Mtu kupewa gifts haimaanishi kuhongwa. Ni vyema mambo haya mawili yakatenganishwa haswa tunapojadili katika muktadha (context) ya mahusiano ya kimataifa. Kuhonga ni kwa njia ya kurubuni na kushawishi uamuzi kupindishwa ili kumnufaisha mtoaji wa hongo. Wakati zawadi ni utamaduni wa ukarimu (courtesy) ambao umekuwepo enzi na enzi hata katika mfumo wa tawala za jadi za kiafrika. **<br /><br />
<br /><br />
Katika ulimwengu wa *mahusiano ya kimataifa-iwe kwenye biashara au diplomasia-kutoa na kupokea zawadi ni utamaduni wa kawaida kabisa. Utamaduni huu uko dunia nzima. Wazungu kutokana na tafsiri yao ya ukarimu wanatoa sana vitu vidogovidogo ambavyo ni alama zaid maarufu kiingereza kama &quot;peniphenalia&quot;. Watatoa kalamu zenye nembo ya kampuni nk ambazo ni za gharama kubwa sana ikitegemeana na hadhi (reputation) ya kampuni yenyewe. *Kwa waarabu na Watu wa far East utamaduni huu upo institutionalized pia. Wao hutoa chochote na kitendo cha kukataa ni kitendo cha udhalilishaji na fedheha kwao. Wazungu au watu wa Magharibi na Waasia au watu wa Mashariki wanatofautiana namna na aina ya zawadi hizo lakini wote wanatoa. Sisi pia Tanzania tunatoa, kiongozi akipita majimboni mwetu tunamkamatia kuku na kumfungashia viroba vya matunda au mihogo kama &quot;good will&quot; na sio rushwa. Makampuni makubwa ya kimataifa nao wana desturi hiyo katika kujenga mahusiano. <br /><br />
<br /><br />
Hivyo kama kweli albawadi alimpa zawadi foreign minister wala sio jambo la ajabu....ipo mifano mingi ya viongozi kupewa zawadi za aina mbalimbali.....huko nyuma kikwete alipewa zawadi za magari ya kubebea viongozi na ndizo zimekuwa zikitumika serikalini mpaka kesho. *Hata Salim A Salim alishawahi kupewa magari alipokuwa waziri, akayatoa jeshini. <br /><br />
<br /><br />
Tukiachilia suala la gifts, kwa nafasi ya waziri wa mambo ya nchi za nje-moja ya kazi zake ni kutekeleza diplomasia ya uchumi ambayo inajumuisha kuwaleta wawekezaji nchini. Na si jambo la kushtusha kuwa mwekezaji yoyote atakutana na Waziri wa Mambo ya nje kwanza au Rais kwa kuwa wawili hawa ndio taswira ya nchi yeti nje ya nchi. Mwekezaji wa Nje ambaye hajafika nchini, Sura ya kwanza atakayokutana nayo huko nje ni aidha ya Balozi kama tuna uwakilishi katika nchi anayotoka au ya Waziri wa Mambo ya Nje. Wakishaingia tu hapo kazi yake inaisha. Kinachobaki ni institutions za ndani kuendelea na michakato ya kushughulikia uwekezaji huo...TIC,PSRC etc. Kupewa zawadi foreign minister hakuwezi kusaidia mtu kuuziwa hoteli ....sababu waziri huyo hana dhamana ya uwekezaji wala ya mamlaka ya kuamrisha Wizara nyingine au Taasisi ya Serikali kumkubali au kumkataa mwekezaji. Wizara ya Mambo ya Nje ni mratibu tu.<br /><br />
<br /><br />
Lakini pia hii wikileak story hailezi chochote Kama jk as an individual alikuwa na mahusiano ya aina ipi na albawadi , pengine ni rafiki yake, sasa kukimbilia conclusion kwamba amehongwa ni insult -kwa nature ya kazi yake-foreign minister anaweza kupita uingereza hata mara 20 kwa mwaka,kwa kazi mbalimbali ziwe bilaterals, commonwealth, trade missions-achilia mbali transit visits. *Posho ya foreign minister inatosha kununua suti zaidi ya pair zinazotajwa kila anaposafiri. Kama ni hongo ni inaingia akilini tu kama itakuwa zaidi ya kile Foreign Minister anachokipata kama lengo la rushwa ni kumshawishi apindishe maamuzi.<br /><br />
<br /><br />
Mimi nadhani kabla ya kujadili thread hii kwanza tujifunze utamaduni wa economic diplomacy ukoje ili tufahamu desturi zake na tamaduni zake. Economic Diplomacy imeazima tamaduni nyingi kutoka katika corporate world. Ili kuyaelewa mambo mengine lazima tufahamu muingiliano wa tamaduni (cross-cultural interactions) na tafsiri ya tamaduni tofauti juu ya desturi tofauti. **Hapo ndipo tutakapokuwa *greathinkers wa ukweli