RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI MWAKA ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI, 2010 inasema
5.9 Kukosekana kwa orodha ya waliolipwa kiasi cha Sh.48,000,270,000 kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa uchumi
Serikali ililipa kiasi cha Sh. 48,000,270,000 katika Benki Kuu ya Tanzania kama sehemu ya mchango wake wa kuchochea ukuaji wa uchumi ili kukabiliana na msukosuko wa uchumi ulioikumba dunia. Hata hivyo, hatukupatiwa orodha ya walionufaika na fedha hizo za kufidia hasara na kulipia mikopo wala utaratibu utakaotumika kwa wafanyabiashara husika kurejesha fedha hizo pindi hali ya uchumi itakapoimarika. Kwa hali hiyo, nimeshindwa kujiridhisha kuhusu uhalali wa malipo hayo na urejeshwaji wake
utakavyokuwa. CAG L.S Utouh
Hii si EPA ya pili?
5.9 Kukosekana kwa orodha ya waliolipwa kiasi cha Sh.48,000,270,000 kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa uchumi
Serikali ililipa kiasi cha Sh. 48,000,270,000 katika Benki Kuu ya Tanzania kama sehemu ya mchango wake wa kuchochea ukuaji wa uchumi ili kukabiliana na msukosuko wa uchumi ulioikumba dunia. Hata hivyo, hatukupatiwa orodha ya walionufaika na fedha hizo za kufidia hasara na kulipia mikopo wala utaratibu utakaotumika kwa wafanyabiashara husika kurejesha fedha hizo pindi hali ya uchumi itakapoimarika. Kwa hali hiyo, nimeshindwa kujiridhisha kuhusu uhalali wa malipo hayo na urejeshwaji wake
utakavyokuwa. CAG L.S Utouh
Hii si EPA ya pili?