dullyhami
JF-Expert Member
- Jun 4, 2012
- 560
- 147
Ili miezi 3 mitatu bila umeme Zanzibar ni mibaya kuliko kipindi chote katika historia , watu walibakwa , waliporwa, makampuni makubwa na mahoteli ya kitalii yalifunga na kuondoka (mfano venta karibu hotel) bei ya mafuta ilifika elfu 5 kwa lita, majenereta yaliwafilisi wafanyabiashara na kuuwa familia nyingi kwa pamoja, bei ya bidhaa ilipanda, moto wa majenereta ulimuunguzia kila mtu makomputer yake pamoja device elektroniki zingine, bora vingetokea vita kuliko hali ile. Kosa lilikuwa usingizi mnono wa Serikali ya Karume na Waziri wake Shemeji Mansour Himid kwa sababu Waya unaoleta umeme Fumba toka Bara ulikuwa ubadilishwe baada ya maximum miaka 25, na ule ulikuwa umezidi 30, ndio maana kwa kuwazuga watu ili viongozi wasifikiriwe kunyongwa walileta burudani la Uamsho ili watu wasikilize show ya ndoto ya Nchi ya Zanzibar, na si haba watu walikubali show na serikali ya Karume pamoja na maovu na ufusadi wa kutisha unakumbukwa vizuri sanaaaa !!!
Nashkuru sana kwa kukubali kuwa Wazanzibar tulikibali show tulochezewa name karume na huo ndio uungwana wetu na daima tutauenzi, suala LA ubakaji na uboraji laweza kutokea kweupee na umeme wenu ukiwepo, lakini hoja Yang kwamba bado Waumgwana wa Kizanzibar twaweza kuishi bila ya umeme was Tanganyika, na wao hilo wanalijua maana Zanzibar tuliwasha umeme mapeema kabla ya hao wanojidai eti wanatuzamin umeme..