Wizi mpya BOT

Lusambara

Member
Oct 31, 2010
38
9
RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI MWAKA ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI, 2010 inasema

5.9 Kukosekana kwa orodha ya waliolipwa kiasi cha Sh.48,000,270,000 kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa uchumi
Serikali ililipa kiasi cha Sh. 48,000,270,000 katika Benki Kuu ya Tanzania kama sehemu ya mchango wake wa kuchochea ukuaji wa uchumi ili kukabiliana na msukosuko wa uchumi ulioikumba dunia. Hata hivyo, hatukupatiwa orodha ya walionufaika na fedha hizo za kufidia hasara na kulipia mikopo wala utaratibu utakaotumika kwa wafanyabiashara husika kurejesha fedha hizo pindi hali ya uchumi itakapoimarika. Kwa hali hiyo, nimeshindwa kujiridhisha kuhusu uhalali wa malipo hayo na urejeshwaji wake
utakavyokuwa. CAG – L.S Utouh


Hii si EPA ya pili?
 
watu walifungua makampuni asubuhi na jioni wakachukua pesa hizi toka benki............
 
Hizi ni habari za zamani sana mkuu na tumekwisha zizungumzia na kupata ufumbuzi wake kutoka sehemu husika, leta hoja mpya na zenye mashiko achana na zilipendwa, nchi hii inahitaji mchango wako.
 
Hizi ni habari za zamani sana mkuu na tumekwisha zizungumzia na kupata ufumbuzi wake kutoka sehemu husika, leta hoja mpya na zenye mashiko achana na zilipendwa, nchi hii inahitaji mchango wako.

Mkuu hii ripoti imetoka juzi tu na wewe unasema hizi ni habari za zamani.. tukueleweje?
 
Hizi ni habari za zamani sana mkuu na tumekwisha zizungumzia na kupata ufumbuzi wake kutoka sehemu husika, leta hoja mpya na zenye mashiko achana na zilipendwa, nchi hii inahitaji mchango wako.

We vipi, ufumbuzi upi tuliupata, ufumbuzi wa pesa kutumika visivyo ni kurejeshwa kwa pesa husika sasa hilo limefanyika lini? Halafu kurudia kulizungumza ni sawa kabisa si unajua hatuna madawati, vyumba vya madarasa, nyumba za walimu nk. fedha hizi zingetumika kwa mambo mengi tu kama serikali ingekuwa makini, unachojaribu kufanya wewe ni kuzima moto wa petrol kwa mafuta ya taa.
 
Anayetetea au kulazimisha tusiseme dhambi, ni MWIZI. Gamba Jipya sawa na CCM without old gamba, ni sawa na genge la mafisadi.

Gamba jipya kama jina lako, tupe matokeo ya hizo habari za zamani, tunazitaka sasa kwa ajiri ya kupambana na mafisadi wa sasa.



Hizi ni habari za zamani sana mkuu na tumekwisha zizungumzia na kupata ufumbuzi wake kutoka sehemu husika, leta hoja mpya na zenye mashiko achana na zilipendwa, nchi hii inahitaji mchango wako.
 
Huyu anayetaka utata uliozunguka malipo haya ya mabilioni ya fedha za wananchi uwekwe chini ya zuria ana lake, lakini kwa wengi wetu tunataka vyombo husika vifuatilie tuhuma hii na wananchi wapewa taarifa juu ya jambo hilo mapema iwezekanavyo.
 
Mkuu hii ripoti imetoka juzi tu na wewe unasema hizi ni habari za zamani.. tukueleweje?

Gamba Jipya nalo linatakiwa kuvuliwa tu, amejadili lini na ni mgeni humu au alibadilisha I'd ndio kajivua gamba?
 
Hizi ni habari za zamani sana mkuu na tumekwisha zizungumzia na kupata ufumbuzi wake kutoka sehemu husika, leta hoja mpya na zenye mashiko achana na zilipendwa, nchi hii inahitaji mchango wako.

Unauhusiano na Chama cha Gamba nini? Umetumwa kuja kuvuruga? Umejiunga juzi tu (16th April, 2011), umezisoma lini hizi taarifa? Gamba lako jipya halibadili mawazo na sumu yako. Tumekushitukia.
 
RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI MWAKA ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI, 2010 inasema

5.9 Kukosekana kwa orodha ya waliolipwa kiasi cha Sh.48,000,270,000 kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa uchumi
Serikali ililipa kiasi cha Sh. 48,000,270,000 katika Benki Kuu ya Tanzania kama sehemu ya mchango wake wa kuchochea ukuaji wa uchumi ili kukabiliana na msukosuko wa uchumi ulioikumba dunia. Hata hivyo, hatukupatiwa orodha ya walionufaika na fedha hizo za kufidia hasara na kulipia mikopo wala utaratibu utakaotumika kwa wafanyabiashara husika kurejesha fedha hizo pindi hali ya uchumi itakapoimarika. Kwa hali hiyo, nimeshindwa kujiridhisha kuhusu uhalali wa malipo hayo na urejeshwaji wake
utakavyokuwa. CAG – L.S Utouh


Hii si EPA ya pili?
Nina wasiwasi na JK na familia yake walichukua fedha hizo na kufanyia kampeni. Kama sivyo, basi JK achukue hatua kali dhidi ya waliotumia viabaya pesa hizo.
 
Mkuu hii ripoti imetoka juzi tu na wewe unasema hizi ni habari za zamani.. tukueleweje?

Mkuu hii report tumeshaizungumzia sana hata kabla ya kutoka ofisini kwa CAG na baadae Zuberi aliipeleka bungeni tukaizungumzia tena, na waziri mkubwa akatoa majibu mazuri tuu na wabunge wakamwelewa, naombeni tuongelee mambo mapya yenye kuleta maendeleo wakuu.

Mleta mada inaonekana siyo mfuatiliaji wa wanayojiri Tanzania.
 
Hizi ni habari za zamani sana mkuu na tumekwisha zizungumzia na kupata ufumbuzi wake kutoka sehemu husika, leta hoja mpya na zenye mashiko achana na zilipendwa, nchi hii inahitaji mchango wako.
Mmezizungumza na nani? Ufumbuzi wake ni upi? tunataka utuambia mmechukua hatua gani kwa hao mafisadi wenu waliozitafuna pesa hizo maana najua zimeliwa na watu wanaojichubua magamba.
 
Mkuu hii report tumeshaizungumzia sana hata kabla ya kutoka ofisini kwa CAG na baadae Zuberi aliipeleka bungeni tukaizungumzia tena, na waziri mkubwa akatoa majibu mazuri tuu na wabunge wakamwelewa, naombeni tuongelee mambo mapya yenye kuleta maendeleo wakuu.

Mleta mada inaonekana siyo mfuatiliaji wa wanayojiri Tanzania.
Tatizo siyo mtoa mada, tatizo lipo kwako wewe unayechanganya madesa. Ripoti iliyopelekwa Rais mwishoni mwa mwezi Machi 2011 na kisha kupelekwa bungeni wiki mbili tu zilizopita wewe unasema mlishaizungumzia zamani. Wapi mlizungumza, UV-CCM, NEC au kwenye CC magamba? Majibu ya kueleweka ni yapi sasa maana wengine hatujapata taarifa hizo?
 
Hizi ni habari za zamani sana mkuu na tumekwisha zizungumzia na kupata ufumbuzi wake kutoka sehemu husika, leta hoja mpya na zenye mashiko achana na zilipendwa, nchi hii inahitaji mchango wako.
We mwanaGAMBA wewe!
Nani aliyesema hizi ni habari za zamani?
Ebu retrieve thread iliyoongelea suala hili siku za nyuma!
Nyie WAPURUZI tushawastukia, acha watu waweke hadharani sehemu ya magamba ambayo hamjayavua bado!
SUBIRI ZIWEKWE NA PAYMENT VOCHA HAPA ndiyo utajua kuwa TUNAMAANISHA TUNACHOSEMA!
 
Mkuu hii report tumeshaizungumzia sana hata kabla ya kutoka ofisini kwa CAG na baadae Zuberi aliipeleka bungeni tukaizungumzia tena, na waziri mkubwa akatoa majibu mazuri tuu na wabunge wakamwelewa, naombeni tuongelee mambo mapya yenye kuleta maendeleo wakuu.

Mleta mada inaonekana siyo mfuatiliaji wa wanayojiri Tanzania.

mkuu hapa JF hauna hata siku 3, uliizungumzia jukwaa gani?
maendeleo gani yatapatikana ikiwa fedha zinapotea bila maelezo ya kuridhisha..
 
mkuu hapa JF hauna hata siku 3, uliizungumzia jukwaa gani?
maendeleo gani yatapatikana ikiwa fedha zinapotea bila maelezo ya kuridhisha..
.... Pesa iliingizwa kwenye benki moja kubwa ina nembo yake ya rangi ya ccm baadaye ikachomolewa. Magumashi ya kampeni. Tufunge mjadala please. said mwema amchunguze shemeji????
 
watu walifungua makampuni asubuhi na jioni wakachukua pesa hizi toka benki............

Haya ni maajabu sana Ed, inauma sana pale mjasiriamali anapokwenda benki kuomba hata 'overdraft' akamatimize order yake na kunyimwa.
 
[I said:
Gamba Jipya;1871107]Hizi ni habari za zamani sana mkuu na tumekwisha zizungumzia na kupata ufumbuzi wake kutoka sehemu husika, leta hoja mpya na zenye mashiko achana na zilipendwa, nchi hii inahitaji mchango wako.[/I]

Umejiunga hapa Jamii Forums tarehe 17/04/2011 na unasema hiyo habari imeshaongelewa na mliipatia uvumbuzi....wewe na nani, na wapi maana hukuwa hapa jamvini? Kazi kubwa tunayo hapa Tanzania ya kuwa na watu kama nyie mnao chakachuwa habari na kupotosha jamii. Au na wewe ulikuwa mmoja wao nini mliyotafuna pesa ya walipa kodi?

 
Back
Top Bottom