Habari nilizopewa kutoka chanzo cha uhakika, zinasema huenda Dr.Slaa ameamua kukacha kipindi hicho cha Azam TV baada ya Said Kubenea kutangaza jana kuwa atamuumbua na kuelezea ukweli wote juu ya kilichopo nyuma ya pazia baada ya uvumilivu kushindikana. Wachambuzi wa mambo wanasema huenda Dr.Slaa amepanga amsikilize kwanza Said Kubenea ili aweze kujipanga kujibu mapigo.
Jana Said Kubenea alitoa taarifa kwenye vyombo vya habari, kuwa sasa ameamua kukabiliana na Dr.Slaa kila hatua ili ukweli wote ujulikane kuhusu Richmond, na sakata zima la yeye kukikacha chama chake. Hii ilitokana na Dr.Slaa kumtaja Said Kubenea wkt akiwa kwenye mahojiano na Star TV siku ya Ijumaa.