MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 793
wafu wawzike wafu wenzao, ww km unasubiria HM aje aalifanye hiili katuu hawezi kutokea, na umempa jukummu kubwa sana ambalo haliwezii, yeye ni mbbunge wa starerhe na mambo ya anasa, nenda bilicanas utamkuta kila siku usiku anakula raha kwa mrija
Hata mimi mwanzo nilidhani ivo ivo baada ya kuwachunguza sana wanasiasa nilikuja kuamini kuwa wanasiasa ni watu wa ajabu sana, huwa wanawachezea wananchi kisaikolojia kwa kuyaongea sana yale madhaifu ya serikali iliko madarakani ikijiaminisha kwa wananchi kuwa wao ni ufumbuzi wa matatizo hayo kumbe ni ulongo.
Halima mdee lile jimbo asingeshinda sema wana magamba walichemka kwa kumtosa mgombea aliyekuwa anakubalika. Kaka huyo dada hana wasiwasi na nyie kwani anajua yeye yuko anajenga chama (Movement 4 Chagaz M4C, or Movement 4 christian M4C)akimaliza atarejea
Kumbe mwenzetu kabaila. Ukwasi wote huo unalilia kiwanja cha uvamizi? Wacha wakuvunjie kama una hati nenda kadai haki yako mahakamani.Kuwa na kiwanja Madale na kuwa mwathirika wa huko sio lazima niishi huko Madale. Mtu akiwa na viwanja 10 atakuwa anaishi kote? Tuwe makini kusoma kinachoandikwa. wapo walio na nyumba Madale lakini walipangisha na pia ni waathirika wa bomoa bomoa hiyo.
Two wrongs can never make it right. Kupewa viwanja kwa wavamizi wa jangwani sio kuhalalisha uvamizi wa viwanja. Madale hakuna maafa yoyote, wavamizi wanaondolewa full stop. Sera zenu mbovu ndio zinazokuza uhalifu kwa ajili ya kutetea wahalifu. Mfano, watu wamegomea sensa wakakamatwa, kundi fulani likaandamana waachiwe, mkafanya hivyo. Wengine wakaharibu mali kwa kuchoma nyumba za ibada wakaachiwa, mto wa mbu vilevile walichoma nyumba za ibada, maandamano waachiwe ikawa. Usilie, maana ndio mfumo mliojitengenezea, wahalifu ndio wenye haki. Umesahau EPA? Wewe kuvamia unaona ni haki, ila kuvunjiwa malalamiko chungu nzima. Makanisa yanachomwa wala hatuwasikii mkitoka povu, ngoja uchomwe msikiti hata mmoja, maandamano nchi nzima, kama vile wao tu ndio wenye haki ya kuabudu, wengine hapana. Kama mmeamua kubariki mfumo wa kihalifu, mkubali na machungu yake maana hayaelekei upande mmoja tu.Hata wa mabondeni walipewa fursa ya kupelekwa Mabwepande ingawa walikuwa wavamizi . Kwa nini Mdee hataka kujua ambacho sisi tunacho kuhusu mgogoro huo?
Ni wazi CCM hawakuweka mgombea mzuri wa kupambana na Mdee kama Kippi Warioba asingeweza kupita na hilo CCM wanajutia. Huyu dada nilikuwa na imani naye sana lakini baada ya kukuta anakaa kimya kwa takribani wakazi zaidi ya 1000 kukumbwa na bomoa bomoa sina imani naye tena.
Katika maelezo yako umedai wewe ni mwathirika wa bomoabomoa ya madale, kama haitoshi ulipoahidiwa heka moja ya kiwanja ukasema kinachokuuma ni pesa uliyowekeza pale na si ukubwa wa kiwanja. Na sasa unadai hukai huko ila ni reporter wa kinachoendelea madale. Hii inaonesha wazi jinsi watu wa aina yako walivyo na asili ya popo, si ndege si mnyama. Katika kutafuta umaarufu mnajifanya ni wenzetu, mambo yakienda kombo hamkuhusika. Hiyo ni picha halisi ya viongozi wa ccm, kukwepa uwajibikaji. Jiamini ndugu na simamia unachokiamini. Sio mara shule za kata, mmechemsha mnaziruka na kukimbilia kilimo kwanza. Mnaendesha nchi kiholela lazima tuwaseme, tukikaa kimya hatuwasaidii na hatuisaidii nchi. Narudia tatizo si Halima Mdee, wala CDM, tatizo ni uongozi wa hovyo wa CCM. Ili tuendelee tunahitaji mambo manne 1. Watu (Human capital, technological capital) 2. Ardhi (Land and all embodied in it) 3. Siasa safi (Dira, Mfumo, sera (Vision, Mission)) 4. Uongozi bora (Planning, Coordinating, Organising, Leading, Strategies). Sasa mama porojo, tunapopungukiwa ni hapo namba nne, na ndio engine yenyewe ya kuleta maendeleo. Hivyo tunapoilaumu serikali yako kwa kushindwa ni hapo kwenye namba nne. Na ndio maana JK na EL wanapishana kauli 1. Kilimo kwanza 2. Elimu kwanza. The issue is no. 4!!!!!! NEED I SAY MORE?
Hata wa mabondeni walipewa fursa ya kupelekwa Mabwepande ingawa walikuwa wavamizi . Kwa nini Mdee hataka kujua ambacho sisi tunacho kuhusu mgogoro huo?
Ni wazi CCM hawakuweka mgombea mzuri wa kupambana na Mdee kama Kippi Warioba asingeweza kupita na hilo CCM wanajutia. Huyu dada nilikuwa na imani naye sana lakini baada ya kukuta anakaa kimya kwa takribani wakazi zaidi ya 1000 kukumbwa na bomoa bomoa sina imani naye tena.
Mimi siwasemei wengine hii ni shida yangu na wananchi walioomba nipaze sauti kwa niaba yao kule Madele.
Bado Kesi iko mahakamani lakini tumebomolewa nyumba na kunyang'anywa ardhi tulitegemea mbunge ungekuja kusaidia namna ya kutafuta haki mahakamani lakini uko kimya. Wananchi masikini wamefungua kesi lakini kabla ya hukumu tumeondolewa kwa nguvu.
Operesheni ya kuwaondoa wavamizi wa mashamba iliyoanza jana saa 12 asubuhi, ilifanywa na Serikali ya Wilaya ya Kinondoni chini ya ulinzi mkali wa askari polisi waliokuwa na magari yapatayo 30 yakiwamo matingatinga manne na gari la wagonjwa. Jumla ya nyumba 300 zabomolewa Mabwepande. | Dullonet Tanzania
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema wametumia nguvu ya wastani katika kusimamia operesheni hiyo na watu takribani 20 wanashikiliwa na jeshi hilo baada ya kuanzisha vurugu. "Tulipata upinzani kidogo wakati tunaanza, jambo ambalo tulilazimika kutumia mabomu ya machozi kutawanya na kuendelea na kazi hiyo. Kazi imefanyika vizuri na hakuna askari wala raia yeyote aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa," alisema Kamanda Kenyela ambaye katika awamu ya pili ya bomoabomoa, alitaka kusiwapo na uchomaji moyo nyumba zilizobomolewa. Source Habari Leo Jumla ya nyumba 300 zabomolewa Mabwepande. | Dullonet Tanzania
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana alisema eneo hilo limekuwa na mgogoro wa ardhi wa muda mrefu na kuwa kazi waliyoifanya ni kuwaondoa wavamizi wapya katika eneo hilo lililovamiwa la kata za Mabwepande na Madale.
"Mgogoro wa hapa ni tofauti, zamani kulikuwa na tatizo la umilikaji wa watu zaidi ya mmoja katika eneo moja, lakini sasa kuna kundi la vijana ambao wanavamia maeneo ya watu na baadaye wanayauza, wengi wa waliobomolewa ni wale waliouziwa na wavamizi," alisema Rugimbana.
BAADA ya bomoa bomoa, yameibuka madai kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) wilayani Kinondoni, Anna Luvanda ‘Mama Makete' amekuwa akiwatumia wananchi wanyonge kwa maslahi yake binafsi kuvamia maeneo yaliyopo katika wilaya hiyo.
Agosti 22, mwaka huu Manispaa ya Kinondoni kwa kushirikiana na vyombo vya dola, ilibomoa nyumba zaidi ya 300 zilizojengwa katika Kata ya Mabwepande na Madale, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam kwa madai ya kuvamia eneo hilo. Pamoja na hilo, Mama Makete anadaiwa kuwapa pesa kinamama na watoto na kuwapakia katika magari binafsi na kisha kuwatelekeza karibu na ofisi ya Ikulu.
Akisoma taarifa ya umoja wa watu waliovamiwa maeneo yao jijini Dar es Salaam juzi, katika mkutano uliofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Kituo cha Polisi Kawe, Kaimu Mwenyekiti wa umoja huo, James Mramba, alidai Mama Makete amekuwa akitumia cheo chake kwa maslai binafsi. Mramba alidai kuwa Mama Makete aliwakodisha kinamama na watoto wao na kuwalipa ujira mdogo ili wafike katika ofisi za Ikulu waonane na Rais Jakaya Kikwete.
"Huyu kigogo ndiye chanzo cha vurugu zote za uvamizi wa maeneo katika wilaya hii, amekuwa akiwatumia wanyonge na mbaya zaidi wakati wa bomoa bomoa aliwachukua wanawake na kuwapeleka karibu na Ikulu.
"Aliwafikisha hapo ili waende wakaeleze kuwa wameonewa na manispaa na waweze kupatiwa maeneo hayo," alidai Kaimu Mwenyekiti huyo.
Aidha, alidai Mama Makete amekuwa akifadhili wananchi waliovunjiwa maeneo hayo kwa sasa kwa kuwapatia hifadhi katika eneo la machimbo ya kokoto ambako wameweka kambi.
Alibainisha kuwa, anashindwa kujitokeza hadharani kwa kuwa anajua eneo analomiliki hakulipata kihalali.
Akichangia katika mkutano huo, Mbunge wa Viti Maalumu, Rita Mlaki (CCM), alisema serikali imeshafanya utafiti wa kina juu ya kuwepo kwa kigogo huyo na ripoti yake imeshafika mezani kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick.
"Hatuna haja ya kulalamika juu ya jambo hilo… ninajua Serikali ya CCM haiwezi kumkubatia mtu kama huyo," alisema.
Mlaki alidai kwa sasa kuna uhuni unafanywa na wavamizi hao ambapo wanajipanga na kuandaa nyaraka, ili ionekane wazi kuwa maeneo hayo ni mali yao kihalali.
Huku akikitetea chama chake, Mlaki alidai kuwa CCM haiwezi kukubali kigogo huyo aendelee kukichafua chama hicho, hivyo anaamini hatua zaidi zitachukuliwa kukomesha vitendo hivyo vya kifisadi. Hata hivyo, alisema ingawa wavamizi walikimbilia Tume ya Haki za Binadamu, bado wanayo nafasi ya kukutana na kiongozi wa tume hiyo ili kujua undani wa maeneo hayo.
"Nasi tusimame imara, Tume ya Haki za Binadamu ninawafahamu viongozi wake na tunaweza kwenda kule na tumevumilia vya kutosha kwa kuwa tunaiheshimu serikali maana nasi tulikuwa na uwezo wa kuwa Mungiki," alisema.
Naye Seif Magugu, alidai kigogo huyo anamiliki machimbo ya kokoto na ndiye mfadhili mkuu wa vijana wanaoendesha vitendo vya kibabe katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.
Akizungumzia tuhuma hizo, Mama Makete aliziita ni za kisiasa na zina lengo la kumchafua.
Alifananisha tuhuma hizo na methali ya ‘akutukanaye hakuchagulii tusi' na akasema hawezi kuitumia Ikulu kuendesha vitendo viovu.
"Mimi nina malori matano na hayo sikai nayo, sasa ni muda upi niliwabeba hao watu na kwenda kuwashusha Ikulu?" alihoji.
Alisema eneo analodaiwa kuvamia aliuziwa miaka nane iliyopita, hivyo kama kuna mtu ana umiliki halali wa eneo hilo, hana budi kujitokeza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema, Jeshi la Polisi litafuatilia juu ya kuwepo kwa kikundi cha wavamizi kuweka kambi katika eneo la mchimbo ya kokoto.
Imeandikwa na Betty Kangonga
Source: Tanzania Daima
http://www.dullonet.com/?p=24350
Bado Kesi iko mahakamani lakini tumebomolewa nyumba na kunyang'anywa ardhi tulitegemea mbunge ungekuja kusaidia namna ya kutafuta haki mahakamani lakini uko kimya. Wananchi masikini wamefungua kesi lakini kabla ya hukumu tumeondolewa kwa nguvu.
Bado hajaolewa, mchumba wake wa mwisho alikuwa Joshua Nasari sijui wamefikia wapi walitangaza hadharani kwenye uchaguzi wa Arumeru Mashariki.
Nafikiri Mdee yupo below expectations kwa mtizamo wa wananchi wengi,mfano ni juzi tu nilikuwa pale afrikana kwa vijana wa bodaboda na bajaji kwa shughuli maalum nao wanalalamikia mwenendo wa mbunge kutoonekana hasa kutatua kero zao za muda mrefu! Mdee take care my sister tunakutakia mema kamanda!