari: tuko na news story hapa tunataka kuichapisha!
 
Ilikuwaje Tanzania Daima wakaenda UWT kuomba ruhusa ya ku print mahojiano na Ballali?

Tunaomba maelezo ya uhusiano wa Ballali, UWT, Tanzania Daima na mpangilio mzima wa gazeti kukiambia chombo kingine nje ya chumba cha habari: tuko na news story hapa tunataka kuichapisha!

Kama ni kweli si wangeleta copy JF where we dare to talk openly?
 
Mtanzania

I got you buddy naungana na hiyo hoja yako lakini pia ukumbuke kuna watu bado ni dhaifu tu,hii ni hulka ya binadamu wote with the exceptions of the very few (I bet you among them judging by the way you argue),sawa kifo ni kifo na kile cha haki ni chema zaidi,perhaps Balali had other motives...once documents zikiwa open scope ya mjadala itapanuka zaidi[/B]

Kwa kweli kila nikifikiria hili jambo linanichanganya mno, kama kuna ndugu walimwambia Ballali akae kimya naamini walifanya makosa makubwa sana.

Wote ni binadamu na wakati mwingine naionea huruma familia ya Ballali lakini pia inabidi hili jambo tuendelee kulijadili maana kilichofanywa na serikali na washirika wao wote ni kibaya mno. Tukiamua kukaa kimya yatatokea tena, hata kama hatuna nguvu za kisheria ni bora tuendelee kupiga kelele.
 
Yale yale; hivi tutaishi na fununu mpaka lini? Yaani tumebaki kuandika mafumbooooooo, mwisho tunanyamaza tunaendelea na fununu. We are doomed!
 
Back
Top Bottom