What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

Uckae kuuliza kafanya, tuko ktk harakati za kutawala nchi, tutaichukua nchi hii 2015 bila hiyo kura yako 1 , ipeleke tu kwa mafisadi wenzako, ila 2015 tunawazika, alafu tutajua amefanya nini 2020, hii ndo M4C.
 
Non-emotional and Politically unbiased answers only please......

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2012/2013 – Ofisi ya Waziri Mkuu na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa 27/06/2012

Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru. Kwanza nikiwa kama Mbunge, napenda kuchukua nafasi hii kulaani yale yaliyomtokea Daktari Ambokile. Sitaki kujiaminisha kwamba ile statement kali iliyotolewa leo asubuhi ina mahusiano ya moja kwa moja na kilichotokea, lakini ninaamini Serikali itahakikisha wale wote waliohusika na huo unyama wanapatikana. Ikishindikana itatufanya kile kiwe kielelezo kwamba sauti ya haki inazimwa na bahati nzuri Mungu kamsaidia...

Mheshimiwa Naibu Spika, najua unaelewa, ndiyo maana umenisimamisha. Ninaelezea kipigo alichokipata Kiongozi wa Chama cha Madaktari.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikiwa kama Mbunge wa Dar es Salaam, ninasikitishwa na kauli iliyotolewa na Waziri Mkuu wakati wa hotuba ya Wizara ya Ardhi akitambua migogoro ya ardhi iliyokuwepo Mkoa wa Dar es Salaam akaahidi atakutana na Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam kuweza kutatua changamoto mbalimbali, akashindwa kufanya hivyo. Hii ni dharau kwa Wabunge, na Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, niungane na Dkt. Ndungulile kwamba kwa hii bajeti, Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam hatuiungi mkono. Lakini zaidi, wananchi wangu wa Mabwepande, mtakumbuka mwaka jana mwishoni yalitokea mafuriko Mkoa wa Dar es Salaam. Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya na kupitia Mkuu wa Mkoa, wakaenda kwa wananchi wa Mabwepande kuwaambia waachie maeneo yao wakiwaambia watalipwa fidia wawahifadhi Watanzania wenzao. Mbaya zaidi, viongozi wa Mkoa na viongozi wa Wilaya wakamleta Rais wa Jamhuri ya Muungano Mabwepande wakitoa ahadi lukuki za kuwalipa fidia za kuwagawia wananchi wa Mabwepande ardhi, lakini tunavyozungumza, mpaka sasa hakuna fidia iliyolipwa, hakuna viwanja walivyopewa wananchi wa Mabwepande, licha ya kwamba ardhi yao ndiyo imechukuliwa na Serikali kuwapa watu walioathirika na mafuriko.


Mheshimiwa Naibu Spika, kuna tuhuma nzito kutoka kwa wananchi wa Mabwepande wakimlalamikia Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa kwa uchakachuzi wa viwanja husika. Suala hili tumelizungumza katika vikao mbalimbali na mbaya zaidi, sio Mwenyekiti wa Mtaa, sio Diwani, sio Wabunge walioshirikishwa katika mchakato wa mgawo wa viwanja. Mgawo ulitawaliwa na usiri mkubwa na hivi tunavyozungumza wananchi wamesema Serikali isipojibu, watarudi kwenye maeneo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, namuomba Waziri Mkuu ambaye kitengo cha maafa kipo chini ya ofisi yake, ahakikishe wananchi wangu wa Mabwepande wanapata haki yao, kinyume na hivyo hatuwezi kuruhusu. Tutaagiza wananchi warudi kwenye maeneo kama ilivyo kwenye mradi wa Kigamboni. Hatuwezi kuruhusu miradi ambayo inaendeshwa shagalabagala ambayo inaathiri wananchi wetu wa Mkoa wa Dar es Salaam ipite hivi hivi. Wananchi wa Kigamboni wajue Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam tuko nao.

Hatuwezi kupindisha sheria, kupokea maeneo ya watu pasipo kufuata taratibu na sheria za nchi kwa sababu tuna dola. Hili ni ujumbe kwa Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, nizungumzie kilimo.
Yamezungumzwa mengi sana kuhusiana na migogoro ya ardhi. Mwaka jana wakati ninachangia bajeti ya Wizara ya Ardhi, nilisema, ni kwa namna gani Serikali kupitia viongozi wakubwa wamekuwa ndiyo madalali wa ardhi kwa wawekezaji kwenye nchi yetu, matokeo yake ni kwamba wananchi wanyonge wananyang'anywa ardhi kwa nguvu za Serikali.

Nikatoa mfano mmoja wa AgriSol Rukwa kwa Waziri Mkuu na Waziri Mkuu akanijibu kwa maelezo kwamba waliingia makubaliano ya awali, nikamwambia Waziri Mkuu ama wamekudanganya ama na wewe hauko makini. Akaniambia kuna Memorundum of Understanding ambayo wameingia baina yao na yule mwekezaji, akasema yale yalikuwa ni makubaliano ya mwanzo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimepitia hii Memorundum of Understanding kuonesha kwa namna gani sasa hivi Serikali ndiyo inasaidia mabeberu kuja kuchukua ardhi yetu, kipengele cha tatu kinaonesha kwamba wanasema wakati huyu Mwekezaji anaendelea na feasibility study wakaingia makubaliano Halmashauri pamoja na yule Mwekezaji, wakatengeneza mkataba. Sheria za nchi ziko wazi na nilisema kipindi kile kwamba Sheria ya Ardhi kifungu cha 19 na 20 na Sheria ya Uwekezaji ya mwaka 1997 inakataza Halmashauri ama mtu yeyote kutoa eneo la uwekezaji. Mamlaka pekee ya kutoa maeneo kwa wawekezaji iko kwa TIC. Lakini hapa kwa makubaliano na ambayo Waziri Mkuu anakiri alishiriki wameonesha hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mbaya zaidi kipengele kingine kinaonesha kwamba hawa jamaa watakuwa wanalipa Sh. 200/= kwa kila heka, na hii ni MOU ambayo Waziri Mkuu namba tatu wa nchi ameingia. Wengine wafanye nini? Anakuja hapa anadanganya Bunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia wanalalamika Rufiji kwamba wawekezaji wanakuja wanapitia migongo ya nyuma wanachukua ardhi. Ni muhimu mkaelewa kwamba kitu ambacho kitakuja kuleta vita nchi hii ni ardhi. Mmeonea migodi kule, yalikuwa ni maeneo ya watu wachache, mnapokuja kupoka ardhi ya Watanzania na kuwapa wageni, mtapata aibu!

Mheshimiwa Naibu Spika, tulisema mkabisha, wale ambao walikuwa Ohio State University Chuo cha Kilimo Marekani ambacho kilikuwa kije kisaidie kuwafundisha wakulima, baada ya kuona kwamba yule mtu wa AgriSol hana nia njema kimejitoa! Ni aibu kuona kwamba eti Serikali inafurahia trilioni 1.4 ya msaada kutoka G8, wakati nyuma ya mgongo wa G8 ukiangalia SAGCOT, kitabu cha SAGCOT nimekipitia, wadau wote ni wa kampuni binafsi ya Kimarekani, ya kibeberu, inatoa msaada mbele, inakuja nyuma, mnawapa maeneo. Vijana tumechoka! Inawezekana
wazee hamna miaka mingi ya kuishi. Sisi tumeshasema msije mkatuachia makapi, msije mkamaliza nchi mkatuachia makapi!

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba dakika zangu.


Hiyo moja. Lakini pili, nilichokisema sasa naomba nirudie. Nimesema ninalaani kipigo alichokipata Bwana Ulimboka kwa
kutekwa nyara usiku na watu ambao inasemekana ni Maafisa wa Polisi. Inasemekana! Nikasema sitaki kujiaminisha wala sitaki kuamini kwamba ile kauli nzito iliyotolewa na Waziri Mkuu leo asubuhi...

Mheshimiwa Naibu Spika, ujumbe umefika, lakini niendelee. Kwa kumalizia namwomba Waziri Mkuu, ofisi yake imepewa jukumu

kubwa sana la kusimamia uwekezaji, na ni aibu juzi Waheshimiwa Wabunge wanashabikia boda boda kuondolewa kodi. Wakati wote tunajua kwamba boda boda ndiyo zinawapa ulemavu, ukienda hospitali leo vijana wamelazwa kwa pikipiki ambazo siyo mali yao.

Kwa hiyo, kama kweli tunajali vijana, badala ya kutumia mabilioni ya fedha kuwaandalia miundombinu mabepari katika kilimo, tutumie mabilioni ya fedha kuandaa miundombinu ya kilimo, kuwekeza kwenye kilimo, tuwapeleke vijana wakalime kama watakataa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa pia Waziri Mkuu anijibu baada ya Chuo cha IOWA kujitoa, ambacho katika yale mapambio waliyokuwa wakiimba katika lile Bunge lililopita kwamba watatoa elimu ya kilimo kwa wakulima wadogo wadogo, mustakabali wa Agrisol ukoje? Nanasema hili kwa sababu moja, huko Rukwa ambako Waziri Mkuu anasema anatoka na kupigania katika asilimia 100, ile ardhi ni asilimia 17 tu ya ardhi ambayo inafaa kutumika katika mazingira ya kilimo na ufugaji. Nyingine ni games reserve, nyingine forest reserve, nyingine ni maji. Sasa nilitaka akiwa anajipambanua katika haya, aeleze athari ya kujitoa katika hiki Chuo cha IOWA ambacho ndio mlikuwa mnajinasabua nacho, lakini vile vile muelezee migogoro ya wakulima na wafanyakazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, siungi mkono hoja hii. Ahsante sana.
 
Jee Kawe- specifically amefanya nini ili angalau wanachi wamchague tena 2015 pale Kawe...

Wana kawe ndio watajibu swali hili na nadhani mtoa mada ulitakiwa uwaulize wana kawe sisi wengine tuko kusini huku ya kawe wayajibu wao na kama na wewe ni mwana kawe tueleze unalojua ili wana kawe wakupandie kichwani....
Hata hivyo kwani unamlinganisha na mbunge wa jimbo gani?
 
Labda tuanze kuuliza kama una list ya ahadi alizotoa na kumbukumbu ya kero kuu za wananchi wa jimbo hilo katika kila kata.
Maana kujibu mtu alichofanya bila kujua alichotegemewa kufanya inakuwa mtego fulani...

Sina listi.... nataka tuu kujua mafanikio yake ili angalau wananchi wa mkumbuke 2015; kumbuka ni hao hao itabidi awarudie.... mimi binafsi sijui amefanikiwa nini ndio maana nauliza kwa sababu sijaona badiliko hata mmoja Kawe... ndio maana nauliza kwa wale wanaojua wanihabarishe lakini naona inakua ngumu hata kwao...
 
mwanaukweli ahsante najua kulizuka kabeef kidogo na Mh waziri Tibs, lakini mbona kaongelea mabwepande tu, kwa nini asilazimishe task force ya wizara kuangalia migogoro mingine ya ardhi kawe? nway ahsante

Rejea post yangu za juu hasa namba 25 ameongelea kwa ufasaha migogoro mingi ya ardhi.


Tena amewasaidia na wabunge wengine wa Dar (wakiwemo wa CCM)
 
Sina listi.... nataka tuu kujua mafanikio yake ili angalau wananchi wa mkumbuke 2015; kumbuka ni hao hao itabidi awarudie.... mimi binafsi sijui amefanikiwa nini ndio maana nauliza kwa sababu sijaona badiliko hata mmoja Kawe... ndio maana nauliza kwa wale wanaojua wanihabarishe lakini naona inakua ngumu hata kwao...

Nakumbuka Mdee alishawahi kuja kutoa list hiyo, nikiipata nitaiweka hapa. Alijibu vizuri. Hata hivyo majimbo ya Dar es Salaam kuyaridhisha siyo rahisi. Ukitengeneza barabara salasala mtu wa msasani hawezi hata kujua, wakati vijijini ukifanya kitu kata moja tu jimbo zima linajua.
 
Nakumbuka Mdee alishawahi kuja kutoa list hiyo, nikiipata nitaiweka hapa. Alijibu vizuri. Hata hivyo majimbo ya Dar es Salaam kuyaridhisha siyo rahisi. Ukitengeneza barabara salasala mtu wa msasani hawezi hata kujua, wakati vijijini ukifanya kitu kata moja tu jimbo zima linajua.

ningeshukuru sana maana naona kufanya hii discussion objectively imekua ngumu...
 
Jamani mbona mmemsahau MWIGULU WANAWAKE NCHEMBA Hammsemi? amefanya nini kule Singida?
 
Kwanini? swali hilo hukumuuliza kwa mbunge aliyepigwa chini! umetumwa wewe! eti wa ukelewe! ugolo!
 
Kwani halima mdee ndio anakusanya kodi? Yeye kazi yake ni kufuatilia matumizi ya kodi yetu

Wanaosema siyo kazi ya mbunge kuleta maendeleo inabid waelewe kuwa kazi za mbunge zilizoelezwa kwenye katiba siyo mpaka wa majukumu yake. Kwa kiasi kikubwa majukumu ya mbunge huwa ni kutekeleza ahadi ambazo ziliwafanya watu wampe kura na vilevile kuzishughulikia kero kuu za wakazi wa jimbo.
Kama aliahidi atajenga daraja, hawezi kusema hiyo siyo kazi yake maana atakuwa anawatukana watu waliomuamini kuwa atajenga.
 
Sina listi.... nataka tuu kujua mafanikio yake ili angalau wananchi wa mkumbuke 2015; kumbuka ni hao hao itabidi awarudie.... mimi binafsi sijui amefanikiwa nini ndio maana nauliza kwa sababu sijaona badiliko hata mmoja Kawe... ndio maana nauliza kwa wale wanaojua wanihabarishe lakini naona inakua ngumu hata kwao...

Mkuu kwa leo soma hii hapa chini kama kweli hujui amefanikiwa nini.

Amewasemea wananchi wake na kuwatetea kwa ufasaha. Kama serikali haijatekeleza, yeye kama mbunge amefanya kazi yake

Zingatia italics na rangi nyekundu.



Mchango kwenye Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Tarehe 16/08/2011

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nukushukuru kwa dhati kwa kunipa fursa hii. Lakini vile vile siungi mkono hoja si kwa sababu sina imani na Waziri wala Naibu Waziri, hapana. Ni kwa sababu licha ya wao kuwa na nia njema ya kufanya kazi mbali ya kuwa na fedha finyu. Lakini nadhani hapati ushirikiano wa kutosha kutoka Serikalini kwa ujumla.


Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mzungumzaji mmoja nadhani ni mama Kikwembe if I am not mistaken wakati nimetoka akapiga mawe kidogo. Lakini nimhakikishie kwamba siwezi kuzungumza kitu ambacho sina ushahidi nacho. Aliniambia nimtajie majina ya Madiwani waliokwenda Marekani siku nne. Nitamtajia Kata, majina itakuwa kazi yake yeye kutafuta. Kuna Diwani wa Kata ya Magamba, kuna Diwani wa Kata ya Sitalike, kuna Diwani Viti Maalum Karema na kuna Diwani Viti Maalum Uruwira. Sasa majina akayatafute yeye.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini inasikitisha. Unapoona Mbunge mnajaribu kutetea eneo lake yeye, anakuja ana-crash down pasipo hoja za msingi na kwa sababu ya uvivu wa kusoma. Juzi kwenye SADC Forum iliyokwisha tu majuzi. Moja ya ajenda ilikuwa ni Land Crabbing Africa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wazungu huko walishamaliza kwao, wanakuja kurudisha ukoloni. Kibaya zaidi mtaalam wa Canada, mzungu huyo huyo akaenda na mikataba mizito hivi na mkataba uliotolewa mfano, kama West Case Scenario ni mkataba wa Agrisoil Tanzania. Nasikitika jana namsikia Mbunge mmoja kutoka Kigoma, anasema eti wenzake wa Kigoma wameshindwa kutumia ardhi, wakati kuna hekta 80,000 wameshindwa kutumia ardhi, kwa hiyo walete wawekezaji. Tena msomi mzuri, inasikitisha. Kwa hiyo, niseme hili la suala la Agrisoil mbali na
upungufu wake wote na upuuzi wake wote umekiuka Sheria ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria zetu ziko wazi kabisa na hii namwambia Mheshimiwa Waziri Mkuu asipoli-handle vizuri anaweza akaanguka nalo. Ataanguka nalo kabisa. Kwa sababu kuna ushahidi wa moja kwa moja unaoonyesha kwamba Ofisi yake ilihusika. Kwa hiyo tutumie busara tuokoe nchi. Sheria ya Ardhi iko wazi. Muwasaidie Mawaziri, mumsaidie Naibu Waziri. Sheria ya Ardhi iko wazi kabisa. Mgeni ama mwekezaji anapotaka kuja kumiliki ardhi ya nchi imeeleza wazi, kifungu cha 19, Kifungu cha 20(i) hadi 20(iv) mabadiliko ya 2004. Very clear na imesema wazi kabisa kama kuna joint venture inamhusu raia na Sheria ya Uraia haijatambua kampuni, haijatambua Halmashauri, haijatambua kitu kingine chochote raia mmoja mmoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mtuambie huko Rukwa ni raia gani anamiliki hekta laki mbili na kitu. Huko Lugufu Kigoma kuna raia gani anamiliki hekta 80,000 ambaye anaingia ubia sasa ili ule mchakato wa kufuata TAC usifuatwe. Naomba tuache ushabiki. Hii ni crisis?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza taarifa yake siitaki. Lakini pili, mimi mwenyewe hivi kiwanja changu sina Hati Miliki. Hati Miliki siyo issue.


Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tatu, kuna kitabu cha makubaliano waliyoingia baina ya Halmashauri na Agrisoil na mkitaka nitaleta kwenye Meza yako. Wao wenyewe hapa wamekiri, kuna hivyo vitu vinavyoendelea Bungeni. Kwa hiyo, kama nyinyi ambao ndiyo mnatakiwa mtekeleze Sheria mnakuja hapa mnatetea wahalifu, tunakoelekea kama nchi kunatisha. Hatutafuti umaarufu wa kisiasa, umaarufu upo tayari, tunataka kujenga nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nirudi Jimboni maana nilisimama kwa ajili ya Jimbo. Lakini alinivurugua system Mama Kikwembe ikabidi nirudi kule ambacho sikutaka kurudi.

Suala la kwanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunilinda. Katika Jimbo langu na nadhani katika Majimbo ya Dar es Salaam ndiyo yanaongoza katika migogoro ya ardhi. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri na Mheshimiwa Waziri suala la Mabwepande. Miaka minne iliyopita mlikwenda pale, mkawaambia wananchi wasiendeleze maeneo yao. Mkawalipa wengine kama 160. Mheshimiwa Naibu Spika, namwonea huruma sana kwa sababu 2015 sijui kama atarudi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Mabwepande. Naomba na muda wangu huu pia uzingatiwe. Miaka minne iliyopita Serikali ilikwenda kufanya tathmini na ninavyozungumza hivi pia na katika mfumo huo huo nazungumzia eneo la Kwembe kwenye Jimbo la Mheshimiwa Mnyika. Nilikwenda kufanya tathmini, wananchi wakaambiwa wasiendeleze maeneo yao na kwamba Serikali ina mipango ya kuja kulichukua lile eneo kwa ajili ya matumizi mapya. Jimbo la Ubungo lilikuwa ni kwa ajili ya kujenga Chuo cha Muhimbili kwa mantiki ya Campus nyingine. Lakini vile vile Mabwepande kulikuwa kuna chuo cha IFM na miradi mingine 20,000 ya viwanja.

Mheshimiwa Naibu Spika, imepita zaidi ya miaka minne. Wananchi hawajui mustakabali wao. Waliolipwa ni wananchi 160 tu kwa kipindi hicho zaidi ya wananchi 600, hawajui mustakabali wao ukoje. Lakini vile vile kwa upande wa Kwembe Serikali iliwaahidi wananchi kuwalipa pamoja na thamani ya ardhi na siyo mimea, kwa sababu pia Sheria zinasema hivyo na wananchi wa Kwembe hawana tatizo la kuhama. Tatizo lao la msingi ni ile haki yao waliyokubaliana kimsingi walipwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Mabwepande tunavyozungumza leo hii na nakumbuka wakati wa Kamati, nilivyokuja kwenye Kamati yao, nilimwambia kuna uvamizi wa hali ya juu unaendelea. Wananchi ambao waliiamini Serikali yao hawakulima, hawakujenga kwa sababu waliambiwa kwamba kuna mipango ya maendeleo, wakaa pembeni leo wamegeuka wakimbizi kwenye ardhi yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa namwomba Mheshimiwa Waziri kwa sababu nimeshapiga kelele katika Halmashauri, nimekwenda kwake kwa njia ya barua. Lakini hali kule ni mbovu. Naomba Serikali ichukue hatua. Mimi kama Mbunge wa Kawe silindi mvamizi hata mmoja. Wasije watu wakawa huko kwa maslahi yao, wanasema Mheshimiwa Halima Mdee anatuunga mkono. Sijatuma mvamizi yoyote akavamie eneo,nataka haki itendeke. Kwa hiyo, naomba suala la Mabwepande na suala la Kwembe naomba myafanyie kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala lingine Mheshimiwa Waziri kuna hili suala la Boko Dovya katika Shamba la Bwana Somji. Kuna taarifa hapa kwa vyombo vya habari kutoka kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kipindi kile alipokuwepo Mheshimiwa Chiligati, alikiri kwamba hili tatizo limekwisha. Serikali itachukua lile eneo kwa ajili ya kugawiwa kwa wananchi. Mpaka leo hakuna kinachoeleweka Somji anaendelea kuwasumbua wananchi ambao wako kwenye maeneo hayo. Kwa hiyo, naomba tafadhali tafadhali niweze kupata ufafanuzi kwa haya masuala.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine ni suala la Chasimba. Hili suala siyo dogo kama watu ambavyo wanataka walifikirie. Ni suala ambalo linahusisha wananchi zaidi ya 10,000. Ni suala ambalo ushahidi wake uko wazi na nimeeleza kwa kina sana kwenye hotuba yangu. Lakini nitalizungumza hapa. Inawezekana Serikali mkaja na scenario kwamba hili suala ni la zamani, lilienda Mahakamani na limeamualiwa Mahakamani. Kwa hiyo, wananchi waondoke, naomba mtumie busara. Nina hukumu ya Mahakama hapa. Nina documents hapa nitamletea Mheshimiwa Waziri zinazoonesha jinsi kijiji kilivyosajiliwa zinazoonesha kwamba mmiliki wa kiwanda hamiliki viwanja vyote vitatu kwa mantiki ya moja, nne na saba. Lakini nimesoma hukumu hapa, inasema naomba ninukuu kidogo: "It is the respondent case from a total twelve witnesses that the village officials of Boko". Mwisho wa kunukuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba muda wangu kidogo, kengele ya kwanza? It is the respondent case from a total of twelve witnesses that the village officials of Boko and Tegeta were contacted with the view of securing more land by organizing meetings with the villages. At the end of the day the respondent managed to buy a number of villages by wealth composition. Hukumu sababu katika hii kesi respondent alikuwa ni TUGHE. Kwa sababu ilikuwa ni Mahakama ya juu kabisa. Wanakiri kwamba walioweza ku-manage ni a number of villages sio all of the villages. Ndiyo maana nashukuru tu kwa maana ya Mheshimiwa Ole-Medeye. Nashukuru sana. Wananchi waliokuwepo pale ni watu wazima, tofauti na maeneo mengine ya uvamizi, unaona ni vijana vijana tu wamekuja juzi. Naomba Serikali iliangalie hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Lakini kesi ambayo ilikuwa inahusu watu takriban 1,000 ikaamuliwa on technical grounds kwamba linapokuja suala la ardhi, hatuangalii suala la representative's suit hairuhusiwi. Ikiwa ni Mahakama ya Rufaa Court of Appeal, haki za maelfu za wananchi zikaminywa simply because kwa uelewa wao labda mdogo waliamua wenzao 13 wakawakilishe Mahakamani na kati ya wenzao 13 waliokwenda kuwakilisha Mahakamani still walishindwa kuthibitisha wanne kati yao kwamba walilipwa fidia. Kwa hiyo, naomba Waziri asiwe mkali, naomba mtumie busara. Nawaombea wapiga kura wangu. Najua kuna haki imeminywa sehemu. Najua kuna interest za watu zinataka kuwaumiza watu maskini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasikia wanataka kuhamishiwa Mabwepande. Sisi hili hatuliafiki. Tunajua eneo la kiwanda ni kubwa. Wakitaka kujipanua wataacha chenji. Tunaomba muwasaidie wananchi na niwaambie kwa hili, maana Madiwani wa Kata hizo mbili ni wa CCM. Moja, tumesema iwe jua, iwe mvua, sisi tutakufa na wananchi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hatufanyi uchochezi. Lakini nadhani natumia lugha laini sana. Ukienda Chasimba mwenyewe, sijui! Ole Medeye, tulikwendanae na anajua zaidi, naomba tuwasaidie wananchi wetu. Kuna siasa hapa, kuna vyama vyote viko kule, tuweke utu kwanza; eneo lipo la kutosha, la msingi ni kwenda kufanya vikao na wananchi, kujua eneo la kiwanda liko wapi, wananchi wanaweza wakakaa wapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mwisho, hivi viwanja 20,000. Kunakuwa kuna tatizo kwamba, Wizara kwa nia njema kabisa mnaandaa miradi mbalimbali. Lakini tatizo ni kwamba, miradi hiyo haimilikishwi kwa wananchi ili waweze kujua viwanja vya wazi ni vipi? Viwanja vya shule ni vipi? Viwanja vya huduma za jamii ni vipi? Matokeo yake viwanja hivi vimegeuka kuwa sehemu ya Wenyeviti wa Mitaa kupata kula yao! Kwa hiyo, naomba katika miradi yoyote ambayo mliifanya, mwende mkai-review, muangalie maeneo ya wazi, maeneo ya umma ni yapi? Myafanye yawe wazi, ili wananchi kwenye maeneo hayo wawe walinzi wa ile rasilimali. Bila kufanya hivyo!

Mheshimiwa Naibu Spika, leo sheria haitambui kama Mwenyekiti wa Mtaa, anaweza akagawa eneo, lakini nitakwambia huko Dar-es-Salaam, wanagawa kwa kwenda mbele! Wakati nyie mnatoa maagizo huku, Wenyeviti wa Mitaa na baadhi ya Madiwani ambao sio waaminifu wanaendelea kuuza maeneo kwa kushirikiana na watu wa Manispaa ambao sio waaminifu. Kwa hiyo, naomba haya myaangalie kwa makini.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kabisa na ambalo pia sio la muhimu, ni viwanja vya wazi Mkoa wa Dar-es-Salaam. Tunajua mna changamoto kubwa kwa sababu, wengi ambao wamewahi kupewa hayo maeneo ya wazi, hususan katika maeneo strategic, ni wakubwa! Wengine wamejenga ma-bungalow yao! Sasa naomba leo mtuhakikishie wakati mnahitimisha, ile taarifa iliyotolewa na Kamati iliyoundwa na Mheshimiwa Lukuvi, mtaitekeleza kwa ukamilifu wake na ndani ya kipindi gani? Nakuhakikishia Mheshimiwa Tibaijuka, ukiniahidi hilo nitakuona kweli wewe ule moto wako unaendelea. Ukiwa unasitasita nitajua yale ambayo yanasemwa, ulianza kwa speed wenzio wakakuminya! Tunakuamini mama, namwamini Mheshimiwa Naibu Waziri sana kama ambavyo namwamini yeye sana, hii sekta ndio uhai wa nchi. Hii sekta tukiipuuza na naiambia Serikali, tukiipuuza watoto wetu, wajukuu zetu watakuja kuchinjana na hatutaki tutengeneze Tanzania ya kuchinjana!

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana.
 
Wanaosema siyo kazi ya mbunge kuleta maendeleo inabid waelewe kuwa kazi za mbunge zilizoelezwa kwenye katiba siyo mpaka wa majukumu yake. Kwa kiasi kikubwa majukumu ya mbunge huwa ni kutekeleza ahadi ambazo ziliwafanya watu wampe kura na vilevile kuzishughulikia kero kuu za wakazi wa jimbo.
Kama aliahidi atajenga daraja, hawezi kusema hiyo siyo kazi yake maana atakuwa anawatukana watu waliomuamini kuwa atajenga.

Ahadi za kujenga madaraja ndio zilichangia kumwangusha aliyekuwa mbuge wa Igunga kwa miezi michache kwa ahadi za Mh. Magufuli.

Kwa kifupi huo ni mtindo wa wabunge wa CCM.

Kazi ya mbunge ni kuwasemea wananchi wake katika kero zao, na kuhakikisha eneo lake linakumbukwa katika kugawa rasilimali za taifa.
 
Jamani mimi nauliza what has she done... not what she speaks in parliament.... if ubunge is all about speaking tuu... then we can all be there..... WHAt HAS SHE DONE FOR KAWE AND ItS PEOPLE??????????????


Mkuu naanza kupata shaka na actual motive ya uzi wako,,kazi yake kama mbunge naona kajitahidi sana kuwasemea wanajimbo kama ambavo baadhi ya wadau wameweka vipande vya hotuba yake,,sasa nikiangalia kwa makini kwenye maandishi yako makubwa naanza kupata shaka,ulitaka awagawie pesa mkononi?awaekee umeme majumbani mwao kwa pesa ya mfukoni mwake?
 
Wanaosema siyo kazi ya mbunge kuleta maendeleo inabid waelewe kuwa kazi za mbunge zilizoelezwa kwenye katiba siyo mpaka wa majukumu yake. Kwa kiasi kikubwa majukumu ya mbunge huwa ni kutekeleza ahadi ambazo ziliwafanya watu wampe kura na vilevile kuzishughulikia kero kuu za wakazi wa jimbo.
Kama aliahidi atajenga daraja, hawezi kusema hiyo siyo kazi yake maana atakuwa anawatukana watu waliomuamini kuwa atajenga.
Kupitia serikali ya Chama cha mabwepande ?
 
Mchango Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) 18 April 2012 (Hii ilichangia Rais kuwawajibisha mawaziri)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia, lakini vilevile niwasihi Wabunge wenzangu tusilalamike, jukumu letu sisi ni kuisimamia Serikali. Pale ambapo tunaona Serikali haitekelezi kile ambacho tunaagiza, tuna jukumu la kutoa azimio na kufanya chochote ambacho tunataka kufanya kama Bunge.


Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wetu wa kulalamika, utaratibu wetu wa kunung'unika ndiyo unawajaza viburi Mawaziri waliokuwepo hapo mbele. Ndiyo maana Tanzania yetu imefika sasa kwamba mtu akiwa Mbunge, akichaguliwa kuwa Waziri anachowaza yeye ni kwenda kupiga deal. Baadhi ya Mawaziri wako hivyo, tumeona, tumemsikiliza Mheshimiwa Kangi Lugola, nimemsikiliza kwa makini nilikuwa ofisini, anazungumza kwa namna gani Mawaziri badala ya kwenda kutekeleza wajibu ambao Rais amewaamini, kumsaidia kuongoza hii nchi wanafanya mambo ndivyo sivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana Wabunge wanalalamika, mimi hiki ni kipindi cha pili, Mheshimiwa Kafulila kasema kweli ukisoma Hansard mambo ambayo yanalalamikiwa leo ndiyo mambo ambayo tuliyajadili Bunge lililopita, Mawaziri wamejisahau.

Kuna baadhi wanafanya kazi, lakini kuna wengi wanadhani kwa kupewa Wizara, kupewa shangingi, kwa kupewa nafasi ya kusaini mikataba ni sehemu ya kupata pesa na majuzi nilisikitishwa sana kwa kuona kwa kiasi gani Mawaziri wetu hawako serious. Lilipoulizwa swali kuhusiana na mashamba kule Kapunga Mbarali, aliuliza Mbunge hapa kwamba jamani maeneo ya wananchi yamemwagiwa sumu
na mwekezaji?

Mheshimiwa Naibu Spika, Naibu Waziri wa Kilimo
anasimama hapo anatoa majibu kama vile hilo suala lilikuwa halijawahi kumfikia, kama vile hilo suala lilikuwa halijawahi kujadiliwa kwenye Vikao vya Bunge, kama hivyo hilo suala halijawahi kutolewa maazimio kufuatia taarifa ya Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma mwaka 2009 kuhusiana na suala la Kapunga.

Maeneo ya wananchi, eneo la wanakijiji linalokaribia hekta 1800 limechukuliwa na mwekezaji kwa kushirikiana na watu wa Serikali ambao siyo waaminifu kinyume na utaratibu. Kamati yetu ikasema kupitia Mwenyekiti wetu, alikuwa Zitto, Serikali ikaji-commit lakini utashangaa miaka miwili na nusu au mitatu baadaye Waziri amesahau, hajui kinachoendelea, anatoa
ahadi mpya, ndiyo Mawaziri wetu, nchi itakwenda?

Haiwezi kwenda! Kwa hiyo, mimi nawaomba Wabunge wenzangu ifike kipindi hawa watu kwa sababu wanalipwa, mara Waziri akienda Jimboni kuna mambomambo huko, wanalipwa ili wafaye kazi za wananchi. Kama hawafanyi kazi za wananchi, tuna uwezo wa kuwazuia katika mazingira mbalimbali, mamlaka hayo tunayo. Tuache
kulalamika, tukilalamika, wananchi waliotuchagua watatushangaa! Watashangaa kwamba Wabunge tumewapeleka wakaisimamie Serikali lakini wao wanageuka walalamikaji, wananchi wafanye nini? Tutekeleze wajibu! Naomba katika hili masuala ya itikadi tuweke pembeni, tunapojadili masuala ya msingi tuache kuangalia u-CCM, u- CUF, u-CHADEMA na u-TLP. Tukiamua kumwadhibu Waziri, tunamwadhibu kwani ni jukumu letu kufanya hivyo. Kwa hiyo, mimi naomba tuache kulalamika.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili, Kamati ya Mashirika ya Umma imezungumzia masuala ya viwanda nadhani pia kwa sababu ya muda hawakuweza kupata nafasi ya kuzungumzia kwa kina taarifa ya ufuatiliaji wa mashamba na viwanda hasahasa mashamba kwa sababu viwanda wamei- capture vizuri sana shughuli ambayo imefanywa na CHC. Tumekuwa tukizungumza kwamba watu wezi, mafisadi na kadhalika lakini kuna taarifa huku zinatisha. Zinatisha kwa nini?

Kuna huyu mtu anaitwa Chavda sijui amekufa au yuko hai? Watu wa aina ya akina Chavda kama kweli wapo hai wanatakiwa wakamatwe kama wezi wengine.

Wakamatwe na wanyongwe, kwa nini tunasema hivi? Taarifa hapa inamwonyesha Bwana Chavda katika mashamba makubwa matatu tofauti yenye ukubwa wa kati ya hekta 5000-6000, mashamba matatu tofauti kwa ajili ya dili zilezile ambazo Mawaziri tuliowapa ridhaa kipindi kile wakamuuzia eneo hilo kwa bei chee! Alichokifanya Bwana Chavda, akaenda kuchukua mkopo kwa mashamba yote matatu, baada ya kuchukua mkopo kwa dhamana ya shamba, mali ya Watanzania ambao wengi hawana ardhi akachikichia, shamba akalitelekeza, eti Serikali inasema inaangalia itamlipaje fidia mtu mwingine aliyeuziwa na Benki ya CRDB ambapo waliuza shamba lile kwa sababu lilitumika kama security ili eti atafutwe mwekezaji mwingine, lugha nyepesi kwa masuala mazito!

Mheshimiwa Naibu Spika, tumetoka Arumeru, ardhi Tanzania itatumwagisha damu baadaye, kila unapokwenda ni mgogoro wa ardhi. Akija mgeni, Waswahili tuna msemo usemao 'mgeni njoo mwenyeji apone'. Tanzania akija mgeni kwenye suala la ardhi, msemo unakuwa 'mgeni njoo mwenyeji asulubike'. Leo Mtanzania wa kawaida ni vigumu kupata hekari moja ya ardhi, wanaishia kuwa wavamizi, lakini kuna wajanja wachache, wenye fedha, wanaojua kula na viongozi Serikalini, wanapewa maeneo chee, hawayaendelezi na Serikali ina-incur gharama mara mbili, hatuoni haya?

Waheshimiwa Wabunge, mimi naomba, hawa watu sisi ni vijana, watoto na wajukuu zetu sisi tutawaachia nini? Hawa watu wazima wanatuangusha, inawezekana wanaona future yao miaka 10 mbele wameshakatika, sisi tuna miaka 30 au 40 mbele mnataka mtuachie nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa dhati, Bunge tuna meno, haiwezekani mashamba 14 makubwa yenye ukubwa kati ya hekta 4000-5000 watu wamechukua, wameyatelekeza halafu Serikali haichukui hatua, inabembelezana nao, kama ninyi siyo wadau, kwa nini hamchui hatua? Kwa hiyo, naomba sheria ichukue mkondo wake, tunavyohukumu mafisadi wengine na hawa ni mafisadi vilevile kama wanashindwa
kusimamia mali za Watanzania.


Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni la TBS, ninasikitika majibu ya Mawaziri na ni kwa mtindo huohuo wa masuala ya ardhi. Hapa kuna report ya CAG, anasema makampuni yamepewa kinyume na utaratibu, makampuni hayana vifaa, makampuni hayalipi tozo kwa TBS lakini bado wanarudiwa kupewa mikataba, eti Waziri anasimama hapa anatoa majibu mepesi, Waziri anasimama hapa anaongea lugha nyepesi, wataalamu wanashauri hii kampuni haifai kupewa kazi hii kwani haina uwezo, lakini wanalindwa. Kwa hiyo, mimi naomba Wabunge tusimame, tumechoka kulalama, msilalame kwani wananchi watawarushia mawe.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
 
Ahadi za kujenga madaraja ndio zilichangia kumwangusha aliyekuwa mbuge wa Igunga kwa miezi michache kwa ahadi za Mh. Magufuli.

Kwa kifupi huo ni mtindo wa wabunge wa CCM.

Kazi ya mbunge ni kuwasemea wananchi wake katika kero zao, na kuhakikisha eneo lake linakumbukwa katika kugawa rasilimali za taifa.

Kweli, lakini kwenda kuongea tu haitoshi. Mbunge has to go an extra mile. Ndio maana wakati wa kampeni wagombea hutoa ahadi. Si sahihi kutoa ahadi halafu ukishachaguliwa unasema wewe kazi yako kuongea tu Bungeni!
Vilevile mbunge anatakiwa kuwa na uwezo wa kuonyesha leadership wa kuorganise community kufanya shughuli za maendeleo. Kwa Dar es Salaam swala kama ulinzi shirikishi lingefaa kuhamasishwa na wabunge. Kiujumla inatakiwa baada ya mwaka mmoja mbunge awe na list ndefu ya mambo aliyowafanyia wananchi wake ambayo impact yake inaonekana kwenye maisha ya watu ya kila siku, siyo list ya matamko aliyotoa na kauli mbalimbali bungeni na vikaoni.
 
halima mdee kama mwakilishi wa wana kawe ndio mwenye haki ya kuiuliza serikali imefanya yapi pale jimboni kawe kuanzia uhuru mpaka leo hii.
Umemsaidia sana huyo jamaa, kama hajakuelewa basi hata achorewe atagoma tu!!!
 
Ahadi za kujenga madaraja ndio zilichangia kumwangusha aliyekuwa mbuge wa Igunga kwa miezi michache kwa ahadi za Mh. Magufuli.

Kwa kifupi huo ni mtindo wa wabunge wa CCM.

Kazi ya mbunge ni kuwasemea wananchi wake katika kero zao, na kuhakikisha eneo lake linakumbukwa katika kugawa rasilimali za taifa.

Hiyo inaweza kuwa sababu ya zaidi ya 67% ya wabunge kuwa wa CCM. Kama wabunge wa upinzani wataendelea kutegemea zaidi mdomo basi hiyo percentage itabaki hivyo miaka mingi sana ijayo.
Wapinzani waliopenetrate wanatakiwa waonyeshe mfano ili wananchi wajue wanapochagua mpinzani kuna kitu kinabadilika katika maisha yao ya kila siku. Ukitoa matamko hata yakiwa makali vipi kama hayana direct impact na maisha ya mtu ya kila siku, hayawezi kupewa thamani na jamii husika.
 
Hiyo inaweza kuwa sababu ya zaidi ya 67% ya wabunge kuwa wa CCM. Kama wabunge wa upinzani wataendelea kutegemea zaidi mdomo basi hiyo percentage itabaki hivyo miaka mingi sana ijayo.
Wapinzani waliopenetrate wanatakiwa waonyeshe mfano ili wananchi wajue wanapochagua mpinzani kuna kitu kinabadilika katika maisha yao ya kila siku. Ukitoa matamko hata yakiwa makali vipi kama hayana direct impact na maisha ya mtu ya kila siku, hayawezi kupewa thamani na jamii husika.
nasikitika sana nikiona hata Iman Kondo hajui majukumu ya mbunge!
 
[FONT=lucida grande, tahoma, verdana, arial, sans-serif] [/FONT]Kunasababu wabunge wengine ni ngumu kung'oleka kwao mbali na kwamba kuna wenye uwezo wa kifedha kufanikisha mambo mengine bila serekali.... lakini hata kama jimbo lako si kwenu ni vizuri kuwajali waliokuchagua kwa ukaribu wa kupindukia na ikibidi nenda katafute sulisho hata nje ya serekali kwa matatizo yao kama hela za sabodo na visima vya Arumeru.... swali ninalouliza hapa leo halima watamuuliza miaka miwili ijayo.... ulitufania nini sisi wana Kawe?.... mimi sina ushabiki wa kichama ushabiki wangu ni wa kimaendeleo pekee.... na kila mtu akiwajibika na maendeleo hata kama madogo...
 
Back
Top Bottom