Habari wana MMU,
Wakuu hebu naombeni mawazo namna ya kupunguza kuwa na wivu, seriously nimechoka na nahisi hili ni tatizo kubwa si kwangu tu bali hata kwa mpenz wangu. Hajawah kuniambia moja kwa moja but I can feel it namnyima furaha sana.
Natamani ajiskie namuamini sana, tatizo linakuja kila ninapojaribu hata kumuacha tu atoke na wafanyakazi wenzake kwa jinsi nitakavyoteseka kwa hayo masaa machache anaweza kunikuta nishakufa kabisa hivyo huwa naona bora nisogee tu hilo eneo hata nimuone kwa mbali. Kuna siku nlikuwa nae kwenye gari ghafla ule wimbo wa 'Kuchapiwa ni siri ya ndani' ukapigwa redioni yani kile kitendo cha yeye kuufatiza tu ule wimbo nikajikuta nimegonga gari iliyokuwa mbele yangu kwa mshtuko.
Analijua tatizo langu na anajitahidi sana kuishi ninavyotaka na najua ananivumila sana, amepunguza sana marafiki kwa ajili yangu, hata kwenye groups hz za wasap kajitoa, fb ndio hata ile app tu kwenye sim yake haipo tena na hata akitaka kuingia anaingia kwa sim yangu.
Kilichonifanya nije kwenu ni baada jana usiku kumgombeza kwa kupigiwa simu na mwanaume akimtakia usiku mwema ilikuwa sa tatu tu usiku, hata sijui ilikuwaje lkn nikajikuta nishaanza kulalama, alisema sorry na kisha akampigia sim huyo jamaa na kumwambia asirudie tena kumpigia simu usiku.
Nimejiskia vibaya sana baada ya yeye kufanya hivyo, japokuwa bado naonyesha ukauzu bt deep inside nimenyong'onyea mbaya kabisa. Najiona mwanaume nisie na shukrani kabisa.
I really want to change nipunguze tu kidogo nibakie na kale ka wivu ka kumuonyesha najali, tatizo sijui cha kufanya pia sijui ntawezaje.
Please wana MMU nisaidien mawazo mrudishe furaha ya mrembo wa watu na amani ya moyo wangu. Nimeeleza kwa kirefu ili at least muone ukubwa wa tatizo, michango ya aina zote inakaribishwa.