Heshima zako kaka MN! Nastahili kukugongea likes za kutosha ila nmebanwa na mtandao hapa.
Ndugu yangu Ruta na wapendwa wengine, njia pekee ya chama chetu kipendwa ambacho kiliwahi kuwa cha wakulima na wafanya kazi ni kukiondoa kwenye dola. Wakiwa pembeni nje ya dola wao watajenga chama chao na sisi tutajenga nchi yetu!
Ni uasi dhidi ya historia kutumia rasilimali za taifa eti kujaribu kutatua migogoro ndani ya chama cha siasa.
Kuna kamtazamo bado kapo miongoni mwa watz wengi hasa baadhi ya watumishi wa umma, TISS na wazee wengine eti bila ccm nchi haitasonga, hvyo kundi hili la watu limekuwa busy kutumia kila mbinu kuwa nchi inabaki mikononi mwa chama hchi ambacho ni chenyewe tu ndio kinaelewa kinapotupeleka. Chama hicho hakina nafasi tena ya kuendelea kushika dola kwa matumaini kuwa huyu atabadili hali ya chama,
je nchi itakuwa wapi??
Watanzania hatuchagui raisi kwa matakwa ya Kikwete wala mtu mwingine yeyote aliyoko madarakani, aidha hatuchagui raisi kwa jinsia yake, dini yake, rangi yake wala kabila lake kwasababu haendi Ikulu kuimarisha dini yake, kabila lake wala rangi yake kwa hiyo basi swala la zamu ya muislamu ni "out of point". Sijashindwa kumtaja mwanamke anaye faa na asiye na tuhuma. Sijataja kwa sababu sipendi kuwaangalia hao walioko huko juu tu, waache CCM kama kweli wanania nzuri na nchi hii waachie demokrasia ifanye kazi. Mchakato uanzie "grassroot", mizengwe iachwe, nakuhakikishia mr Ruta, tutapata kiongozi aliyebora na sio hao watu unaowapigia debe saa hizi.mimi simpigii mtu debe ninangalia mazingira yalivyo ya kisiasa na jinsi ccm inavyoweza kujipanga upya...................wanawake wemgi waliopo ninasikitika hata wewe umeshindwa kumtaja hata mmoja kwa sababu wenye mandhari ya mvuto hawapo..................
Dr. Asha Rose Migiro ilooks too lethargic and continuation of another ten years of a Moslem is unthinkable.................................part of JK campaign in 2005 ilikuwa ni zamu ya Muislamu sasa unafikiri hiyo hoja ilimnufaisha yeye pekee yake?
Kwa Taarifa yako Asha Rose Migiro ndio CCM wanamwandaa 2015
Tuombe Uzima
kimsingi ninakubaliana na wewe lakini shilingi ina pande mbili....................................usifikiri ccm itaachia tonge la ugali without a fight....................kwa hisia zangu huu ndiyo mkakati wa kuwabakisha madarakani..........................ingwaje hata mimi ningependa wadondoke......ili wajifunze kumheshimu mpigakura...................
tatizo ni mfumo wa kupata viongozi......................atakachotusaidia ni kubadilisha katiba kazi ambayo miaka minne ijayo haitafanyika kukidhi kiu iliyopo hususani ya kuleta uongozi shirikishi katika kupata viongozi madhubuti......................mfumo uliopo ni wa kujuana tu.
I believe we need a transition period...........................and she can fit in as that transformational figure that will encompass the opposition too.............It is not easy to discard ccm altogether no matter how virulent the party has turned out to be................
Mpaka sasa huyu mama kuna lolote la maana kalifanya hapa Tanzania?
Watu wanauwana kwenye kugombea viwanja kama kawaida na huku yeye ndiye Boss.
Huyu mama ana huruma sana kuwa Rais wa nchi mbovu kama Tanzania na hasa hapa tulipo.
Tunataka mtu ambaye atachokonoa hadi nyoka pangoni mwake kwa moshi wa mti mbichi ambao utawaka kwa miaka 5 bila kukoma.
Tunamtaka Putin/Kagame wetu Tanzania aje asafishe. Huyu mama huwezi kumuona hata siku moja akimuweka ndani Mkapa au Lowassa.
wa nini? Kulikuwa na transition period Zambia? Kenya je? wacha kuwa muoga wa kufikiri ndugu yangu. Dare to think the impossible, dare to be different. Be bold! Nani alidhani mwisho wa huu mwaka Gaddafi angekuwa hapo alipo?hahahaha
Nadhani ungemwita huyo mtu kichaa!
kwa hiyo na yeye amefikaje hapo? Ivi wewe kweli unaamini kuna msafi ccm? ndugu yangu, kile chama kimeoza. Hakuna anayefaa kuongoza nchi yetu pale. Kama kweli ni wasafi, basi watoke huko....
Nchi ina matatizo mengi sana: misingi yetu ya elimu ya chini ni mibouvu, hali ya maisha ni ngumu (kwa watanzania halisi na si wa humu JF, wengi humu ndani ni longolongo tupu hila ukweli wenyewe a majority are somewhat comfortable), ajira zinachukuliwa na wageni kwa kisingizio wazawa are unprepared for the job market and we have poor work ethics, economical development plan amna despite all the natural resources we have been blessed with.
So far amna kiongozi yoyote anaeongea like a politician despite all the social problems facing us, sisi tumekazana tu na zamu sijui ya nani lakini the important aspect of a good politician is never mentioned someone who talks about his economical plans which will take us from where we are into the next stage of our development and how he/she intends to accomplish those goals. Aren't we tired of political slogans without action plans.
Embu tuache siasa za maji taka sujui nani anatufaa atuhitaji majina au elimu ya mtu kutishika what we need is a serious politician na so far no one as stood up above the rest.
Sitaki kukufundisha cha kusema ila kwa maslahi ya Tanzania tunayoitaka ingekuwapoa sana kama tungeweka mijadala ya namna gani ya Tanzania bila CCM, hili la mgombea bora wa ccm 2015.... dah sijui nalionaje maana kwangu hata waweke malaika bado sitamuamini na atashindwa tu kufanyakazi kimazingira na nature ya siasa za chama chao....
Watanzania hatuchagui raisi kwa matakwa ya Kikwete wala mtu mwingine yeyote aliyoko madarakani, aidha hatuchagui raisi kwa jinsia yake, dini yake, rangi yake wala kabila lake kwasababu haendi Ikulu kuimarisha dini yake, kabila lake wala rangi yake kwa hiyo basi swala la zamu ya muislamu ni "out of point". Sijashindwa kumtaja mwanamke anaye faa na asiye na tuhuma. Sijataja kwa sababu sipendi kuwaangalia hao walioko huko juu tu, waache CCM kama kweli wanania nzuri na nchi hii waachie demokrasia ifanye kazi. Mchakato uanzie "grassroot", mizengwe iachwe, nakuhakikishia mr Ruta, tutapata kiongozi aliyebora na sio hao watu unaowapigia debe saa hizi.
Ndugu yangu Rutashubanyuma, naona unasahau kuwa Mhaya haruusiwi kuwa kiongozi wa ngazi ya urais, kadhalika Msukuma na wale wote watokao katika makabila makubwa hapa Tanzania!Mkakati wa kujivua gamba unaelekea kuwa sasa ni kioja ndani ya ccm kwa sababu una matatizo ya ujumbe na wajumbe wenyewe kwani kuna migongano mikubwa hapo...ingawaje mjumbe hauwawi...
ujumbe wa kujivua gamba una walakani kwa kuwa siyo sera ya chama na mkakati wake siyo shirikishi...matawi ya ccm hayana taarifa na hayajui kinachoendelea....vivyo hivyo mikoani na wilayani tatizo ni hilo hilo hawajui...kipi kinaendelea...
pili uteuzi wa safu mpya ya uongozi wa juu ndani ya ccm pia ni matashi ya viongozi wa juu na huku chini wanaona wanaburutwa tu...haya si mazingira ya kukiaanda chama kubaki madarakani....na isitoshe baadhi ya vinara wa ufisadi wameachwa kundini...
mbinu za kukisafisha chama yaelekea nahivyo kueleweka na wengi ya kuwa lilikuwa changa la machoni kwani vinara wa ufisadi bado wanaendelea kutesa ndani ya chama hicho na wengine wamepata ujasiri hata kuanza kujenga ngome za kujiandaa kutwaa nchi...kwa nguvu ya pesa na na kwa gia ya dola...lakini hawaungwi mkono na wapigakura...
lakini wenye uwezo wa kutafakari ndani ya ccm wanaamini ya kuwa yaliyotokea katika uchaguzi wa 2010 hayawezi kujirudia tena mwaka 2015...ccm haiwezi kuendelea kutegemea kuokolewa na TISS na NEC katika uchaguzi ujao...
mbinu za ujumbe wa nguvu mpya, kasi mpya na ari mpya wengi wa wapigakura sasa wameushtukia kwa sababu hakuna mabadiliko na viongozi huendelea kuwa wale wale kwenye ngazi zote na hivyo kufifilisha matarajio ya wananchi....kuwa kuna malengo kweli ya kubadilisha mwelekeo wa taifa kutoka hadhi ya kujuana na kujali sifa za wahusika ili kusukuma kwa kasi maendeleo ya taifa...
kutokana na mazingira tajwa wapo wanaoamini ya kuwa mwanamke mwenye taswira ya mvuto ndani ya ccm anaweza kuwa karata ya mwisho ya kumalizana na Dr. slaa na Chadema yake...mwanamke huyo awe ana sifa zifuatazo:-
1) Asiwe na tuhuma hata moja ya ufisadi katika utumishi wake wa umma.
2) Awe Mkristu kuendeleza azma isiyo rasmi ya wakristu na waislamu kupokezana kiti cha Uraisi ndani ya ccm kwa hoja ya kujenga umoja na mshikamano bila ya kubaguana kwa misingi ya udini, ukabila au jinsia....au tofauti nyinginezo kama katiba inavyobainisha.
3) Asiwe Mnzanzibara kwa sababu wao wamekazana kuonyesha hawana imani na serikali ya Muungano kwa kurekebisha katiba yao na kujipa madaraka makubwa ambayo yanaonyesha dhahiri kuwa wanataka kujitenga...huwezi ukaendelea kuwaamini watu na masuala ya Muungano watu ambao wanadai wao ni nchi....hata hizi hongo za kuwapa vyeo kwenye masuala yasiyo ya Muungano kama u-R.C zina harufu kali ya rushwa za kisiasa...
4) Awe ni mwanamke ambaye ni mcha Mungu ili kuonyesha kwa vitendo ya kuwa kweli hizi ngonjera za ya kuwa wanawake wanaweza zinatoka moyoni.....mwanamke mwenye kashfa za ngono au mwenye tabia ya kulonga hovyo atakuwa mwiba kwa ccm...chadema watamrarua vilivyo...
5) Awe ndani ya baraza la mawaziri la JK la sasa kuonyesha ya kuwa uongozi wa kitaifa ni endelevu...hili pia litasaidia kuwatoa hofu washirika wa ufisadi ya kuwa hakuna lengo la siri la kuleta mtu mpya atakayewashughulikia....
6) Prof. Anne Tibaijuka hakuwa na upinzani katika kiti chake cha ubunge na hakuhitaji kuwawekea wapinzani mapingamizi kama viongozi wengi ndani ya chama cha magamba walivyofanya ili kujinusuru na hasira za wapigakura...huu ni uthibitisho ya kuwa hata vyama vya upinzani hususani Chadema vinamheshimu kwa sababu anajiheshimu mno...
kwa mbinu hizi ccm itatesa kwa kipindi kirefu sana....toa maoni yako bila ya shaka yoyote.......
Umesahau kidogo mkuu, pamoja na kuchagua sura pia tunachagua chama maslahi ya taifa baadae!Ruta, Huyu mama Tibaijuka ni hatari sana kwa CCM kwa sababu she is for real, CCM haihitaji watu ambao there are for real, inahitaji watu wanaojua kupiga zengwe.
Kwa taarifa yako, Mama Tibaijuka, ameshapeleka mezani kwa JK, maombi ya kuvifutia miliki, viwanja vyote vya wazi ambavyo CCM imejimilikisha, akamsisitizia JK lazima avifute ili itakapo kuja kuwafutia umiliki wale wote waliomilikishwa maeneo ya wazi kuijanja ujanja, kusiwe na mahali pa kulilia. Sasa kama mtu huyu ndio kwanza anataka kuipokonya CCM mtaji wa kujivunia, unategemea nini?.
Prof. Tibaijuka akipewa urais, kwanza atamfikisha Ben mahakamani kwa kufanya biashara Ikulu, pia anaweza kumfikisha JK mahakamani kwa kuifanya Ikulu ni pango la walanguzi!. Huyu sio mtu wa kuaminika hata kidogo!.
Dr. Migiro pia ni kama Mama Tibaijuka kwenye ukweli, tatizo la mama Migiro, nae zengwe, fitna na unafiki hana, ambazo Dr. Migiro hana, hivyo hana sifa zinazohitajika CCM.
Mtu kama Magufuli ni hatari zaidi kuliko hao wote, anaweza kabisa kuwa dictator, ni mtu asiyeheshimu kabisa sheria, taratibu na kanuni, yeye hufikia maamuzi kwa utashi wake, kule Mwanza alivunja petrol station, serikali ikalipishwa mabilioni ya fidia. Serikali itakula tena hasara hivi karibuni kwa kulipishwa mabilioni ya fidia ya wale samaki wa Magufuli, hivyo naye hafai kabisa.
Kwa vile rais mpendwa wetu ni JK, CCM inamhitaji mtu kama JK, na kati ya waliopo, ambaye ni kama JK ni Membe, tena anamzidi JK kwa vile JK ni Mswahili, Membe sio mswahili. Kisifa, wanaendana, kitabia wanaendana, hata kimuonekano, wote ni ma HB, hivyo wanaendana, msiwe na wasiwasi kuhusu uwezo, Watanzania hatuchagui uwezo, tunachagua sura, kwa 2015, sura ya kupendeza ni Membe Pekee!.
Serikali ya Tanzania haina dini hilo lipo kikatiba, sioni kwanini dini ichukue ujiko hapa. Hata hivyo watanzania tusio na dini au ambao ni "atheists" tutawakilishwaje kama kweli dini mhimu kiasi hicho. Tukubaliane kimsingi kama marehemu Nyerere kwamba tumchague kiongozi kwa uwezo wake na sio dini yake. Visingizio vya dini, jinsia, usawa, kabila n.k. mara zote huletwa na watu au viongozi mbao huwa wamebeba agenda za siri nyuma yao. Hili lilifanywa na mafisadi katika kumuengua fisadi mwenzao katika kugombea uspika wa bunge la muungano. Lilirudiwa ktk uchaguzi mdogo wa Igunga waliponyapalia swala la hijabu ya mkuu wa wilaya. Watanzania tukatae mitazamo hii. Tumewakosa viongozi wengi wazuri kwa ujuha huu, ofisi inaongozwa hovyo kwa sababu kiongozi aliwekwa sio kwa ubora na uwezo wake bali kwasababu ni mwanamke, shit!mawazo mazuri sana lakini yanahitaji kusukumwa hasa lile la kuwashirikisha grassroots kwenye zoezi la kumchagua Raisi kupitia vyama vyao vya siasa badala ya kuwaachia powerbrokers............lakni kuhusu dini, jinsia, kabila n.k huwezi kuyakwepa kwa sababu hata huko nyuma nafasi zilikuwa zinagawiwa kwa kuzinatia vigezo hivyo...............................na hoja ya muhimu ni kuwa sote tunaweza sasa haiwezekani upande mmoja uonekane ndiyo unaweza zaidi iwe jinsia, dini, kabila rangi n.k.............................upende usipende hivyo vigezo vitaendelea kutumika ili kuleta maelewano ya kitaifa.........................................
mawzo mazuri lakni siasa na mchezo wa kulinganisha Putin na kagame sio watanzania na Raisi lazima awe mmoja wetu..........................kuhusu kuuana kwenye viwanja si ndiyo kaanz a kazi hata miaka miwili bado.........................miaka ya tisini alisaidia kuanzisha BAWATA ambayo Rose Asha Migiro akiwa waziri wa wanawake na watoto alifuta na kesi hadi leo ipo mahakamani ikisota...................BAWATA lilikuwa chombo cha kumkomboa mwanamke.............
Ruta, Huyu mama Tibaijuka ni hatari sana kwa CCM kwa sababu she is for real, CCM haihitaji watu ambao there are for real, inahitaji watu wanaojua kupiga zengwe.
Kwa taarifa yako, Mama Tibaijuka, ameshapeleka mezani kwa JK, maombi ya kuvifutia miliki, viwanja vyote vya wazi ambavyo CCM imejimilikisha, akamsisitizia JK lazima avifute ili itakapo kuja kuwafutia umiliki wale wote waliomilikishwa maeneo ya wazi kuijanja ujanja, kusiwe na mahali pa kulilia. Sasa kama mtu huyu ndio kwanza anataka kuipokonya CCM mtaji wa kujivunia, unategemea nini?.
Prof. Tibaijuka akipewa urais, kwanza atamfikisha Ben mahakamani kwa kufanya biashara Ikulu, pia anaweza kumfikisha JK mahakamani kwa kuifanya Ikulu ni pango la walanguzi!. Huyu sio mtu wa kuaminika hata kidogo!.
Dr. Migiro pia ni kama Mama Tibaijuka kwenye ukweli, tatizo la mama Migiro, nae zengwe, fitna na unafiki hana, ambazo Dr. Migiro hana, hivyo hana sifa zinazohitajika CCM.
Mtu kama Magufuli ni hatari zaidi kuliko hao wote, anaweza kabisa kuwa dictator, ni mtu asiyeheshimu kabisa sheria, taratibu na kanuni, yeye hufikia maamuzi kwa utashi wake, kule Mwanza alivunja petrol station, serikali ikalipishwa mabilioni ya fidia. Serikali itakula tena hasara hivi karibuni kwa kulipishwa mabilioni ya fidia ya wale samaki wa Magufuli, hivyo naye hafai kabisa.
Kwa vile rais mpendwa wetu ni JK, CCM inamhitaji mtu kama JK, na kati ya waliopo, ambaye ni kama JK ni Membe, tena anamzidi JK kwa vile JK ni Mswahili, Membe sio mswahili. Kisifa, wanaendana, kitabia wanaendana, hata kimuonekano, wote ni ma HB, hivyo wanaendana, msiwe na wasiwasi kuhusu uwezo, Watanzania hatuchagui uwezo, tunachagua sura, kwa 2015, sura ya kupendeza ni Membe Pekee!.