Wizi mpya vituo vya mafuta

Wizi mpya vituo vya mafuta

Mimi mara nyingi huwa nashuka kwenye gari halafu namkodolea macho,huwa wanaonyesha kununa lakini huwa sijali...
 
Wizi mwingine ni pale camel petrol station ya kwa Mwalimu Nyerere, huwa wanawatumia waendesha bajaji na bodaboda wanaopaki pale pembeni.
Ni kama vile wale pump attendant wamewakariri wazee wa kujaza full tank basi wakishaona gari yako inaingia wanapeana ishara na bodaboda au bajaji kiana , wakati unapaki vizuri bajaji inajazwa chap chap then kabla pump haijapoa inatumbukizwa kwako. Yaani lazima wakupige 5 liters .
Pale ukiona bajaji au bodaboda kwenye pump usingize gari hadi itoke na ikitoka kabla hawajaanza kukujazia mafuta hakikisha mita iko zero.
 
Hii nchi kila mtz mwizi,
Waache waibe tuu mshahara wenyewe pasua kichwa
 
Hizi sheli za Lake Oil na Camel oil zina wafanyakazi vibaka sana.
Jana nilikua najaza mafuta Camel oil mbezi kwa yusufu, jamaa nimemwambia aweke mafuta ya 20K yeye kaniwekea ya elfu tatu.
Kisha akaniambia tayari.
Kuangalia pump nakuta kaweka ya elfu tatu nauliza vipi mbona elfu tatu... Oh pampu inazima zima.
Kiukweli kanikuta hii wiki nina stamala wajada lakini alinikera sana.
Akaongeza mafuta yaliyo kua yamepungua nikaondoka zangu.

Tue makini Kwakweli.
 
Huwezi kuibiwa kizembe namna huyo utakuwa bogus namba moja kwenye Nchi ya Shit hole, au labda uwe umepewa gari na Shemeji yako na haujui uchungu wowote kuanzia mafuta mpaka gari lenyewe
Hongera Kwa Kua na La Kwako Mwenyewe
 
Haya wale wamiliki magari,mtindo mpya umeibuka!Wakati wewe ukiamini mafuta yanawekwa kwa tanki la Gari,kumbe muweka mafuta anakuziba ili usione dumu dogo ili aweze kuwa anakuibia jionee kwa picha

View attachment 741655
Hapa ni kama kituo cha mafuta cha Lake Oil pale Kongowe njia ya kwenda Mkuranga. Mimi pia hapo nimewahi kuchezewa huo mchezo nilipomshtukia yule mhudumu nilimripoti kwa boss wake hapo hapo. Sijui kwa nini wanatabia hiyo baadhi ya wahudumu hawa
 
Wale wana mbinu nyingi sana huwezi kuwadhibiti labda utembee na kidumu chako.
 
Back
Top Bottom