Nyamizi
Platinum Member
- Feb 19, 2009
- 9,192
- 13,736
Pana kina Rev Masanilo,Rev Kishoka,Sikonge,Bubu ataka kusema (BAK),Gender Sensitivity (Regia Mtema RIP),Kada Mpinzani,Kiranga,Msanii,Kuhani Mkuu na wengine wengi.Jambo Forum enzi hizo ilikuwa moto wa kuotea mbali.Wakati najiunga JF nilikuta miamba inakata ishu si mchezo, alikuwepo Kichuguu, Mkandara, Mwafrika wa Kike, Mzee Mwanakijiji, Fundi Mchundo, Nyani Ngabu(sijui yuko wapi huyu mwamba), Bubu ataka kusema(BAK), Kuhani, njabu the dude, Phillemon Mikael, JMushi, Kiranga, Field Marshall ES (Sauti ya Umeme), Gamba la Nyoka na wengineo wengi. Wakati huo JK tukimuita Muungwana, na msemo Maarufu ukiwa "Kumkoma Nyani Giladi".
Topic pekee naikumbuka ni ilikuwa ya Mzee Mwanakijiji kwa Lowassa akiwa PM mpaka Lowassa uzalendo ukamshinda akamnanga Mzee Mwanakijiji Bungeni .Mzee Mwanakijiji akarudisha makombora hapa hapa akikejeli Uchumi kupaa,Mwafrika wa kike akaweka mchoro wa Ndege inapaa (uchumi) kisha ikadondoka ikitanguliza pua.Wapi Mwafrika wa Kike,ulinifanya nijiunge JF 2006 kabla ya kurudi tena 2009.