Naifahamu ukerewe, nimewahi kufanya field kule. Ni wilaya isiyotofautiana na wilaya nyingine zote za nchi yetu hasa zile za vijijini. Imeshapata umeme wa grid ya taifa tokea mara.
Madhali ni kisiwa usafiri unaounganisha kisiwa hicho ni wa maji na anga. Kuna meli za kutosha:- mv butiama, mv clarius, mv kipepeo...kwa upande wa mwz-uk. Na pia kuna ferry kwa upande wa kisolya(bunda)-lugezi ukerewe. Wana barabara chache za lami kama zilivyo w nyingine. Uwanja wa ndg hautumiki kulingana na hali halisi na hautofautiani na mazingira ya sehemu kubwa ya Tz.
Ushirikina si lolote tena pale kisiwani maana watu wanasoma na kufaulu kwa idadi kubwa. Zamani walikuwa wanapewa nafac 70 za kati ya shule 80, kwa wanafunzi wanafaulu kwenda sec schools. Siku hizi pamoja na shule za kata wana sec school nyingine km:- kagunguli, murutunguru, bwisya, nansio kwa kutaja nnazokumbuka. Wanajenga nyumba za kisasa na hasa kutokana na uvuvi maarufu kama MMAJOLHO! Hili la nyumba na kusoma, kwa zamani ungerogwa kwa mjibu wa maelezo yao!
Anyway inatosha kusema kuwa wikileaks hawapashwi kuaminiwa kwa kila wanachosema. Ntarudi kwa takwimu mnawara. Ngoja umeme urudi nichukue laptop yangu.