Wokovu wa zamani vs wasasa

Wokovu wa zamani vs wasasa

Mwl Mwakujonga

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2023
Posts
362
Reaction score
714
Kwanini Wokovu wa zamani ulikuwa wa Moto

Wakati nikiwa kwenye kongamano la maombi la kitaifa la 18 linaloongozwa na Mwalimu Christopher Mwakasege.

Wakati ibada zikiwa ziliendelea na wakati tukiwa safarini kutoka kwenye hosteli kwenda ukumbini, kuna kitu nilijifunza

Nikamuuliza mama mmoja mtu mzima miaka 60s nikataka jua enzi zao wakati wanaokoka nini kiwasaidia wokovu wao kuwa wa moto

Kitu ambacho aliniambia na nilichokiona kwamba zamani hakukuwa na nyimbo za sifa wala kuabudu kulikuwa na nyimbo za tensi na ili mtu aonekane ameokoka lazima tenzi za rohoni ziwe moyoni

Ilikuwa ni muhimu kuimba nyimbo za tenzi kwa sababu vitabu vilikuw vichache na hivyo ukipata kitabu unajitaidi kuimba kwa bidii ili nyimbo zikae ndani yako

Nilichokiona wakati wa nyimbo mara nyingi tulikuwa tunaangaika na simu kuweza kupata kitabu husika lakini wenzetu walikuwa wanaimba kutoka moyoni.

Nyimbo za tenzi asilimia 100 ni nyimbo za ushuhuda wa matendo ya Yesu, nyimbo zote zinamjenga muhumini kuwa karibu na Yesu

Katika nyimbo za tenzi sehemu kubwa zilikuwa ni kumjenga Mkristo kuwa karibu na Yesu na sio vinginevyo

Miaka yetu hii nyimbo nyingi za kikristo nyingi ni zile za kutaka vitu kwa Yesu na sio za kujenga uhusiano wako na Mungu

Nyimbo za kuimarisha uhusiano na Mungu ni lazima zikutengezee moyo wa kumpenda Yesu, kumlingana Mungu kwa sababu nyimbo zile zilikuwa ni shuhuda za watu ambao walitembea na Yesu ndio maana zilijenga waumini kiu ya Yesu ndio maana ziliitwa tenzi ya roho au nyimbo ya Kristo nk
 
Mambo mengi yameparanganyika, watu wa zamani ambao sasa ni watu wazima wanaonekana ni washamba wanapoendelea kushikilia misimamo motomoto ya zamani. Siku hizi ukihubiri injili kali mchungaji anaweza kukuambia usihubiri hivyo watu watahama kanisa, hubiri injili lainilaini
 
Mambo ya uzinzi siku hizi hayakemewi, mabinti wanapata mimba huku wanaimba kwaya, poa tu hawatengwi. Wengine wanafunga ndoa huku tayari ni wajawazito hawaulizwi kwa nini mmeanza kufanya tendo la ndoa kabla ya kufunga ndoa. Maagano ya ndoa hayafuatwi, wanandoa wanaachana haraka bila hofu ya Mungu
 
Back
Top Bottom