Chama Kipya,
Kwanza niliisha kuahidi katika jamvi hili kuwa uchochezi na uwongo wowote hautaachwa bila kujibiwa. Pamoja na kuwa fedha za Chama ni haki kwa wanachama kupata taarifa sahihi, haki hiyo hiyo inamtaka yeyote anayepotosha ajibiwe palepale ili wanachama, wapenzi na wananchi kwa ujumla wasipotoshwe na propaganda zisizo na maana. Dr Slaa ndiye accounting Officer, yaani msimamizi Mkuu wa fedha na Mali za Chama kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Chadema ( tz Katiba Toleo la 2006). Hivyo:
1. Chama kipya, Kama wewe si mwongo, mchochezi, many propaganda, weka hadharani vielelezo kuwa Mbowe na Dr Slaa wanalipwa mishahara hiyo. Mimi Kama Accounting Officer, na kwa mujibu wako mnufaika mmojawapo wa hiyo fedha sijawahi kulipwa wala kupokea. Njia ya kuondoa majungu na watu wakuamini ni kwa wewe kuweka hadharani nyaraka husika. Chadema hatutoi fedha Kama Karanga, kuna nyaraka nyingi zinahitajika hadi pesa, hata sentimmoja kulipwa. Hivyo weka hizo nyaraka jukwaani ili watu wakuamini. Vinginevyo wewe ni mwongo, na unaajenda yako, au kwa kutumwa.
2. Aidha Chama Kipya, ni kweli mkutano wa Jangwani una gharama, kwani Jukwaa ni gharama, viti hukodishwa, mikutano hutangazwa, hata kwenye harusi au sherehe yeyote ni hivyo hivyo, huhitaji elimu ya juu kuelewa hivyo. Lakini kwa makusudi imeamua kupotosha. Kiwango ulichokitoa ni cha uwongo wa kupindukia. Ili watu wakuamini na kukuona wewe ni wa maana, weka nyaraka za malice hayo ikiwa ni pamoja na fedha za posho ya viongozi na kukodi magari ya kubeba watu. Usipoweka hadharani watu wakuone mwongo, na mpotoshaji mkubwa na mharibifu wa demokrasia ya kweli katika nchi yetu.
3. Sababu unazotoa kuwa Mbowe anang'ang'ania uwenyekiti na kuwasemea vijana unawasemea vijana gani. Kwa utaratibu wa kawaida tu, ukikisemea kundi ni kuwa lilikutana mahali. Tuwekee hadharani ni kikao gani cha vijana kilifqnya tathmini ya utendaji wa Mbowe na kuweka azimio lililofikiwa kuwa " anang'ang'ania na akifanya watahama". Kikao hicho kilifanyika ukumbini gani na tarehe ngapi? Ukishindwa kuweka hadharani, ueleze umma wa Watanzania kwanini usikuone mwongo, mchonganishi, mharibifu na usiyetakia mema Tanzania na adui wa ukombozi wa kweli, kwani watanzania wengi wametoa Mali zao, damu Yao, wengine Leo vilema kwa ajili ya kupigania ukombozi wa pili nawe bila aibu unaleta hoja za kichonganishi na kipuuzi. Muda wa kubembelezana umeisha, na Kama nilivyosema, jukumu la katibu Mkuu ni pamoja na kulinda Taswira ya Chadema inapotaka kuchafuliwa bila sababu ya msingi na bila ukweli. Ukweli kwa mtu yeyote mstaarabu ni msingi wa kutoa hoja, Kama hakuna ukweli katika unayosema, jitafakari uhalali wa kauli yako!
4.Chadema ni chama chenye Katiba, Kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali. Kama unayoyasema yana hata chembe ya ukweli na Kama kweli una nia njema, weka hadharani Kama ulikwisha kuwasilisha malalamiko yako kuhusiana na hayo unayosema kwa chombo chochote cha maamuzi. Mbowe na Slaa siyo wa mwisho ndani ya Chadema. Wanasimamiwa na Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu. Weka hadharani kuwa malalamiko yako hayakufanyiwa kazi, yamepuuzwa, hukutendewa haki. Bila ushahidi huo, ni kwanini watanzania wasikuweke kwenye kundi la maadui wa Ukombozi wa Taifa hili. Tangu lini JF au chombo chochote kile Kama hicho kimegeuka kuwa chombo cha nidhamu ya chama. Kama hujui hata Katiba ya Chama chako, na taratibu za utendaji ndani ya Chama, hata vita dhidi ya ufisadi ambayo kwa muda mrefu chadema imesimamia na itaendelea kusimamia kwa Taratibu za kisheria, ndio maana hatuna uwoga, wewe utawezaje kusimamia misingi hiyo, Kama jambo dog Kama hili umeshindwa kulielewa.
5. Kwa manufaa ya wasomaji wetu, licha ya jukwaa, viti, Mkutano wa Jangwani ulichangiwa na vyama vyote vitatu, na formula ya kuchangia mkutano huo ilikubaliwa kwenye vikao rasmi na wala siyo barabarani Kama unavyotaka kuwaaminisha watanzania. Ni upuuzi kurukia vita na kuyapotosha kwa lengo lako binafsi. Kwa mujibu wa formula hiyo, Chadema ilipangiwa kugharimia mkutano huo kwa asilimia 57 na Kila chama kilipewa asilimia yake kwa kuzingatia vigezo mbalimbali. Kazi hizi zinafanyika kisayansi, tofauti na unavyofikiri na kundi lako. Kati ya hizo asilimia 57 sehemu kubwa ya matumizi hayo ilitumika kulipia matangazo ya moja kwa moja ya ITV ( live Transmisdion) ili ujumbe uwafikie Watanzania wote).
Sasa utuambie Kama Live transmission haikufanyika. Ni kwa msingi huo ninawaomba Watanzania kumpuuza Chama Kipya na wote wa aina yake, kwani kwa upuuzi wao huu wana nia tu ya kutuondoa kwenye hoja muhimu, na kujenga hisia ya matumizi mabaya ndani ya chadema, au kugombania vyeo. Narudia ten a, vyeo ndani ya Chadema ni dhamana na havigawiwi Kama karanga. Mtu atuhumiwe kwa utendaji wake mbovu, na utendaji mbovu hupimwa kwa vigezo dhahiri na siyo kwa hisia, au kwa " kuambiwa..." au " kusikia" Kama Chama Kipya anavyodhihirisha katika indigo lake.mapambano daima, na kwa dalili hizi naona ukombozi wa oil umekaribia, kwani hila hizi zimeshindwa hata kabla hazijaanza.