PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,724
Wakubwa,
Nilishasikia toka zamani kidogo kuwa kawaida Baba ndani ya nyumba anapata wivu kidogo inapofikia wakati wa kumuoza bintiye, hali kadhalika Mama anakuwa na aina fulani ya kijicho pale Kijana wake wa kiume anapotangaza kuanzisha uchumba na binti wa mtu kwa nia kumuoa!...
Huenda wengine tumeshaona Live pale binti anapoleta habari nyumbani kuwa amepata Mchumba, Mama anaweza kuipokea taarifa hiyo kwa vigelegele, lakini Baba itamchukua muda kidogo, na wakati mwingine ataanzisha sababu sababu, na hata kufikia baadaye kumkataa kijana muoaji!
Binafsi sasa hivi nina'handle 'ushenga' ambao una mvutano mkali sana kati ya Baba na Bintiye, ambapo baba anaonyesha wazi kutokumkubali kijana muoaji bila sababu za msingi, na anasema kuwa "huyo mwanaume atakuja kukuacha baadaye"...My hairs!
Wanajamvi, naomba maoni yenu endapo jambo hili la wivu lina ukweli ama ni hisia tu!
Nilishasikia toka zamani kidogo kuwa kawaida Baba ndani ya nyumba anapata wivu kidogo inapofikia wakati wa kumuoza bintiye, hali kadhalika Mama anakuwa na aina fulani ya kijicho pale Kijana wake wa kiume anapotangaza kuanzisha uchumba na binti wa mtu kwa nia kumuoa!...
Huenda wengine tumeshaona Live pale binti anapoleta habari nyumbani kuwa amepata Mchumba, Mama anaweza kuipokea taarifa hiyo kwa vigelegele, lakini Baba itamchukua muda kidogo, na wakati mwingine ataanzisha sababu sababu, na hata kufikia baadaye kumkataa kijana muoaji!
Binafsi sasa hivi nina'handle 'ushenga' ambao una mvutano mkali sana kati ya Baba na Bintiye, ambapo baba anaonyesha wazi kutokumkubali kijana muoaji bila sababu za msingi, na anasema kuwa "huyo mwanaume atakuja kukuacha baadaye"...My hairs!
Wanajamvi, naomba maoni yenu endapo jambo hili la wivu lina ukweli ama ni hisia tu!