Salaam,
Niende kwenye mada hapo juu Mimi niko America toka 2023 nabeba box, awali ilikua kila siku wife anapiga tunaongea hata mda mfupi wa break (naingia night shift)sasa hiv mpk mimi ndo nipige simu.
Mbaya zaidi weekend hii imepita hatujaongea hajali, tatizo kubwa lilianza pale alipotembelewa na dada aliyenitambulisha ni mamdogo mimi ndugu zake wote siwajui, nifanyeje?
Sitaki hii familia isambaratike tuna watoto wawili na kila mwez natuma 1.4 matumizi, wanakaa nyumba nzuri peke yao, wazazi wapo mkoa mwengine.
Huyu mamdogo nimefukuza kesho anasepa, hata hapa sa hivi wife hapokei simu.
Ushauri please!!
Nisikilize mimi:
Nilikwenda kusoma US. Nikaacha pisi ya Kichaga mbichi ndo tu kwanza inaanza kuitambua dunia (Mama E usicheke!). Na kabla sijaondoka nikahakikisha naipachika mimba kabisa nikidhani eti itatulia. Eee bana eeeh!
Wanawake ni viumbe wa hisia. Na kama wewe haupo basi haupo tu! Masela lazima wapige. Utatuma pesa na makorokocho kibao mpaka uchoke lakini hakuna mbadala wa wewe mwenyewe kuwepo. Siyo wanawake wote wako hivyo lakini utakuwa na bahati sana kubahatisha mwanamke ambaye hutakuwepo na bado akawa loyal kwako na kukuheshimu. Labda Mama E tu!
Pisi yangu ya Kichaga iliolewa na mimba yangu aisee...nami baadaye kibabe tu nikarudi nikachukua kibinti kimalaika changu nikasepa nacho US. Mpaka ninapoandika hapa kibinti changu hiki nilichopambana nacho tukiwa wawili tu na Mungu wetu sasa kipo mwaka wa pili Medical School John Hopkins University lengo kuu likiwa ni kuwa pediatric cardiologist mbobevu! 🙏🏿
Mamake huku Bongo nasikitika mambo hayakwenda vizuri sana. Tajiri wa madini aliyemuoa alimuungisha kwenye grid ya taifa; akaondoka na kumwachia watoto wawili. Ni mama wa binti yangu na tungali marafiki sana. Ndiyo. Kuna majuto ya hapa na pale. She was my first true love (wa pili ni Mama E); na huwa ananilaumu sana kwamba kwa nini nilimwacha nikaenda kusoma. Nami huwa namlaumu ni kwa nini hakuvumilia japo semester moja tu ili nije kumchukua kama tulivyokuwa tumeahidiana. Kwa bahati mbaya. Majuto. Ni. Mjukuu!
Angalia usije ukatumika sana. Wewe unapiga box unateseka lakini watu huku Bongo wanatanua hatari. Nilinunua kiwanja Kigamboni nikaanza ujenzi kumbe hakuna kitu. Lots of dough wasted. Usiwe kama mimi; na usimwamini mtu hata kama ni ndugu wa damu moja. Siku hizi hakuna undugu!
Na ukija kurudi Bongo bila kuwekeza sawa sawa utachekwa mno hata na huyo mkeo na ndugu zako ambao unawatumia pesa kila leo na kuwapambania. Tunza fedha zako. Wekeza kwenye miradi isiyohitaji third party mf. Bonds. Hudumia wanao lakini kwa uangalifu ili usitumike sana. Be frugal....
Mkeo likely ana baharia mwingine anaymtimizia mahitaji yake ya kihisia na kimwili. Au tu hisia kwako zimekata kutokana kutokuwepo kwako.
Kama unampenda na ni mama mwema kwa watoto wako unaweza ukamvumilia ila hakikisha unakuwa naye na wanao physically. Ama uende nao US au urudi Bongo kama umeshajilimbikiza japo $500,000. Na kama mkeo ana kichwa kidogo jiandae hata kuuliwa ili hizo hela unazozihangaikia waje wazile na mama zake wadogo, mashangazi na huyo mwanaume wake aliyenaye.
Kwa kilichonisaidia mimi, njoo inbox nikupe datails zaidi kuhusu ambacho unaweza kufanya lakini kwanza itakulazimu uwe na Emotional Intelligence kubwa na uwe unajitambua.
Pole!