JIULIZE KWANZA
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 2,569
- 500
Wakati mwingine tunafikiri wapinzani ni dawa ya matizo yetu kumbe si kweli ukimya wa Halima Mdee kwenye tatizo letu la Madale hakika nimeushangaa sana.
Nilikuwa na imani kuwa wabunge wa upinzani ni wabunge mbadala. Mimi ni mmoja wa waathirika wa bomoa bomoa ya Madale ambayo kuna kila aina ya ujanja ujanja lakini tangu tupate matatizo hayo sijawahi kuona mbunge wangu HALIMA MDEE akisema lolote au hata kuwatembelea waathirika kujua shida zao na namna ya kuwasaidia kwani ni wapiga kura wake.
wapo wanaolala nje hadi sasa, wapo walionyang'angwa ardhi kwa nguvu ya fedha lakini Halima ambaye ni mjumbe wa baraza la madiwani la Kinondoni nilitegemea angekuwa na kauli ya kutueleza wananchi tulioathirika na bomoa bomoa hiyo katika eneo la Madale nakalekwa, madale tuaroho na madale nakasangwe. Ni zaidi ya mwezi sasa tangu kupita kwa bomoa bomoa hiyo.
Halima anajua ukweli kwa sababu yuko kwenye vikao vya manispaa ya kinondoni lakini pia niliambiwa kasomea sheria ( i stand to be corrected) ni sheria ipi inaruhusu kumnyang'anya mwananchi aliyekaa eneo kwa miaka kumi bila kuendelezwa hao wamiliki halali akina Michael Chacha na wenzake walikuwa wapi miaka yote. Sheria inatoa miaka mitatu tu kwa ardhi ambayo haijaendelezwa kunyang'anywa au kuwa mali ya yule anayelindwa na sheria hiyo kwa maana kwamba kama mwananchi ameishi hapo kwa zaidi ya miaka mitatu bila mmiliki halali kutokea sheria inatambua na kumpa umiliki yule aliyopo kwa wakati huo.
My take: Halima Mdee acha kukimbilia kigamboni kuwalilia wananchi wake kutokakana na hofu ya mji mpya anza na jimbo lako. Bado tunakusubiri uje kuongea na sisi wananchi wa Madale ingawa umechelewa.
source: Mimi mwenyewe nilikuwa na kiwanja cha nusu heka Madale.
Sera ya bomoa bomoa Manispaa ya Kinondoni ambayo inayoongozwa na Meya wa CCM sasa imehamia kwenye Jimbo la Uchaguzi la Kinondoni kwa Mh. Iddi Azzan baada ya kutoka Jimbo la Kawe.
Jana wakazi wa Sinza Mori na Bamaga walibomolewa nyumba zao. Zoezi hilo lililoacha simanzi, majonzi na vilio kwa wakazi hao, limefanyika jana na kushuhudiwa na kamera ya mwandishi
Greda likijiandaa kuanza kazi!
Wananchi wa Sinza wakijaribu kuokoa mali zao kabla Greda halijapitia
Wanamgambo wa Halmashauri wakisimamia zoezi
Greda likivunja Geti la Nyumba
(Habari /Picha : Haruni Sanchawa, GPL)
Hivi Harima mdee ndio nani tena?
ACHA UJINGA WEWE,uvamie maeneo ya watu kwa ujinga wako alafu umlalamikie halima?usitegemee msaada kwa ujinga wako na halima hayuko kutetea maovu na kura usimpe kama unatabia ya kuiba vya watu ukitegemea kuna mtu wa kukutetea,usipoteze muda wako kumsubili mbuge kwa upuuzi wako na ukome maana uko mmezidi kuvamia maeneo ya watu,ulivamia ukisubili hiyo sheria ya mwaka 47 pole na umkome mbunge wetu na uvae gamba tuje tukuchome moto
mm nafikiri kama wananchi tunapaswa kuwa makini. haiwezekani ww ukauziwa na mtu anayedai mmiliki pasipo ushahidi usio na shaka. ukinunua kiwanja kwa mwizi huwezi kuwa mmiliki halali kwani aliyekuuzia hana umiliki halali
wakati mwingine tulaumiane wananchi, mm mwenyewe nina viwanja maeneo yasiyo rasmi, nilifanya yafuatayo-
1. nilifuatilia kujua uhalali wa mmiliki
2. nilihakikisha tunasainiana mkataba kuwa kama amenificha basi atanirudishia gharma zangu na za maendelezo
3. nilifuatilia kujua nyumba yake binafsi anayoishi, siyo ya kupanga
4. nilisaini mkataba na mmiliki kwa wakili
pia ni vizuri kujua ramani ya jiji na mpango wa serikali. usipojua hata kama CUF itaingia madarakani hata baada ya miaka 50 au 100 watakaokuwa hai serikali itatekeleza mpango wake
hata mbunge akitaka kutoa kauli ktk mazingira haya sio salama kwake kwani anaweza kuzushiwa na kucafuliwa kuwa anahimiza wananchi kukiuka sheria. sheria ni kwa wananchi wote
MAMA POROJO:f
hatusemi halima aje kutengua maamuzi ya bomoa bomoa bali aje kutusikiliza hata mahakamani wahalifu husikilizwa na wakati mwingine wanashinda kesi dhidi ya dhuluma
Operesheni ya kuwaondoa wavamizi wa mashamba iliyoanza jana saa 12 asubuhi, ilifanywa na Serikali ya Wilaya ya Kinondoni chini ya ulinzi mkali wa askari polisi waliokuwa na magari yapatayo 30 yakiwamo matingatinga manne na gari la wagonjwa. Jumla ya nyumba 300 zabomolewa Mabwepande. | Dullonet Tanzania
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema wametumia nguvu ya wastani katika kusimamia operesheni hiyo na watu takribani 20 wanashikiliwa na jeshi hilo baada ya kuanzisha vurugu. "Tulipata upinzani kidogo wakati tunaanza, jambo ambalo tulilazimika kutumia mabomu ya machozi kutawanya na kuendelea na kazi hiyo. Kazi imefanyika vizuri na hakuna askari wala raia yeyote aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa," alisema Kamanda Kenyela ambaye katika awamu ya pili ya bomoabomoa, alitaka kusiwapo na uchomaji moyo nyumba zilizobomolewa. Source Habari Leo Jumla ya nyumba 300 zabomolewa Mabwepande. | Dullonet Tanzania
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana alisema eneo hilo limekuwa na mgogoro wa ardhi wa muda mrefu na kuwa kazi waliyoifanya ni kuwaondoa wavamizi wapya katika eneo hilo lililovamiwa la kata za Mabwepande na Madale.
"Mgogoro wa hapa ni tofauti, zamani kulikuwa na tatizo la umilikaji wa watu zaidi ya mmoja katika eneo moja, lakini sasa kuna kundi la vijana ambao wanavamia maeneo ya watu na baadaye wanayauza, wengi wa waliobomolewa ni wale waliouziwa na wavamizi," alisema Rugimbana.
Nilikuwa na imani kuwa wabunge wa upinzani ni wabunge mbadala. Mimi ni mmoja wa waathirika wa bomoa bomoa ya Madale ambayo kuna kila aina ya ujanja ujanja lakini tangu tupate matatizo hayo sijawahi kuona mbunge wangu HALIMA MDEE akisema lolote au hata kuwatembelea waathirika kujua shida zao na namna ya kuwasaidia kwani ni wapiga kura wake.
wapo wanaolala nje hadi sasa, wapo walionyang'angwa ardhi kwa nguvu ya fedha lakini Halima ambaye ni mjumbe wa baraza la madiwani la Kinondoni nilitegemea angekuwa na kauli ya kutueleza wananchi tulioathirika na bomoa bomoa hiyo katika eneo la Madale nakalekwa, madale tuaroho na madale nakasangwe. Ni zaidi ya mwezi sasa tangu kupita kwa bomoa bomoa hiyo.
Halima anajua ukweli kwa sababu yuko kwenye vikao vya manispaa ya kinondoni lakini pia niliambiwa kasomea sheria ( i stand to be corrected) ni sheria ipi inaruhusu kumnyang'anya mwananchi aliyekaa eneo kwa miaka kumi bila kuendelezwa hao wamiliki halali akina Michael Chacha na wenzake walikuwa wapi miaka yote. Sheria inatoa miaka mitatu tu kwa ardhi ambayo haijaendelezwa kunyang'anywa au kuwa mali ya yule anayelindwa na sheria hiyo kwa maana kwamba kama mwananchi ameishi hapo kwa zaidi ya miaka mitatu bila mmiliki halali kutokea sheria inatambua na kumpa umiliki yule aliyopo kwa wakati huo.
My take: Halima Mdee acha kukimbilia kigamboni kuwalilia wananchi wake kutokakana na hofu ya mji mpya anza na jimbo lako. Bado tunakusubiri uje kuongea na sisi wananchi wa Madale ingawa umechelewa.
source: Mimi mwenyewe nilikuwa na kiwanja cha nusu heka Madale.
mtabeba na makapi mwaka huu katika 22 mmewachuja kuona wanafaa???? kisa kuikomoa CCM.
Huu ndio msimamao wa chama chako hata CCM ikifanya zuri ndio jukumu la upinzani wala haishangazi.
Tupe ushahidi kwamba wamelipwa????????????? unaweza kuficha fidia ya watu wengi kiasi hicho!!!! ni siri gani hiyo ya watu wengi hivyo???
bad language.... uko upande wa chadema na ndio maana unasilikiza na kuamini ya upande mmoja tu
Mimi naona ccm na nuru tororo ..... Ni mtazamo wangu tu.
Nimefurahishwa na bango lako la wino wa kijani ni rangi ya CCM
MAMA POROJO,
Maneno yako mekundu hayakutoka moyoni, ni unafiki.
Nimechukua muda kidogo kuangalia posts zako za zamani. Baadhi ya nilizoona ni hizi:
Nimeelewa kwa nini lawama zote unamtupia Halima Mdee, na huoni kuwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda CCM, kuwa ndiye aliyetuma wabomoaji na askari.
Ndio maana kwenye thread hii umekazana kujaza lawama dhidi ya Halima Mdee.
Siasa za kupakana matope hazilipi MAMA POROJO!
nyie hamjajua tu, ila ukweli ni kwamba wabunge wanawake hawana uwezo wa kuwakilisha jimbo. Nafasi sahihi kwa wanawawe ni ubunge wa viti maalum. Mdee alikuwa viti maalum ghafla mkamkabidhi jimbo kitu ambacho yeye haoni kama ni dili sana kwake. Yeye kugombea kawe ilikuwa shinikizi la chama chake na walikuwa hawategemei ushindi ndio maana walikuwa wamesha mtengea nafasi yake ya viti maalum aliyoizoea na ambayo yeye anaimudu kwani anakuwa hana majukum kijimbo ila kichama tu.
Sawa Mr Bright, Mie naona kama kuna mtu anahitaji kufundishwa udhaifu wa mwanamke katika nyadhifa za uongozi ni wewe. Mwanamke ameubwa kutoka ubavuni mwa mwanaume. Mwanamke ana kazi anazoziweza na si zote. Ebu kwa uelewa wako nitajie mbunge yeyote wa chama chochote hapa bongo mwanamke unayeona ana qualify kuwa kiongozi.nani kakwambia jinsia ndiyo inaongoza jimbo?
Watu tunaangalia huwezo wa mtu sio jinsia! Kumbe kuna watu bado mnaitaji elimu kuondokana na mawazo mgando kama hayo.
Jaribu kufikiri kwa kina.
mm nafikiri kama wananchi tunapaswa kuwa makini. haiwezekani ww ukauziwa na mtu anayedai mmiliki pasipo ushahidi usio na shaka. ukinunua kiwanja kwa mwizi huwezi kuwa mmiliki halali kwani aliyekuuzia hana umiliki halali
wakati mwingine tulaumiane wananchi, mm mwenyewe nina viwanja maeneo yasiyo rasmi, nilifanya yafuatayo-
1. nilifuatilia kujua uhalali wa mmiliki
2. nilihakikisha tunasainiana mkataba kuwa kama amenificha basi atanirudishia gharma zangu na za maendelezo
3. nilifuatilia kujua nyumba yake binafsi anayoishi, siyo ya kupanga
4. nilisaini mkataba na mmiliki kwa wakili
pia ni vizuri kujua ramani ya jiji na mpango wa serikali. usipojua hata kama CUF itaingia madarakani hata baada ya miaka 50 au 100 watakaokuwa hai serikali itatekeleza mpango wake
hata mbunge akitaka kutoa kauli ktk mazingira haya sio salama kwake kwani anaweza kuzushiwa na kucafuliwa kuwa anahimiza wananchi kukiuka sheria. sheria ni kwa wananchi wote