Wilaya ya Kisarawe, mkoa wa Pwani ipewe tuzo kwa kuhifadhi uoto wa asili na kutunza mazingira ijapokuwa miundo mbinu ni ya kizamani

Intelligence Justice

JF-Expert Member
Oct 23, 2020
3,039
3,486
Wanajukwaa

Mada tajwa hapo juu inahusika moja kwa moja kwa mjadala mpana.

Ombi kwa
1. Serikali kuu
2. Makamu wa rais muungano na mazingira
3. Tamisemi

Kwanza mamlaka husika ipongezwe kwa kutumia jeshi usu kusimamia mazingira ya eneo lote lla wilaya ya Kisarawe dhidi ya wavamizi na matajiri waporaji wa ardhi kwa ushawishi rupia kwa wenyeji wasio na ukwasi. Msitu wa Kazimzumbwi umedhibitiwa vuzuri sana kuanzia Vikindu Mkuranga hadi Kisarawe ijapokuwa kuna baadhi ya maeneo yanavamiwa kimya kimya na watu kisha viongozi wa kisiasa wa ngazi za juu wakipendezwa na maeneo hayo nao wananunua na kujenga kisha serikali kuhalalisha ukaaji watu.

Serikali isifanye kosa kama ilivyofanya kwa kuzembea msitu wa Mabwepande kumegwa kidogo kidogo hadi kwa sasa kimebaki kipande kidogo sana katikati ya makazi ya watu hivyo kushindwa kusafisha hewa za ukaa zinazozalishwa na uchafuzi wa mazingira, viwanda nk hata hali ya hewa inashindwa kuwezesha mvua za kutosha kunyesha maeneo makubwa ya mkoa wa Dar Es Salaam. Imebaki mvua inanyesha Mabwepande, Bunju, Tegeta, Madale, Msumi, Mbopo, Kinondo, Mbezi Msakuzi na Kwembe pekee.

Barabara ya lami iliyosimama tangu 2021 inayoelekea Masaki, Mkamba, Maneromango hadi mbuga ya utalii ya Nyerere huko Selous ikamilishwe maana wananchi wa huko wanalalamika sana kwamba wameikosea nini serikali yao? Huko ndiko mojawapo ya barabara utakuta mabasi ya miaka ya 70 na 80 (Leyland Albioni, Benzi) wanatumika kana kwamba hawana haki ya kwenda na mabadiliko ya vyombo vya usafiri vya kisasa.

Halmshauri ya wilaya ya Kisarawe itunzwe vizuri kimazingira ni urithi mzuri kwa vizazi vilivyopo na vijavyo kwa kuhifadhi misitu na uharibifu wa ardhi maana ndio eneo lililo juu sana katika usawa wa bahari
 
Wanajukwaa

Mada tajwa hapo juu inahusika moja kwa moja kwa mjadala mpana.

Ombi kwa
1. Serikali kuu
2. Makamu wa rais muungano na mazingira
3. Tamisemi
Kwanza mamlka husika ipongezwe kwa kutumia jeshi usu kusimamia mazingira ya eneo lote lla wilaya ya Kisarawe dhidi ya wavamizi na matajiri waporaji wa ardhi kwa ushawishi rupia kwa wenyeji wasio na ukwasi. Msitu wa Kazimzumbwi umedhibitiwa vuzuri sana kuanzia Vikindu Mkuranga hadi Kisarawe ijapokuwa kuna baadhi ya maeneo yanavamiwa kimya kimya na watu kisha viongozi wa kisiasa wa ngazi za juu wakipendezwa na maeneo hayo nao wananunua na kujenga kisha serikali kuhalalisha ukaaji watu.

Serikali isifanye kosa kama ilivyofanya kwa kuzembea msitu wa Mabwepande kumegwa kidogo kidogo hadi kwa sasa kimebaki kipande kidogo sana katikati ya makazi ya watu hivyo kushindwa kusafisha hewa za ukaa zinazozalishwa na uchafuzi wa mazingira, viwanda nk hata hali ya hewa inashindwa kuwezesha mvua za kutosha kunyesha maeneo makubwa ya mkoa wa Dar Es Salaam. Imebaki mvua inanyesha Mabwepande, Bunju, Tegeta, Madale, Msumi, Mbopo, Kinondo, Mbezi Msakuzi na Kwembe pekee.

Barabara ya lami iliyosimama tangu 2021 inayoelekea Masaki, Mkamba, Maneromango hadi mbuga ya utalii ya Nyerere huko Selous ikamilishwe maana wananchi wa huko wanalalamika sana kwamba wameikosea nini serikali yao? Huko ndiko mojawapo ya barabara utakuta mabasi ya miaka ya 70 na 80 (Leyland Albioni, Benzi) wanatumika kana kwamba hawana haki ya kwenda na mabadiliko ya vyombo vya usafiri vya kisasa.

Halmshauri ya wilaya ya Kisarawe itunzwe vizuri kimazingira ni urithi mzuri kwa vizazi vilivyopo na vijavyo kwa kuhifadhi misitu na uharibifu wa ardhi maana ndio eneo lililo juu sana katika usawa wa bahari
Daa umenikumbusha mbali sana kuhusu majina ya mabasi uliyotaja nikalikumbuka jingine lililokuwa likiitwa Austin sijui nalo liko huko Maneromango?
 
Wapewe tuzo pia kwa kuzalisha mkaa wote unahudumia mkoa wa DAR es Salaam na maeneo jirani huku wakijinasibu kutunza mazingira.
Viongozi wasio waaminifu wanatumia dhamana waliyopewa ya kiuongozi kujinufaisha na uharibifu wa mazingira, bajaji zinatumika kubeba mikaa kila uchwao, pikipiki ndiyo usiseme achilia mbali maroli yanayopewa vibali kila siku ili kukata na kubeba mkaa.
Ikiwa tunayo nia ya dhati ya kuhifadhi mazingira tuache kutoa hela mfuko wa shati na kuweka hela hiyo hiyo kwenye mfuko wa suruali tunajidanganya
 
Daa umenikumbusha mbali sana kuhusu majina ya mabasi uliyotaja nikalikumbuka jingine lililokuwa likiitwa Austin sijui nalo liko huko Maneromango?
Inawezekana mkuu lipo maana mengi ni yale yanayobeba mizigo juu ya 'carrier' halafu yakiwa yanapanda mlima yana yanasikika yakilalamika sana.
 
Wapewe tuzo pia kwa kuzalisha mkaa wote unahudumia mkoa wa DAR es Salaam na maeneo jirani huku wakijinasibu kutunza mazingira.
Viongozi wasio waaminifu wanatumia dhamana waliyopewa ya kiuongozi kujinufaisha na uharibifu wa mazingira, bajaji zinatumika kubeba mikaa kila uchwao, pikipiki ndiyo usiseme achilia mbali maroli yanayopewa vibali kila siku ili kukata na kubeba mkaa.
Ikiwa tunayo nia ya dhati ya kuhifadhi mazingira tuache kutoa hela mfuko wa shati na kuweka hela hiyo hiyo kwenye mfuko wa suruali tunajidanganya
Unawasingizia Kisarawe wanajitahidi sana. Unaowaona wakiwa na magunia wanatoka mbali Masaki, Mkamba nk ambako wanakuwa wanasafisha mashamba kwa kupunguza miti ya mikorosho.
 
Unaifahamu Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe au unaifahamu Kisarawe kama kata ya Kisarawe iliyozungukwa na misitu ya Pugu?
Kusafisha mashamba wanapata magunia na magunia full season of the Year?
Vijana wa ccm mna akili mbovu sana!
Niambie kama kuna siku mikaa haipiti Kisarawe,hayo mashamba ni kila siku?
 
Back
Top Bottom