Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 37,375
- 86,866
Hamjambo!
1. Bado tunawekana Sawa. Tunazungumza. Ili mambo yakae sawa.
2. Kuna vitabia vya ajabuajabu ndani ya nchi yetu. Tabia ya kujimilikisha mambo ambayo hayamilikiwi na yeyote. Mambo ya wote kundi na genge Fulani linahodhi na kujimilikisha. Hiya ni dhulma.
3. Ukweli, uzuri, uponyaji, haki havinaga mmiliki kwa ni halali ya Kila MTU na Kila kiumbe.
4. Mtibeli atatumia kisa cha Yesu na Wanafunzi wake, ambao nao walikuwa na tabia mbaya kama hii. Kujimilikisha mambo ya wote.
5. Wanafunzi wa Yesu walipokuwa kwenye pitapita zao huko mitaani wakiwa wenyewe. Mara wanashuhudia Kundi jingine huko mitaani likiponya na kutoa mapepo watu huku likitaja jina la Yesu.
6.wanafunzi wakapatwa na kihoro, hasira. Wakakimbia mbio wakirudi kushtaki kwa Yesu. Walipofika wakamwambia, Bwana! Bwana tumepita huko Mitaa ya Buza, Nyehunge, na Kaloleni tumeona watu wakitoa Pepo na kuponya watu kwa jina lako. (Wakimaanisha alafu sio wanafunzi wako).
7. Yesu akajibu akawaambia, Wapo kondoo walionje ambao hawapo hapa lakini ni kondoo wa zizi hili.
8. Kisa hiko ni kisa cha umiliki na maslahi.
9. CCM wanaamini kuwa Wao ndio pekee wanahaki ya kumiliki nchi hii huku vyama vingine wakionekana kama wapangaji.
Jambo hili linanyima haki vyama vingine.
10. CCM lazima waelewe vyama vingine navyo vinahaki sawa na wamiliki wa nchi hii.
11. CHADEMA nao wamejikuta katika hali hiyohiyo ya wao kujifanya wamiliki wa ukweli, haki na demokrasia.
12. Chadema wanaamini kwamba huwezi kuwa mpenda Ukweli, demokrasia na mpenda Haki ukiwa nje ya CHADEMA.
Jambo ambalo kama Mtibeli na watibeli wote waliopo siasani na wasio siasani tunalikataa.
13. Wanafunzi wa Yesu waliamini ili uponye na kutoa mapepo lazima uwe mwanafunzi wa Yesu lakini pili waliamini kwamba wao wanammiliki Yesu.
Lakini walipokutana na watu wengine huko duniani ambao hawajawahi hata kuwaona wakiponya, na wakitoa Pepo Kwa jina la Yesu ikawapa kihoro na hasira.
14. Ubaya hauna Kwao. Kama ulivyo wema. Wapo Wabaya Chadema, na wapo Wabaya CCM. Wapo wema Chadema na wapo Wema CCM.
15. Chadema ni chama cha siasa. CCM ni chama cha siasa. Watanzania wanahaki ya kuwa chama chochote Kati ya hivyo au nje ya hivyo. Au wasiwe na Chama Kabisa.
16. CHADEMA pia wanatatizo la wao kutaka kusema Ukweli kwa wengine lakini wao hawataki kuambiwa Ukweli. Jambo ambalo tunarudi kulekule kwamba Ukweli kwao ni ule wanaousema wao sio unaosemwa na watu walionje. Hii kimantiki na masuala ya haki haipo Sawa.
17. Tabia ya kutaka maoni ya watu yafanane na mtazamo wa CHADEMA ni tatizo jingine linalowakabili Chadema.
Katika hilo wanakuwa hawana tofauti na CCM ambao nao unageuka adui yao pale unapowaambia ukweli wanakuhisi wewe ni CHADEMA au adui yao.
18. Demokrasia ni pamoja na kuheshimu maoni ya watu wengine bila kuwashambulia na kuwavunjia haki zao. Kuwatukana, kuwazushia n.k.
19. Unapopigania Demokrasia alafu muda huohuo hutaki mawazo ya wengine au unatukana wenye mawazo kinzani na yako unakuwa hujui maana ya Uhuru wa maoni na demokrasia.
20. Sisi Watibeli Tunajua Ukweli haumilikiwi na mtu, watu au taifa Fulani. Ukweli ni wawatu wote na unaweza kuupata popote.
21. Ukweli kwetu lazima uchunguzwe ili uthibitike.
Ndio maana Watibeli Wote. Unaweza kumkuta Mtibeli ni Muislam lakini hiyo haimaanishi haoni Ukweli na uongo uliopo kwenye Ukristo. Pia ataona kasoro na uongo katika Uislam na haoni shida kusema kasoro na uongo uliopo katika uislam hata kama ni dini yake.
22. Vivyohivyo, Mtibeli Mkristo lazima aone ukweli na uongo uliopo kwenye dini zingine ikiwemo uislam na kasoro zake.
Na pia katika Dini yake.
23. Halikadhalika na mambo ya vyama vya siasa. Watibeli sio mashabiki. Sio watu wakujiendea endea au kupelekwa pelekwa.
24. Sisemi watu wawe kama Watibeli, ila nazungumzia umuhimu watu kuyaangalia mambo vile yalivyo, bila ushabiki. Kutojimilikisha mambo ya watu wore.
25. Mfano kwenye jamii yetu;
Heshima ni haki na mali ya Kila mtu. Lakini utashangaa kundi au tabaka Fulani likijimilikisha heshima, kwamba wao ndio wanastahili kuheshimiwa.
Mfano Wazazi baadhi hutaka kuheshimiwa wao tuu lakini kuheshimu watoto wao wanaona mzigo. Hii sio sawa.
Pia viongozi wa Jamii na taifa baadhi yao hutaka wapewe heshima tuu. Alafu wao kutoa heshima hawataki au wanaona kama ni kujishusha.
26. Sisi Watibeli, Heshima inaanzia juu kwenda chini. Sio chini kwenda juu.
Wajuu akionyesha heshima ataheshimiwa. Sio atake heshima. Nope! Aonyeshe heshima. Mkubwa na wajuu ndio role model.
Kufikia hapo sina la ziada.
Sabato Njema Sana.
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
1. Bado tunawekana Sawa. Tunazungumza. Ili mambo yakae sawa.
2. Kuna vitabia vya ajabuajabu ndani ya nchi yetu. Tabia ya kujimilikisha mambo ambayo hayamilikiwi na yeyote. Mambo ya wote kundi na genge Fulani linahodhi na kujimilikisha. Hiya ni dhulma.
3. Ukweli, uzuri, uponyaji, haki havinaga mmiliki kwa ni halali ya Kila MTU na Kila kiumbe.
4. Mtibeli atatumia kisa cha Yesu na Wanafunzi wake, ambao nao walikuwa na tabia mbaya kama hii. Kujimilikisha mambo ya wote.
5. Wanafunzi wa Yesu walipokuwa kwenye pitapita zao huko mitaani wakiwa wenyewe. Mara wanashuhudia Kundi jingine huko mitaani likiponya na kutoa mapepo watu huku likitaja jina la Yesu.
6.wanafunzi wakapatwa na kihoro, hasira. Wakakimbia mbio wakirudi kushtaki kwa Yesu. Walipofika wakamwambia, Bwana! Bwana tumepita huko Mitaa ya Buza, Nyehunge, na Kaloleni tumeona watu wakitoa Pepo na kuponya watu kwa jina lako. (Wakimaanisha alafu sio wanafunzi wako).
7. Yesu akajibu akawaambia, Wapo kondoo walionje ambao hawapo hapa lakini ni kondoo wa zizi hili.
8. Kisa hiko ni kisa cha umiliki na maslahi.
9. CCM wanaamini kuwa Wao ndio pekee wanahaki ya kumiliki nchi hii huku vyama vingine wakionekana kama wapangaji.
Jambo hili linanyima haki vyama vingine.
10. CCM lazima waelewe vyama vingine navyo vinahaki sawa na wamiliki wa nchi hii.
11. CHADEMA nao wamejikuta katika hali hiyohiyo ya wao kujifanya wamiliki wa ukweli, haki na demokrasia.
12. Chadema wanaamini kwamba huwezi kuwa mpenda Ukweli, demokrasia na mpenda Haki ukiwa nje ya CHADEMA.
Jambo ambalo kama Mtibeli na watibeli wote waliopo siasani na wasio siasani tunalikataa.
13. Wanafunzi wa Yesu waliamini ili uponye na kutoa mapepo lazima uwe mwanafunzi wa Yesu lakini pili waliamini kwamba wao wanammiliki Yesu.
Lakini walipokutana na watu wengine huko duniani ambao hawajawahi hata kuwaona wakiponya, na wakitoa Pepo Kwa jina la Yesu ikawapa kihoro na hasira.
14. Ubaya hauna Kwao. Kama ulivyo wema. Wapo Wabaya Chadema, na wapo Wabaya CCM. Wapo wema Chadema na wapo Wema CCM.
15. Chadema ni chama cha siasa. CCM ni chama cha siasa. Watanzania wanahaki ya kuwa chama chochote Kati ya hivyo au nje ya hivyo. Au wasiwe na Chama Kabisa.
16. CHADEMA pia wanatatizo la wao kutaka kusema Ukweli kwa wengine lakini wao hawataki kuambiwa Ukweli. Jambo ambalo tunarudi kulekule kwamba Ukweli kwao ni ule wanaousema wao sio unaosemwa na watu walionje. Hii kimantiki na masuala ya haki haipo Sawa.
17. Tabia ya kutaka maoni ya watu yafanane na mtazamo wa CHADEMA ni tatizo jingine linalowakabili Chadema.
Katika hilo wanakuwa hawana tofauti na CCM ambao nao unageuka adui yao pale unapowaambia ukweli wanakuhisi wewe ni CHADEMA au adui yao.
18. Demokrasia ni pamoja na kuheshimu maoni ya watu wengine bila kuwashambulia na kuwavunjia haki zao. Kuwatukana, kuwazushia n.k.
19. Unapopigania Demokrasia alafu muda huohuo hutaki mawazo ya wengine au unatukana wenye mawazo kinzani na yako unakuwa hujui maana ya Uhuru wa maoni na demokrasia.
20. Sisi Watibeli Tunajua Ukweli haumilikiwi na mtu, watu au taifa Fulani. Ukweli ni wawatu wote na unaweza kuupata popote.
21. Ukweli kwetu lazima uchunguzwe ili uthibitike.
Ndio maana Watibeli Wote. Unaweza kumkuta Mtibeli ni Muislam lakini hiyo haimaanishi haoni Ukweli na uongo uliopo kwenye Ukristo. Pia ataona kasoro na uongo katika Uislam na haoni shida kusema kasoro na uongo uliopo katika uislam hata kama ni dini yake.
22. Vivyohivyo, Mtibeli Mkristo lazima aone ukweli na uongo uliopo kwenye dini zingine ikiwemo uislam na kasoro zake.
Na pia katika Dini yake.
23. Halikadhalika na mambo ya vyama vya siasa. Watibeli sio mashabiki. Sio watu wakujiendea endea au kupelekwa pelekwa.
24. Sisemi watu wawe kama Watibeli, ila nazungumzia umuhimu watu kuyaangalia mambo vile yalivyo, bila ushabiki. Kutojimilikisha mambo ya watu wore.
25. Mfano kwenye jamii yetu;
Heshima ni haki na mali ya Kila mtu. Lakini utashangaa kundi au tabaka Fulani likijimilikisha heshima, kwamba wao ndio wanastahili kuheshimiwa.
Mfano Wazazi baadhi hutaka kuheshimiwa wao tuu lakini kuheshimu watoto wao wanaona mzigo. Hii sio sawa.
Pia viongozi wa Jamii na taifa baadhi yao hutaka wapewe heshima tuu. Alafu wao kutoa heshima hawataki au wanaona kama ni kujishusha.
26. Sisi Watibeli, Heshima inaanzia juu kwenda chini. Sio chini kwenda juu.
Wajuu akionyesha heshima ataheshimiwa. Sio atake heshima. Nope! Aonyeshe heshima. Mkubwa na wajuu ndio role model.
Kufikia hapo sina la ziada.
Sabato Njema Sana.
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam