What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

Huyu Marabu wa hapa Tegeta Namnga naona ameiweka sehemu ya serikali mfukoni mwake
 
Kwa masikitiko makubwa Mh. Halima Mdee ukiwa mbunge wa jimbo la kawe ulitokea kuwa tumaini jipya kwa wakazi wa jimbo hilo. Kwani mtangulizi wako Ritha Mlaki alishindwa kutekeleza hata kiduchu kile kinachowakera wakazi wa jimbo la kawe na hasa maeneo ya makongo juu. Eneo hilo lina kero ya muda mrefu iliyosababisha makongo kama sio sehemu ya wilaya ya Kinondoni mkoa wa Dar es Salaam. Hapa nitataja kero kuu mbili ambazo hadi niandikapo bandiko hilo nashindwa kuelewa tatizo liko wapi waheshimiwa nyie kushindwa kupata utatuzi.

1. Barabara. Ukianzia njia panda ya Chuo cha Ardhi hadi makongo mwisho na baadae kuendelea goba kutokea mbezi samaki hii barabara ni mbaya mbaya haina jinsi ya kuelezea. Imefikia mahali wakazi wa makongo juu wamechukulia kuwa sehemu ya maisha yao kila ifikapo saa 12 jioni na kuendelea kupanda dala dala kwa bei ya kuanzia sh. 500 kwa umbali usiozidi kilomita 5. Kinachoumiza hata huo usafiri wenyewe nao licha ya kuwa nauli yake iko juu bado haupatikani angaalau fadhila za madereva wa mabasi kutoka mwenge kwenda bagamoyo ndio zinasaidia vinginevyo sijui hali ingekuwaje..

2. Wakazi wa makongo juu tulishasahau hadithi ya kupata maji ya bomba. Mwaka 2009 kulifanyika uwekaji wa mtandao wa mabomba ya maji karibu eneo lote la makongo juu. Mabomba haya maarufu kama mabomba ya "mchina" tangu yalipowekwa na hiyo kampuni ya kichina mwaka huo hadi leo hayajawahi kutoa maji hata yale ya majaribio...Halima Mdee ulikuwa kuomba kura zetu kwa mbwembwe nyingi kuwa kilichomshinda Mlaki wewe utakimaliza..Lakini wakati tukiingia mwaka wa 2 tangu kufanyika uchaguzi mkuu 2010 hakuna hata dalili kuwa kuna kitakachofanyika....Mh..Halima Mdee kila nikikuangalia kupitia runinga ukiwa mle mjengoni napata hasira kuwa nilipoteza muda na kura yangu na sasa imani yangu inapotea kwako. Sina jinsi ya kuelezea hasira zangu kwako.

Mtu anaweza kusema kuwa tukikutegemea wewe peke yako utatue kero zetu ni uvivu wa kufikiri lakini hata sisi wananchi tulikuwa tayari kuchangia nguvu zetu kutatua tatizo la barabara...lakini wapi...wapi...bure tu...Nafikiria kusimama na wewe kwenye uchaguzi 2015 kupambana na wewe. Umekuwa mzuri wa kupiga kelele huko mjengoni lakini unasahau kuwa sisi tulikupa kura zetu ili utuongoze kutatua kero zetu na si vinginevyo..Naomba pindi utakaposoma thread hii jiulize moyoni mwako hivi unawatendea haki wapiga kura wa makongo????
 
Mkuu umekaa na UTAWALA WA CCM miaka zadi ya 45 hukupata hayo maji sasa unataka MDEE akupe maji kwa muda wa Miaka 2.

Yeye ndiye WAZIRI WA MAJI.?

Yeye ndiye Mkurugenzi wa HALMASHAURI YA KINONDONI.?
 
mkuu umekaa na utawala wa ccm miaka zadi ya 45 hukupata hayo maji sasa unataka mdee akupe maji kwa muda wa miaka 2.

Yeye ndiye waziri wa maji.?

yeye ndiye mkurugenzi wa halmashauri ya kinondoni.?

mdee ndie mbunge wao, ni muwakilishi wa wananchi bungeni na ni kiungo kati ya serekali na wananchi so lazima ajaribu kadri awezavyo kutatua kero za wananchi wake na anaposhindwa arudi kwa wananchi kuwapa majibu.
Tuache majibu rahisi kwa maswali magumu, ukweli na usemwe, anapaswa kuwajibika kwa wananchi wake.

 
mkuu halima hawezi kutatua matatizo yako.kazi yake ni kukusemea kama anvyofanya pale bungeni...hiyo ni kazi ya serikali yako dhaifu ya jk! Wao ndo wenye mamlaka na wanaopokea kodi zetu so wana wajibikia kukuletea maendeleao..tafakari chukua hatua...
 

mdee ndie mbunge wao, ni muwakilishi wa wananchi bungeni na ni kiungo kati ya serekali na wananchi so lazima ajaribu kadri awezavyo kutatua kero za wananchi wake na anaposhindwa arudi kwa wananchi kuwapa majibu.
Tuache majibu rahisi kwa maswali magumu, ukweli na usemwe, anapaswa kuwajibika kwa wananchi wake.


Ameshawajibika na anaendelea kuwajibika japokua anapata ukandamizwaji Bungeni huku mkiangalia na kuchekelea na mkasahau kama athari 2nazipata sie wapiga kura.

Hizo lawama za kusema amepoteza kura ndo namshangaa na hao aliowapa dhamana ya miaka 47 wamefanya nn..?
 

mdee ndie mbunge wao, ni muwakilishi wa wananchi bungeni na ni kiungo kati ya serekali na wananchi so lazima ajaribu kadri awezavyo kutatua kero za wananchi wake na anaposhindwa arudi kwa wananchi kuwapa majibu.
Tuache majibu rahisi kwa maswali magumu, ukweli na usemwe, anapaswa kuwajibika kwa wananchi wake.

Basi mleta hoja angehitaji majibu ya hoja alizomtuma mdee bungeni sio kudai maji,hiyo ni kazi ya magamba..
 
Mkuu umekaa na UTAWALA WA CCM miaka zadi ya 45 hukupata hayo maji sasa unataka MDEE akupe maji kwa muda wa Miaka 2.

Yeye ndiye WAZIRI WA MAJI.?

Yeye ndiye Mkurugenzi wa HALMASHAURI YA KINONDONI.?

Haya majibu tunayatoa baada ya kufikiri kwa kutumia vichwa vyetu timamu ama ile kitu nyingine inayokwenda kwa jina la Mstahiki Meya wa Jiji la Dsm?
Hivi unawezaje kuja na jibu la aina hii ukiweka pembeni ahadi alizomwaga Mheshimiwa Mbunge wakati wa Kampeni?
 
Kwa masikitiko makubwa Mh. Halima Mdee ukiwa mbunge wa jimbo la kawe ulitokea kuwa tumaini jipya kwa wakazi wa jimbo hilo.

2. Wakazi wa makongo juu tulishasahau hadithi ya kupata maji ya bomba. Mwaka 2009 kulifanyika uwekaji wa mtandao wa mabomba ya maji karibu eneo lote la makongo juu. Mabomba haya maarufu kama mabomba ya "mchina" tangu yalipowekwa na hiyo kampuni ya kichina mwaka huo hadi leo hayajawahi kutoa maji hata yale ya majaribio...Halima Mdee ulikuwa kuomba kura zetu kwa mbwembwe nyingi kuwa kilichomshinda Mlaki wewe utakimaliza..Lakini wakati tukiingia mwaka wa 2 tangu kufanyika uchaguzi mkuu 2010 hakuna hata dalili kuwa kuna kitakachofanyika....Mh..Halima Mdee kila nikikuangalia kupitia runinga ukiwa mle mjengoni napata hasira kuwa nilipoteza muda na kura yangu na sasa imani yangu inapotea kwako. Sina jinsi ya kuelezea hasira zangu kwako.

..Naomba pindi utakaposoma thread hii jiulize moyoni mwako hivi unawatendea haki wapiga kura wa makongo????

Hoja yako ni nzuri sana na inagusa vichwa vya Wananchi wengi; Kweli tuna matumaini makubwa na Mbunge kutekeleza ahadi na kutatua kero za Wananchi.

Tatizo la maji safi na salamu ni kero ambayo inagusa wananchi walio wengi, Serikali imekuwa na ahadi zisizotekelezeka kila mwaka wa bajeti kuhusu suala hili.

Serikali ilikuja na mradi wa mabomba ya Mchina (wengi tuliyaita hivyo amabyo yalienezwa eneo kubwa la jiji ambalo lina shida ya maji) lakini ile ilikuwa ni propaganda ya kisiasa, mikakati kwaajili ya uchaguzi wa mwaka 2005. na baada ya uchaguzi ule mradi ukabaki hewa. Mbinu ya kuunda mradi ule ilikuwa ni finyu sana, chanzo cha maji kilikuwa ni finyu sana, leo hii huwezi kutegemea kupata maji toka Ruvu na ikiwa kina cha maji hakitoshi. Hivyo Serikali ilipaswa kutafuta chanzo kingine cha maji kwa ajili ya ule mradi na siyo kutumia Ruvu (ndio maana nasema ilikuwa ni propaganda ya kisiasa)

Suala la barabara za mitaa lipo chini ya Manispaa ambayo pia yupo Mh. Diwani, hivyo ni vizuri pia wananchi wa eneo husika kuwasiliana na Diwani ili alipatie ufumbuzi tatizo la barabara. Kama Madiwani wa maeneo mngine wamefanikiwa iweje Diwani wa Makongo asifanikiwe???



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Haya majibu tunayatoa baada ya kufikiri kwa kutumia vichwa vyetu timamu ama ile kitu nyingine inayokwenda kwa jina la Mstahiki Meya wa Jiji la Dsm?
Hivi unawezaje kuja na jibu la aina hii ukiweka pembeni ahadi alizomwaga Mheshimiwa Mbunge wakati wa Kampeni?

Naomba Uorodheshe ahadi alizotoa Mdee Kawe.? Ambazo hajaazisema Bungeni pamoja na kukatishwa tamaa.
 
Tuache kuendekeza ujinga, kaa chini tafakari lini CDM imekusanya kodi yako kama unataka barabara na maji peleka maombi yako CCM utatusaidia na sisi pia
 
Mkuu umekaa na UTAWALA WA CCM miaka zadi ya 45 hukupata hayo maji sasa unataka MDEE akupe maji kwa muda wa Miaka 2.

Yeye ndiye WAZIRI WA MAJI.?...Biohazard...nadhani mtu aliyebuni kuwepo na kitu kinachoitwa bungwe alitumia busara sana. Sidhani kama wananchi wote tungekusanyika kwenye ofisi ya waziri wa maji au ofisi ya manispaa kupeleka kero zetu. Halima ametumwa na tuliompigia kura anawajibika kwetu 100% hiyo haina ubishi. Kuzungumza bungeni peke yake sio lengo anatakiwa kufuatilia na kutupa taarifa tuliomtuma ili kujua wapi amekwama na tufany nini? anapokaa kimya eti ameongea bungeni haina maana. Magamba kwa miaka 47 walishindwa kufanya na ndio maana tukasema basi na wao. Je na hawa nao tukae kimya mpaka wafikishe miaka 47? Hapana!!

 
Tuache kuendekeza ujinga, kaa chini tafakari lini CDM imekusanya kodi yako kama unataka barabara na maji peleka maombi yako CCM utatusaidia na sisi pia
...Nadhani kama n ujinga huenda ukawa wewe namba moja. Walitaka kazi tumewapa kazi...Visingizio kuwa CDM hawakusanyi kodi hata mimi nafahamu wanapoingia mle wanapokutana na hao wakusanya kodi ni jukumu lao kuwaeleza tuliyowatuma...Nina imani hufikiri kwa kutumia masaburi...:loco:
 

Yeye ndiye WAZIRI WA MAJI.?...Biohazard...nadhani mtu aliyebuni kuwepo na kitu kinachoitwa bungwe alitumia busara sana. Sidhani kama wananchi wote tungekusanyika kwenye ofisi ya waziri wa maji au ofisi ya manispaa kupeleka kero zetu. Halima ametumwa na tuliompigia kura anawajibika kwetu 100% hiyo haina ubishi. Kuzungumza bungeni peke yake sio lengo anatakiwa kufuatilia na kutupa taarifa tuliomtuma ili kujua wapi amekwama na tufany nini? anapokaa kimya eti ameongea bungeni haina maana. Magamba kwa miaka 47 walishindwa kufanya na ndio maana tukasema basi na wao. Je na hawa nao tukae kimya mpaka wafikishe miaka 47? Hapana!!


inawezekana Halima sio Waziri wa Maji, je ni Waziri wa migogoro ya Ardhi Kinondoni?
 
...Nadhani kama n ujinga huenda ukawa wewe namba moja. Walitaka kazi tumewapa kazi...Visingizio kuwa CDM hawakusanyi kodi hata mimi nafahamu wanapoingia mle wanapokutana na hao wakusanya kodi ni jukumu lao kuwaeleza tuliyowatuma...Nina imani hufikiri kwa kutumia masaburi...:loco:

acha kukurupuka, jitoe ujinga unarukia tu comment za watu kusudi uonekane una hoja soma mjinga mwenzio alichoandika halafu ndio ucomment pia waweza kuandika za kwako sio lazima uquote upeo wangu kaoshe magamba yako yanatoa harufu kali
 
Mkuu umekaa na UTAWALA WA CCM miaka zadi ya 45 hukupata hayo maji sasa unataka MDEE akupe maji kwa muda wa Miaka 2.

Yeye ndiye WAZIRI WA MAJI.?

Yeye ndiye Mkurugenzi wa HALMASHAURI YA KINONDONI.?

Mkuu hapa Umejibu Maswali yake yote.
 
...Nadhani kama n ujinga huenda ukawa wewe namba moja. Walitaka kazi tumewapa kazi...Visingizio kuwa CDM hawakusanyi kodi hata mimi nafahamu wanapoingia mle wanapokutana na hao wakusanya kodi ni jukumu lao kuwaeleza tuliyowatuma...Nina imani hufikiri kwa kutumia masaburi...:loco:

Kama unafuatilia Bunge la Bajeti bila shaka utagundua kuwa kuna mikakati madhubuti ya kuwakatisha tamaa na kuwafunga midomo wabunge wa upinzani.

Ukifuatilia utaona kuwa wabunge kambi ya upinzani wamekuwa mara kwa mara wakitoa kero za wananchi kwa ujumla lakini Serikali kwa kupitia Mh. Lukuvi na Werema kwa kisingizio cha kanuni za Bunge wamekuwa ni mwiba mkali kwa hoja za upinzania ambazo ni kwa ajili ya kutetea wananchi.

Serikali haitaki kuwapa nafasi wapizani kuongea kwa kujua kuwa wanawafungua wananchi masiki na kujua kilichopo yuma ya pazia.

Hivyo si kweli kuwa tumewachagua wabunge wa upinzania kisha hawatimizi ahadi zao, tatizo lililopo ni kwamba wanafungwa midomo kwa manufaa ya kisiasa na siyo kwa manufaa ya wananchi.

Mimi mwenyewe ni mwananchi wa jimbo la Kawe na nilimpa kura yangu Halima Mdee lakini siwezi kumlaumu kwa kipindi hiki kwani sababu zipo wazi za kutotekeleza baadhi ya kerohasa zile ambazo zinazosimamiwa na Serikali. Na pia siwezi kumtetea endapo kama atakuwa amepotoka. Nitasema ukweli wangu.

Hivyo wito wangu tusiwe tunalalamika kisiasa tusijekuwa sawa na Wabunge wetui wanaoweka masilahi ya Chama mbele badala ya kutatua kero za wananchi.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
inawezekana Halima sio Waziri wa Maji, je ni Waziri wa migogoro ya Ardhi Kinondoni?


Kwa upeo wangu mdogo wa kufikiri na kuelewa, ni kwamba Halima Mdee ni Waziri kivuri wa Kambi ya Upinzani katika Wizara ya Ardhi.


Hivyo anapoongelea suala la migogoro ya Ardhi, si Kinondoni tu bali Tanzania nzima inamuhusu, ni wizara yake ile katika upande wa upinzani.

Yeye ni Waziri mwenye dhamana hiyo.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Tatizo letu watanzania tunapenda sana ushabiki ambao hauna kichwa wala miguu.....tupo tupo na ndio maana hatuendelei!!!! Wewe kama ni CDM kama mie itakua vizuri pale wanapojikwaa wakosolewe na sio kuchekelea hata visivyochekesha khaaa!
 
CCM wameshindwa kutatua kero sugu za wananchi, nchini kote. Badala ya kujaribu, wanatenga bajeti kisha wanahujumu mipango yote ya kuleta maendeleo kwa wananchi, pamoja na kutatua kero zao. Ukiwa mbunge wa upinzani unakwamishwa kila upande. Utadhani hao wanaowakwamisha SIO Watanzania?

Ndio maana siku hizi CCM inaambiwa ijiandae kuondoka madarakani. Wameshindwa kwa miaka 50, sasa wawaachie wengine wenye utashi wa kuwakomboa wananchi, la sivyo TUTAINGIA VITANI. CCM inatupeleka vitani.

Mdee anakwamishwa, kwani anajua fika jinsi Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni inavyotumika kumhujumu.
 
Back
Top Bottom