Wizara: Ni sahihi kuchoma vifaranga na utaratibu unatambulika kimataifa, yarusha lawama kwa waliosambaza picha

Natamani siku moja Wahamiaji Haramu, Magari yalioyoingizwa Kwa makosa nchini yachomwe moto maana ndio Mwisho wa busara zetu
 
Katibu mkuu wangu sio kweli kuwa kueneza hizo picha ni kosa,sema sheria gani itakuwa imevunjwa ?ni haki yetu kujua kuwa hao vifaranga walikuwa na maradhi,vile vile hata kama walikuwa na maradhi njia uliyotumia sio,acha siasa kwa wanasiasa wewe ni mtaaalamu katika wizara hiyo,na please mshitue katibu mkuu mwenzako wa wizara ya afya kuwa jirani zetu Madagascar kuna ugonjwa wa PLAGUE,kwa hiyo tuanze kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kuuelimisha umma dalili zake ,utabibu wake(huu unatibiwa kirahisi)na njia za kujikinga tusije chelewa kama utapiga hodi mlangoni kwetu;again issue kama hizi please usizijibu kisiasa.
 
Hivi kuchoma moto vifaranga, na kupiga picha, lipi ni kosa? Ama kweli mwaka huu mpaka wanyama na ndege wataona cha mtema kuni.
 
Wizara iko sahihi ,Kuhusu bidhaa zisizo na ubora kama zimethibitika na mamlaka husika zinapigwa chini, mbona tunachoma vifaa fake vingi kutoka nje? ni mara ngapi vitu vimepatikana airport au bandari tena macontainer yanakamatwa na yanachomwa moto? je huwa tuna ugomvi na hizo nchi ambazo watanzania wamenunua bidhaa hizo? tatizo tumekubali kujenga undugu usio na tija na nchi jirani hivyo kupelekea kushindwa kusema hapana hata kwa mambo yasio na msingi, tukipata chickenpox ndo tutajua ni kwa nini serikali inakataza hao vifaranga.

Kikubwa ambacho kitaleta stability kati yetu na nchi zote za jirani, ni serikali ya Tanzania kuanza kutenga maeneo maalum kwa ajiri ya kuchungia mifugo hasa kwa wananchi wanaoishi maeno ya mipakani au karibu na mipakani.
Itathibitkaje ikiwa umeambiwa hawakupimwa
 
Mantiki yao nzima ktk utetezi wao sababu kuu wanasema ni Ugonjwa wa Mafua ya Ndege ,je ni kweli vile Vifaranga vilikuwa na Homa ya Mafua ya Ndege ?.
 
Wizara ya mifugo na uvuvi imetetea uamuzi wa kuchoma vifaranga kwani ni utaratibu unaotambulika kimataifa na kwa mujibu wa sheria namba 17 ya sheria ya wanyama ya mwaka 2003 imechukua uamuzi huo wa kuteketeza vifaranga hivyo 6400 ili kuepusha kusambaza mafua ya ndege.

Msimamo huo umetolewa na katibu mkuu wa wizara, amesema hatua hio imefikiwa kuzuia kuenea ugonjwa wa aina yoyote wa kuku kuingia kwenye kuku wa nchini na kuzuia uingizaji holela wa vifaranga bila kupitia utaratibu na sheria zilizopo.

Amesema hasara ambayo ingeletwa na vifaranga 6400 kama wangeingia kwa namna waliyoingia na kuleta madhara yangekuwa makubwa zaidi kuliko yanayoonekana kwa kuteketeza vifaranga 6400.

Alipoulizwa kama hakukuwa na namna nyingine ya kuviaribu zaidi ya kuviteketeza hadharani, amesema havikuchomwa hadharani na amesema waliosambaza hizo picha walikuwa na lengo tofauti, amesema vitu vinavyofanyika nje ya hadhara maana yake havitakiwi kuonekana kwenye hadhara na mtu akikiuka ndio analeta madhara kama yaliyotokea.

Amesema utaratibu wa kuwachoma umetumika pia na mataifa mengine akitolea mfano Ulaya kilipotokea kichaa cha Ng'ombe lakini amesema sio kitendo cha kumuonyesha kila mtu ndivyo walivyofanyiwa.

Kuhusu kuwapima, amesema hawawezi kupima vifaranga ambavyo tangu awali walishatoa katazo visiingie nchini.


Bullshit.
Moto?? Vifaranga?? Dah, huu ni ukatili.vingerudishwa huko huko.
 
Sasa nimetambua kuwa watanzania baadhi yao hawajui sheria na taratibu zinazoendesha biashara. Wizara wapo sahihi kuchoma, tatizo ni nini. Kuna bidhaa ngapi fake zinateketekezwa tena za fedha nyingi, ifikie mahali tufikiri kwanza kabla ya kulaumu tu. Vifaranga hivyo ni vichache sana ukilinganisha na hasara ambayo tungeipata, halafu vimepitia njia za panya!
 
Back
Top Bottom