What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

Wakazi wa kawe? Mbona swali linaeleweka?
Tuhabarisheni mazuri ya mh. Mdee jimboni kwake?

Huu siyo wakati wa ku-review nini wabunge wamefanya kwenye majimbo yao bali ni wakati wa kusimamia serikali ya sisiemu imefanya nini!!!Ok?
 
kati ya wabunge wote wa mkoa wa dar-es- salaam umemuona halima tu,kama una agenda yako binafsi na jimbo la kawe si useme tu,
 
Nothing apart from collecting a huge MP's payout! No water services at Bunju B (mradi 20,000), even a response or a follow up on the matter, she has forgotten why we chose her, a typical TZ MP, forgettenng their responsibilities, what a mess, I fear and shudder for the rest of the opposition IF they come into power, "changa la macho wakongwe"!

Tutolee mfano wa mbunge CCM wa Dar ambaye ni mfano wa kuigwa. Tuelezee vizuri amefanya nini kwa watu wake.
 
Tutolee mfano wa mbunge CCM wa Dar ambaye ni mfano wa kuigwa. Tuelezee vizuri amefanya nini kwa watu wake.

Mimi sijaribu ku-benchmark Performance ya Halima Mdee na wabunge wa CCM; kwanza naona hiyo ni sign mapema ya udhaifu... hauwezi kusema na kusimama jukwaani na kusema kwamba wabunge wa CCM hawafai halafu ukija kuulizwa umefanya nini unaanza kuuliza hao amabao hawafai wamefanya nini.... Wabunge wanaosema wako tofauti na wataleta mabadiliko makubwa lazima waweke Benchmark yao juu zaidi.... hata ukiwa shuleni hauwezi kupata "D" halafu ukasema lakini wenzangu wamepata "F"; sisi tunataka Changes za ukweli na tunataka watu wa "A"...... Nimeshasema mimi sina ushabiki wa ki-chama I am merely an innocent observer..... siko upande wa CCM na siko CDM niko upande wa Maendeleo... Kwa mchango wake bungeni juu ya Maslahi ya kitaifa kwa ujumla mimi sina tatizo na Mheshimiwa Mdee, lakini kwa wapiga kura wa Kawe walio mchagua bado naona hajawafanyia lolote la kumsifia....
 
Mimi sijaribu ku-benchmark Performance ya Halima Mdee na wabunge wa CCM; kwanza naona hiyo ni sign mapema ya udhaifu... hauwezi kusema na kusimama jukwaani na kusema kwamba wabunge wa CCM hawafai halafu ukija kuulizwa umefanya nini unaanza kuuliza hao amabao hawafai wamefanya nini.... Wabunge wanaosema wako tofauti na wataleta mabadiliko makubwa lazima waweke Benchmark yao juu zaidi.... hata ukiwa shuleni hauwezi kupata "D" halafu ukasema lakini wenzangu wamepata "F"; sisi tunataka Changes za ukweli natunataka watu wa "A"...... Nimeshasema mimi sina ushabiki wa ki-chama I am merely an innocent observer..... siko upande wa CCM na siko CDM niko upande wa Maendeleo... Kwa mchango wake bungeni juu ya Maslahi ya kitaifa kwa ujumla mimi sina tatizo na Mheshimiwa Mdee, lakini kwa wapiga kura wa Kawe walio mchagua bado naona hajawafanyia lolote la kumsifia....

Please soma makala hii ya Privatus Karugendo halafu naomba comments zako

SWALI langu la msingi katika makala hii ni je, sisi Watanzania tunafahamu kazi za wabunge? Na je, wabunge wetu wanafahamu kazi zao na wajibu wao? Tunapokaribia uchaguzi mkuu, tunafahamu umuhimu wa kazi hii ambayo ni ya gharama kubwa?

Taifa letu linatumia fedha nyingi kuendesha uchaguzi mkuu, je, tunafahamu umuhimu wake? Tunawachagua wabunge kwa sifa zao na uwezo wao au tunachagua wale wanaotununulia pombe na kutupatia sukari?
Tunachagua wabunge wetu kwa kuangalia uzuri wa sera za vyama vyao siasa au tunaangalia madaraka na nguvu za kifedha za vyama vyao?
Tunawachagua wabunge kwa kubaini kwamba wanayatabua na kuyashiriki matatizo yetu na mafanikio yetu au tunawachagua kwa shinikizo na pengine inawezekana hatuwachagui kabisa bali wanatangazwa washindi na mamlaka husika?
Katika pitapita zangu nimekutana na bango linalomnadi mbunge wa sehemu fulani hivi: Baadhi ya misaada mbalimbali niliyotoa kwa wanajimbo langu, Binafsi:
- Nilisaidia upatikanaji wa majeneza pamoja na kusafirisha marehemu kutoka wilaya yangu waliopata ajali ya treni huko Dodoma na kushughulikia majeruhi kwa kuwawahisha hospitali ili kupata matibabu ya haraka.

-Nilifanikisha uletwaji wa mwili wa marehemu Mathias Kasoso kutoka Dar-es Salaam; Nilisaidia sana uwezekano wa usafiri wa ndege pamoja na usafiri wa gari wa kutoka uwanja wa ndege kwenda alikozikwa.
-Nilitoa baiskeli kwa mlemavu wa .... yenye thamani ya Tsh 60,000 na 100,000/- kumnunulia mlemavu mwingine baiskeli ya gurudumu tatu.
-Nilimsaidia mama mtu mzima kupata haki zake Dodoma zilizokuwa hatarini kupotea bure.
-Nilimsaidia Salehe na rafiki yake (shs 40,000) nauli ya kutoka Dar es Salaam, waliokuwa wamekwama.
-Niliwasafirisha vijana wawili kutoka jimboni mwangu waliokwenda Dar es Salaam baada ya kudanganywa waende huko ambako wangepatiwa ajira.
-Nilitoa ada ya mtoto wa mzee wa Mahakama ya Mwanzo binti yake aliyekuwa akisoma sekondari ya kata.
- Tarehe 24/6/09: Nilihudhuria mazishi ya mzee Maddu aliyezikwa huko Mtakuja na kuchangia sh 100,000 kama rambirambi.
Ningepata nafasi ya kumkumbusha ndugu yetu huyu ni kwamba kati ya yote aliyoyataja hakuna hata moja linalohusiana na kazi yake ya ubunge. Labda alitaka kujitangaza kwamba yeye ni raia mwema. Hivyo anafaa kuchaguliwa kuwa mbunge. Hata hivyo bado ana kazi ya kujifunza na kuzifahamu kazi za mbunge!

Sasa hivi tunaingia kwenye kipindi cha uchaguzi. Waheshimiwa wabunge wameanza kupita kwenye majimbo yao. Wengine wanayachukulia majimbo haya kama mali yao kama ilivyo nyumba, ardhi, gari au familia. Jinsi mtu asivyotaka nyumba yake au ardhi yake isiguswe ndivyo waheshimiwa wabunge wasivyotaka majimbo yao yaguswe. Sasa ndipo wanaanza kuwakumbuka wapiga kura. Wale waliokuwa wakiishi Dar es Salaam na Dodoma, wanaanza kuyakumbuka majimbo yao.

Mbunge anaweza kuishauri serikali kujenga shule, lakini si kazi ya mbunge kujenga shule kwa pesa zake binafsi, akifanya hivyo, itakuwa si kwa vile ni mbunge, bali ni kwa vile atakuwa raia mwema mwenye uwezo na roho ya kuwasaidia wananchi wenzake.

Mbunge anaweza kutoa sukari kama vile wananchi wenye nia njema na uwezo wanavyofanya, lakini si kwamba ni kazi ya mbunge, kugawa sukari, kana kwamba asipotoa sukari au vitenge atakuwa hakufanya kazi yake ya ubunge. Hata hivyo si lazima kila raia mwema kuingia bungeni. Raia wema, ambao tunao wengi, wanaweza kuendelea na kazi yao ya kuihudumia jamii kwa matendo yao mema, na wanasiasa wenye uwezo wa kujieleza na kueleza kile walichotumwa na wananchi.

Wenye uwezo wa kuchambua na kuiweka sawa miswada mbali mbali inayowasilishwa bungeni, wasomi, wazalendo na wenye moyo wa kukubali kutumwa, wapewe nafasi ya kuwatumikia wananchi Bungeni.

Tunaweza kuzifahamu kazi za mbunge, kwa kuangalia kazi za Bunge, maana mbunge, ni mwakilishi wa jimbo (wananchi) katika Bunge: " Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi. Kuisimamia na kuishauri serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa katiba hii," Ibara ya 63(2), pia na Ibara ya 64(1) inaelezea kazi za Bunge, juu ya kutunga sheria.

Hivyo basi, Mbunge ni mwakilishi wa jimbo lake katika chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kina madaraka, kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake. Hivyo kutoa misaada, kusalimia misiba na kuwatembelea wagonjwa si kazi za mbunge. Huu ni wajibu wake yeye kama mwananchi katika jamii anamoishi. Hata asingekuwa mbunge, angetakiwa kufanya hivyo maana wananchi wote wanafanya hivyo, wawe madaktari, walimu, viongozi wa dini au viongozi wengine wa vyama na serikali. Inawezekana pia kwamba hata wananchi wanafikiri kwamba kazi za mbunge ni kujenga madaraja, ni kuleta maji, ni kuleta umeme, ni kusalimia misiba na kujenga shule.

Ndiyo maana wale wanaohimiza elimu ya uraia si wa kupuuzwa, ni lazima serikali isikie kiliko hiki na kuweka nguvu zote katika kufundisha elimu ya uraia. Ni jambo muhimu kabla ya uchaguzi wa mwaka huu wananchi wote pamoja na wale wanaotangaza nia ya kugombea wakatambua wajibu na kazi za mbunge. Hayo matendo ya ndugu yetu niliyoyataja hapo juu si ya kubuni au kutunga, hili ni bango liliotundikwa na kusambazwa kwa wananchi wa jimbo lake.

Bila shaka mbunge huyo, anaomba kurudi tena bungeni. Yote aliyoyataja hakuna linalohitaji mtu kuwa mbunge, ndipo alitende. Haya ni matendo ya kujituma katika jamii. Kusalimia misiba na kutoa rambirambi ni jukumu la kila mwananchi.
Kusafirisha watu, kulipa karo, kununua jeneza ni matendo ya kawaida katika jamii. Mtu kutaka kuyatumia katika kampeni ya kuingia bungeni, ni kielelezo kwamba mtu huyu anakuwa si makini vya kutosha.

Kama ni mtu anayetetea kiti chake, kama inavyoelekea kwa mbunge huyu, tungependa kusikia jinsi alivyoishauri serikali kujenga hospitali, kuwapatia watu maji, kujenga shule, kujenga barabara nk. Na si kwa jimbo lake peke yake, lakini kwa majimbo jirani na majimbo yaliyo na shida zaidi. Mtu anapojinadi, ni bora kutaja kazi za Bunge, Ni bora kutaja alivyowawakilisha wananchi katika chombo kikuu cha nchi, chombo chenye mamlaka ya kutunga na kuzifuta sheria.

Bango hili nililolitaja katika makala hili ni ushahidi wa kutosha kwamba watu wanaendelea kupumbazwa na wagombea ubunge. Wanapumbazwa kwa ahadi za kitoto.

Kuna haja ya kuwafundisha watu wakazijua kazi za Bunge. Wajue kwamba hawamchagui mbunge wa kutembelea misiba, kulipa karo na kusafirisha maiti. Wajue kwamba mbunge ni sauti yao ya kuwatetea na kufikisha malalamiko yao bungeni. Malalamiko ya maendeleo na ustawi wa jamii.

Wajue kwamba Mbunge, anaendelea kuwa mmoja wao katika jamii, hivyo anapofika kwenye msiba si tendo la huruma au msaada, na wala si tendo la kibunge! Bali anakuwa anatimiza wajibu wake kama mwanajamii. Mbunge anayeshindwa kuelezea mafanikio yake katika kuchangia maendeleo ya jimbo lake, si kwa misaada yake binafsi, maana si kazi yake kulisaidia jimbo lake binafsi, hafai kuchaguliwa kuingia bungeni.

 
Jamani mimi nauliza what has she done... not what she speaks in parliament.... if ubunge is all about speaking tuu... then we can all be there..... WHAt HAS SHE DONE FOR KAWE AND ItS PEOPLE??????????????

Imekuwa jambo la kawaida kwa wananchi kuwaomba viongozi wao, hasa wabunge wawasaidie kugharamia miradi ya maendeleo. Mazoea haya yametufanya tusahau majukumu halisi ya wawakilishi wetu na pengine jukumu letu la kuwawajibisha pale wanapokwenda kinyume na wajibu wao.

Wabunge wamesahau majukumu yao ya msingi (legislative), badala yake wanajitwika majukumu ya serikali (excecutive). Hali hii pia inasababisha wananchi tusahau vigezo muhimu vya kuchagua viongozi na kutumbukia kwenye mkumbo wa kuchagua viongozi matajiri-ambao nao wanaitumia fursa hiyo vilivyo kuimarisha utajiri wao pamoja na kuulinda.

Ieleweke kuwa sio wajibu wa wabunge kulipia/kugharamia miradi ya maendeleo majimboni mwao. Wabunge wengi wamekuwa wakitoa ufadhili mbalimbali katika majimbo yao, na kusahau majukumu yao ya msingi ya kuwawakilisha wananchi na kuwasilisha mawazo yao Bungeni ili yapatiwe ufumbuzi na kuisimamia, kuishauri na kuikosoa serikali katika kutoa huduma za jamii na kufanya miradi ya maendeleo.

Aidha, mfuko wa jimbo ambao, wabunge wa upinzania na chama tawala, CCM walisahau tofauti zao na kuupitisha kwa kishindo umekuwa nao ukitumika kama mali ya mbunge na katika kutafuta wema kwa wapigakura, wamekuwa wakiahidi mambo kadhaa huku wakiacha kuwaweka wazi wapigakura. Mwishowe wananchi wanaamini hizo ni huruma za mbunge wao.

Hali hii hakika umetupeleka pabaya kwani umesababisha na unaendelea kusababisha yafuatayo:

Mosi, hali ya wabunge kulipia miradi ya maendeleo kunavuruga utaratibu wa mchakato mzima wa mipango ya maendeleo. Tunazo sera nzuri za kusaidia jamii kuibua miradi ya maendeleo na fursa za hiyo miradi kuweza kugharamiwa. Hivyo wabunge wanapochukua jukumu la kugharamia miradi hiyo, kunafanya wananchi wanakosa imani/hawaoni umuhimu wa kufuata mchakato uliwekwa kwa ajili ya kuwaletea maendeleo na badala yake wanatupia jukumu hilo kwa wabunge.

Pili, hali hii inapunguza uwajibikaji wa pande zote mbili hasa uwajibikaji wa wananchi. Mradi unaogharamiwa na wabunge, unakuwa mradi wa mbunge. Hivyo wananchi wanakosa umiliki wa miradi hii kitu ambacho kinafanya miradi hii isiwe endelevu, na zaidi isiwanufaishe wananchi kwa upana wake.

Wakati mbunge kwa upande wake anashindwa kutumia nafasi yake ya uwakilishi kwa kujenga hoja kwa lengo la kupata fedha kwa ajili ya kugharamia miradi ya wananchi. Hatima yake ni kwamba serikali haioni umuhimu wa kutenga fedha kwa ajili ya miradi ya wananchi kwani mbunge anazo hela na hataki ibainike kwamba serikali/wananchi wanaweza kuendeleza miradi yao wenyewe.

Pia, mwenendo huu wa wabunge husababisha migongano kwenye Serikali za Mitaa; hii hutokea pale panapokuwepo fedha ambazo tayari zimeshatengwa kwa ajili ya miradi husika, ambapo fedha hizo zinaweza kuishia mikononi mwa wajanja. Wajibu wa mbunge katika hili ni kuwahamasisha wananchi kushiriki katika utekelezaji wa miradi hii na kusimamia matumizi ya fedha ya miradi hii.

Tatu, wabunge kugharamia miradi ya maendeleo inachochea hali ya utegemezi ndani ya jamii zetu. Serikali kupitia sera ya ugatuzi wa madaraka inalenga kuijengea jamii utamaduni wa kujitegemea kwa kuitaka jamii ishiriki moja kwa moja katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kuchangia gharama. Sasa mbunge anapofadhili hii miradi, inafanya wananchi wajijengee utamaduni wa kusubiri kufanyiwa kila kitu. Na ndiyo hali ilivyo sasa kwani mara nyingi wenye fedha ni rahisi kupata madaraka.

Nne, wananchi wanajikuta wanapima viongozi wao kwa ufadhili waliotoa badala ya kutathmini utekelezaji wa majukumu yao kama wabunge. Hii inasababisha watu wasiokuwa na uwezo wa kifedha kukosa nafasi za uongozi hata kama wanao uwezo wa kuongoza vizuri. Hali imesababisha wananchi wengi kukosa uwakilishi na kuongezeka kwa matatizo makubwa ya uongozi mbovu, ufisadi, rusha na hali ngumu ya maisha huku wachache wakiendelea kunufaika na rasilimali za nchi hii.

Tano, wabunge wanaelemea katika kutafuta fedha za kugharamia miradi ya maendeleo badala ya kufanya majukumu yao ya msingi. Hii imesababisha wabunge kutoonekana majimboni kwa sababu inawabidi watafute mbinu mbalimbali za kupata fedha badala ya kutumia muda wao kutimiza majukumu yao ya msingi.

Badala ya kuwapigania wananchi ili kuwakwamua kutoka hali waliyonayo, wabunge wamejikuta wakipigania maslahi yao binafsi mfano wa sasa wa wanavyopambana kufa na kupona kuhalalisha kupanda kwa posho kwa madai ya kuwa wanatoa hela nyingi kwa wapiga kura kufadhili shughuli mbalimbali za maendeleo. Amenena mtu mmoja kuwa wanatumia fedha za walipa kodi kuwahonga wapiga kura.

Richard Lucas
 
Sitaki mhesmiwa atumia fedha zake kugharamia maendeleo kwenye Jimbo lake... Mchango wake uwe wa uwezo wake, ushawishi wake na ubunifu wake, usimamiaji wake wa kutatua matatizo Jimboni kwake, ndio hili nina shaka nalo.... kama kweli alikua anawasimamia kidedea hawo waliopewa kazi kutekeleza kupata ufumbuzi wa matatizo Kawe, mbona tunashindwa leo kutaja hata fanikio mmoja; Ameshauri nini na kusimamia nini jimboni kwake kwa matatizo Kawe na kufanikiwa kufikisha utekelezaji hadi mwisho au kuleta ubunifu mbadala au kuwashawishi wananchi au taasisi ambazo sio za kiserekali wa jiunge kutatua kero sugu za Kawe....

tunataka viongozi wanao-Stand out kwenye jimbo...... who go the extra mile kwa ajili ya majimbo yao..... hakuna evidence kwa kuangalia mafanikio jimboni kwake kwamba amefanya chochote cha ziada....
 
Sitaki mhesmiwa atumia fedha zake kugharamia maendeleo kwenye Jimbo lake... Mchango wake uwe wa uwezo wake, ushawishi wake na ubunifu wake, usimamiaji wake wa kutatua matatizo Jimboni kwake, ndio hili nina shaka nalo.... kama kweli alikua anawasimamia kidedea hawo waliopewa kazi kutekeleza kupata ufumbuzi wa matatizo Kawe, mbona tunashindwa leo kutaja hata fanikio mmoja; Ameshauri nini na kusimamia nini jimboni kwake kwa matatizo Kawe na kufanikiwa kufikisha utekelezaji hadi mwisho au kuleta ubunifu mbadala au kuwashawishi wananchi au taasisi ambazo sio za kiserekali wa jiunge kutatua kero sugu za Kawe....

tunataka viongozi wanao-Stand out kwenye jimbo...... who go the extra mile kwa ajili ya majimbo yao..... hakuna evidence kwa kuangalia mafanikio jimboni kwake kwamba amefanya chochote cha ziada....

Nimekuwekea michango yake bungeni. Ndilo jukumu lake kuifuatilia serikali. Kama vitu havijatekelezwa inathibitisha jinsi serikali isivyo makini.

Toa mfano wa hao viongozi wanao stand out kwenye jimbo na wamefanya nini. Mahanga? Mtemvu? Zungu?

Wewe ulitaka afanye nini? Toa practical suggestions.
 
Nimekuwekea michango yake bungeni. Ndilo jukumu lake kuifuatilia serikali. Kama vitu havijatekelezwa inathibitisha jinsi serikali isivyo makini.

Toa mfano wa hao viongozi wanao stand out kwenye jimbo na wamefanya nini. Mahanga? Mtemvu? Zungu?

Wewe ulitaka afanye nini? Toa practical suggestions.

Nishasema sina tatizo na Michango yake bungeni kiujumla... lakini jimboni kwake ndio nina mashaka.... vitu visipo fanyika vile vile inaweza kuwa juu ya ufwatiliaji dhaifu wa mbunge akishatoka jengoni.... labda yuko pre-occupied na Chama kuchukua nchi hadi amewasahau waliompigia kura.... Au labda hana uwezo wakufuatilia hoja za jimbo lake; au sifa ya kuhakikisha jimbo lake linapewa kipaumbele kwenye maendeleo.... au labda ni inexperience yake...

Kwangu binafsi Mbunge anaepiga gumzo jengoni licha ya umuhimu wake halafu anashindwa kusimamia maendeleo jimboni kwake ni worth nothing to me.... Wengine ninaona wanafanya vizuri kwenye usimamizi ambao angalau nacho kimoja au viwili kuwasemea ni kama Ndesamburo, Nassari, Mkono, January, nk... lakini sio Mdee...

Practical suggestions: I don't have one for her If i did i would have ran for her seat.... but since she stood up infront of hundred of thousands of voters and asked for their votes which she was given then she need to take ownership of what she will do or change for Kawe... Advice would be to look at the likes of those mentioned above and see what she can emulate to their approaches...
 
Non-emotional and Politically unbiased answers only please......

I know that curiosity killed the cat, but just curious to know the intent of your question

Do you really believe that all Kaweians are members of JF and can use this forum to list down (for your satisfaction) what Mdee has done for them? Why would you single out just the Kawe constituent out of more than three hundred constituents in the country? Are sure that all other constituents under their current parliamentarians are faring better than Kawe?

I am inclined to the belief that you probably just hate Mdee, and you can use any opportunity whatsoever to throw your punches against her.


Jamani mimi nauliza what has she done... not what she speaks in parliament.... if ubunge is all about speaking tuu... then we can all be there..... WHAt HAS SHE DONE FOR KAWE AND ItS PEOPLE??????????????

Inategemea wewe (kama kweli ulipigia kura yako) ulikuwa unataka yeye afanye nini bungeni, kwa sababu kazi ya mbunge ni kutunga sheria ndani ya bunge, siyo kulala wala kuzomea; na anaweza kufanya hivyo kwa kusimamama na kuchangia kwenye mijadala ya bunge ili maamuzi yawe kama anavyotaka kuwawakiliahs wanachi wake. Sasa kama wewe ulimchagua kusudi ndiye awe waziri wa ujenzi akakujengee barabara huko Kawe, (kama ambavyo watu wengi wanvyoamini) basi nawe ni mpotevu. Soma Katiba tena kwa makini sana ujue kazi ya mbunge.

Utekelzaji wa miradi yoyote ni jukumu la serikali, inategema kura yako ya uraisi ulimpa nani.
 
Kafatalia kwa umakini maeneo ya wazi yaliyopolwa, watu walio nyanganywa mashamba yao na mafisadi. Mfano kunduchi, wazo na madale
 
....[/QUOTE]

Nilichoona kwenye thread hii ni kwamba watetezi wa Mdee wanaukimbia ukweli na hii ni dalili kuwa hakuna kitu anachoweza kujivunia kinachofahamika kwa wachangiaji hao.

Mimi ni mdau wa jimbo la Kawe. Sijaona manufaa ya Mdee ya moja kwa moja katika maisha yangu ya kila siku, lakini ningefarijika kuona kuwa kuna sehemu nyingine waliobenefit.

Kumbe anachofanya Mdee ni kuongea tu Bungeni! Well ngoja niwakumbushe tu kuwa hakuna muda ambao Bunge linakuwa silent, ukifungua Bunge kila wakati kuna mbunge anaongea, hii ni kumaanisha kuwa kama kutekeleza majukumu ya mbunge ni kuongea tu basi kwa ujumla wao wabunge wametekeleza majukumu yao kwa asilimia 100 or in other words Bunge limetekeleza majukumu yake kwa asilimia 100.

Sasa tunapokuja kwenye individual case ni lazima twende beyond kuongea. Na hapa tunatakiwa tuanze na utekelezaji ahadi alizotoa. Ukimuahidi mtoto wa rafiki yako kuwa utampa ada ya shule, inapofika wakati wa kulipa ada huwezi kumwambia kuwa jukumu hilo si lako ni la wazazi wake! you didnt know that when you promised?

Labda tuangalie mfano wa January na Shirika la Maendeleo ya Bumbuli, you can see the guy is trying to do something to involve the people of Bumbuli in development of their own as a community. Vitu vya namna hii ndivyo tunavyotaka kusikia toka kwa wabunge mbalimbali wa CCM na upinzani.

Labda nitoe mfano katï ya African Union na European Union. African Union kila siku inakaa vikao vya organs zake mbalimbali, European Union pia.

Lakini kwa upande wa Europe mwananchi wa kawaida atapata ajira kwa ajili ya project fulani za EU za kuongeza ajira, atapata scholarship kupitia EU, mji wao utaboreshwa kwa project za EU, yaani mwananchi wa Ulaya anaiona EU katika maisha yake ya kila siku.

Personally sijaona African Union katika maisha yangu ya kila siku wala ya majirani zangu. That doesnt mean kwamba AU haifanyi vikao au haijadili shughuli za maendeleo, lakini kujadili alone is not enough. The same applies to wabunge, je wananchi wanaona uwepo wa mbunge katika maisha yao ya kila siku?
 
Amesadia watu wa Chasimba na madale wasidhulumiwe haki zao
Amepigia kelele uozo wa Manispaa na kufanikiwa kurekebisha baadhi ya mambo
 
Hii iliwekwa hapa juzi, July..... labda tuanzie hapa...

Kwa masikitiko makubwa Mh. Halima Mdee ukiwa mbunge wa jimbo la kawe ulitokea kuwa tumaini jipya kwa wakazi wa jimbo hilo. Kwani mtangulizi wako Ritha Mlaki alishindwa kutekeleza hata kiduchu kile kinachowakera wakazi wa jimbo la kawe na hasa maeneo ya makongo juu. Eneo hilo lina kero ya muda mrefu iliyosababisha makongo kama sio sehemu ya wilaya ya Kinondoni mkoa wa Dar es Salaam. Hapa nitataja kero kuu mbili ambazo hadi niandikapo bandiko hilo nashindwa kuelewa tatizo liko wapi waheshimiwa nyie kushindwa kupata utatuzi.

1. Barabara. Ukianzia njia panda ya Chuo cha Ardhi hadi makongo mwisho na baadae kuendelea goba kutokea mbezi samaki hii barabara ni mbaya mbaya haina jinsi ya kuelezea. Imefikia mahali wakazi wa makongo juu wamechukulia kuwa sehemu ya maisha yao kila ifikapo saa 12 jioni na kuendelea kupanda dala dala kwa bei ya kuanzia sh. 500 kwa umbali usiozidi kilomita 5. Kinachoumiza hata huo usafiri wenyewe nao licha ya kuwa nauli yake iko juu bado haupatikani angaalau fadhila za madereva wa mabasi kutoka mwenge kwenda bagamoyo ndio zinasaidia vinginevyo sijui hali ingekuwaje..

2. Wakazi wa makongo juu tulishasahau hadithi ya kupata maji ya bomba. Mwaka 2009 kulifanyika uwekaji wa mtandao wa mabomba ya maji karibu eneo lote la makongo juu. Mabomba haya maarufu kama mabomba ya "mchina" tangu yalipowekwa na hiyo kampuni ya kichina mwaka huo hadi leo hayajawahi kutoa maji hata yale ya majaribio...Halima Mdee ulikuwa kuomba kura zetu kwa mbwembwe nyingi kuwa kilichomshinda Mlaki wewe utakimaliza..Lakini wakati tukiingia mwaka wa 2 tangu kufanyika uchaguzi mkuu 2010 hakuna hata dalili kuwa kuna kitakachofanyika....Mh..Halima Mdee kila nikikuangalia kupitia runinga ukiwa mle mjengoni napata hasira kuwa nilipoteza muda na kura yangu na sasa imani yangu inapotea kwako. Sina jinsi ya kuelezea hasira zangu kwako.

Mtu anaweza kusema kuwa tukikutegemea wewe peke yako utatue kero zetu ni uvivu wa kufikiri lakini hata sisi wananchi tulikuwa tayari kuchangia nguvu zetu kutatua tatizo la barabara...lakini wapi...wapi...bure tu...Nafikiria kusimama na wewe kwenye uchaguzi 2015 kupambana na wewe. Umekuwa mzuri wa kupiga kelele huko mjengoni lakini unasahau kuwa sisi tulikupa kura zetu ili utuongoze kutatua kero zetu na si vinginevyo..Naomba pindi utakaposoma thread hii jiulize moyoni mwako hivi unawatendea haki wapiga kura wa makongo????

 
Back
Top Bottom