Wife Anazingua

Wife Anazingua

Mkuu mkubalie tu kwa hili, tafuta tu hekima yakuelezea juu ya jambo hilo, na usikubali HG ndoa itapotea mwache tu afanye hizo kazi ni wajibu wake hasa kama hafanyi kazi za ofisini. kama ni mfanyakazi basi mwambie atafute yule anayetaka yeye aca kng'ang'ana et tu kwa sababu ewe ni mwanaume

ndoa kazi....n'way alishastuka kuwa unaweza kupita,pengina anajua una kauzoefu hako

Sasa kumbe kama ni mama wa nyumbani huyo house girl ni wa nini wkt mimba yenyewe ni ya mwezi mmoja? mrudishe huyo house girl then usijihusishe tena katika mambo ya kutafuta atakapohitaji,yawezekana mimba inamuendesha so hajui anataka nini!

Nlimaanisha mimba ya kwanza sio ulivyoelewa wewe.

Binti ni mdogo haiwezi ikawa wivu
 
kaka nakushauri tu umrudishe mtoto wa watu!

la sivyo utamkuta kaunguzwa na maji ya moto bure!

yani ni bora ungelimchukia wewe kuliko mkeo!

wanawake si wanawake wale wa kale siku hizi... kitu kidogo tu unakuta mtu kateketezwa na maji ya moto kabisa!
 
Wakina mama saa nyingine ni kuwaombea tu, siwaonei ila wanapenda sana kufanya maamuzi kwa hisia kuliko hali halisi.
 
Mh!we unamng'ang'ania wa nn?akiondoka kazi c anafanya mkeo?kuna kitu mkeo atakua ame hisi kati yako na hg!hta mm nishahisi!hii kauli hii,kama anaenda na aende heheeeee!somethng is wrong somewhre!

Passion lady huyo mke wa jamaa ana matatizo yale binafsi, haiwezekani tumlete hg toka mbali hivyo then after 1 week arudi kwao, kwanini huyo mke asijiamini? Najua mnamtetea coz ni ke mwenzenu lakini ukweli anamihaibisha mme wake kienyeji, km ni mimi mke asepe asitake kunipanda kichwani, maana hata akija mwingine itakuwa hivyo daima, nina mifano halisi ya suala hilo.
 
Naona umeona yasiwe makubwa kijana. Maamuzi mazuri ulofikia nakusifu.
 
Habari MMU.

Jumanne jioni tulipata mgeni nyumbani kwetu (Housegirl). J5 asubihi nkamuacha wife na hsg home nkaenda kazini. Kabla ya kumleta yeye ndiyo alikuwa anamtaka na kusistiza ni muhimu atusaidie shughuli za hapa Home anachoka sana. Alionyeshwa picha tuliyotumiwa kwa email na kumhoji maswali kwa simu kabla sijatuma nauli (100,000) aje. Hsg katoka mbali sana Bukoba tulimpata kutokana ya kuwa ni mdogo wa Hsg wa rafiki yangu.

Cha ajabu ni kuwa toka alhamis wife aliniomba tumrudishe kwao eti hamtaki, mi nkamsihi ampe mda amzoee. Aliendelea kusema hamtaki mpaka jana usiku ukazuka ugomvi mkubwa kati ya mimi na yeye. Mwanamke haelewi kasimama kidedea Hsg aondoke. Hakuna kosa alilofanya mdada wa watu tena mpole sana. Namuuliza mke wang tatizo ama kosa lake hana hata moja anachojua yeye binti arudi kwao. Eti jamani utamfukuzaje mtu bila Kosa?

Mpaka sasa sababu kubwa ni kuwa roho yake inamchukia na anahisi si mtu mzuri. Kwa kuwa namtetea na sioni mantiki ya Hsg kufukuzwa jana kazusha kuwa nimempenda na nataka nitembee nae. Kila ninalomwambia aelewi mpaka sasa yeye kang'ang'ania Hsg lazma aondoke. Naona aibu kwa rafiki yangu aliyotutafutia kumrudisha tena kwako huyu bint tena bila kosa. Pia sitaki wanaume wenzangu ambao wananikubali waone kuwa naburuzwa na mwanamke.

Kilichonifanya niandike hapa ni kuwa kasema kama Hsg haondoki mpaka kesho basi ataondoka yeye aniache naye. Mimi nafikiria kukomaa kama anaenda na aende sitaki anipande kichwani au nakosea? Nishaurini jamani maana tatizo ni kwa nini analotaka lake na ni lazma liwe?



UPDATE


  • Ahsanteni sana kwa ushauri wenu ingawa ni tofauti na nlivyofikiria nimefuata mawazo ya wengi.
  • Nimeongea na rafiki yangu aliotutafutia na alimuomba nimpeleke kwake na ndivyo nlivyofanya asubui hii ya leo nimempitisha ninavyoenda kazini, Kwa sasa binti yupo na dada yake kwenye nyumba moja.
  • Kuna wengine walihoji kuhusu hsg kuwa na email, Mkisoma maelezo hapo juu utajua kuwa dada wa hsg tuliyeletewa anafanya kazi kwa rafiki yangu, Picha ilitoka kwa dada yake na best yangu ali scan na kututumia ili tumu aprove kabla hajaja. Wife aliiona picha na kuongea naye kwa simu.
  • Mpaka sasa hana sababu yeyote ya maana ya kumkataa.
  • Kwa mlioomba Hsg kidogo itakuwa ngumu, best kakataa kwa usalama wa binti maana yeye ndio anawajibika kwa wazazi wake.


Mwisho wa yote nilijishusha na kukubali kushindwa. Leo nimefanya anavyotaka yeye sasa namsubiri kwa hamu aanzishe jingine tena.
Ahsanteni kwa mawazo yenu. Si mjaji wa huku sana hivyo sitaweza kujibu maswali yenu papo kwa hapo.

Mwanaume inatakiwa ukomae,ukishaonyesha unatetereka kwenye misimamo yako itakuletea matatizo,leo unasema hivi kesho unabadilika unasema hivi,inatakiwa uwe na msimamo!
 
Aisee.................. hivi mwanamke unaanzaje kumshutumu mumeo kuwa anataka kummega msichana wa kazi (au mwanamke mwingine yeyote) unaanza tu? Au ndo unakuwa umeshawahikumfumania ndo unajua ni tabia yake? Mie naona kama ni kumvunjia heshima mwenzi wako vile!! mwe au pengine mie mapenzi nayasoma kulia kushoto
 

lakini ujue mke ndio anashinda
na beki tatu muda wote,huenda kuna
mapungufu kayaona,ma hg wana mambo nyie hamjui tu
arudishwe thn mke atafute hg amtakae.coz hiyo ni kazi ya mama na si ya baba!!
 
Back
Top Bottom