Imekuwa kawaida sasa kwa vijana wengi kushabikia mno CHADEMA.Hii inapelekea hata kusahau pale chama hiki kinapo boronga,wao hufumba macho na kutanguliza ushabiki mbele.
Jambo hili ni baya kwa mustakabali wa taifa letu,kwani pale ambapo CHADEMA itafanikiwa kuchukua dola,itakumbana na wakati mgumu kwani imezoea kujiona sahihi wakati wote.
Mbaya zaidi wengi wa mashabiki ni wale wasio hata na kadi ya chama,nao wanajiita wana CHADEMA.
Jambo la msingi kukumbushana ni kuwa sisi ni watanzania.Nawasihi mashabiki wa CHADEMA ni bora wakajiondoa CHADEMA na kujiona kama watanzania neutral ambao watashabikia maslahi ya taifa,na chama kinacho yatekeleza ndicho kiungwe mkono.
Hii itawawezesha kuikosoa chadema pale inapo kosea,na hivyo CHADEMA itakuwa imara na kupata nguvu zaidi.
TANZANIA:Nakupenda sana.
isshi! Na familia yako je?kwakuwa tulianza na mungu tutamaliza na mungu......i mean tutafia chadema
sio tutafia, utafia peke yakokwakuwa tulianza na mungu tutamaliza na mungu......i mean tutafia chadema
Mtu wa Nape,
Kwani wewe uliingia na nani huko CHADEMA?
Je, ni nani aliyekuambia kuwa CHADEMA inajiona iko sahihi?
Mbona unaongelea ...mjitoe, wakati maelezo yako yanadai...wao CHADEMA....!!!
Kama CHADEMA inao mashabiki wengi wasio wanachama je, mbona wanashinda Chaguzi mbalimbali?
TAKE NOTE:
CHADEMA, ina nguvu Kubwa mno tena inatosha waambie walokutuma wawe wepesi wa Kusoma Alama za Nyakati.
Kumbuka wakishakutumia hao akina Nape utatupwa kama....Ko@n*O%U !!!
Una akili sana wewe. Huu ushabiki is too much, sasa naona umeshika kasi. hakuna aliye mtakatifu hapa duniani sasa iweje hawa wanaojiita wanachadema wasione mapungufu ya chadema? au ndio kusema hayapo? acheni ushabiki bwana wekeni maslahi ya taifa mbele.
nakumbuka kuelekea uchaguzi mzee mwanakijiji alitoa uzi ulio kuwa unakemea watu kuwa neutral sasa leo wewe unatuambia tuwe neutral kwa hoja za kimasaburi saburi, nenda kawaambie vijana hatuna muda wa kurudi nyuma na hatutafuti chama cha malaika, tumaini letu kwasasa ni chadema siku wakituzingua tunapiga chini tunatafuta chama kitakcho kuwn mlengo mazuri wa watanzania lakini kwasasa ni chadema
Bora ungekaa kimya kuliko kutuletea utumbo wa mjusi kama huu.
Tena Ule wa chooni!!pure vapour!