Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Kwanza napenda kusema kuwa,wakati najihusisha na masuala ya mahusiano sijawahi kucheat,so sikuwahi kujua sababu ya kufanya hivyo,kiumri nina miaka 3....So that nimeona mengi mpaka mimeamua kuuliza hapa jamvini leo,nimeshashuhudia na watu wakilalamika wengine mpaka wamejiua wengine wapo gerezani wengine maisha yakipata dhroruba(mimi pia nipo kwenye kundi hili thats why sitaki ndoa wala mahusiano ya kimapenzi)wengine wana vilema n.k kwa sababu ya cheating!Hivi wakati unafanya hayo unakuwa unawaza nini?Je ni kisasi,au ni kutokuridhishwa kimapenzi,fedha au ni nini?Nauliza coz malalamiko ya jambo hili na athari zake ni kubwa katika jamii yetu,hebu mnaocheat au mliofanya jambo hili mtuambie sababu japokua mpaka leo sijaona sababu ya msingi ya kufanya jambo hilo,pia mtakua mmewasaidia wale walioko kwenye uhusiano au wanaotaka kuanzisha mahusiano!Maana kama unataka kuondoa tatizo tafuta chanzo cha tatizo!