What does this picture say about Us the People?

ha h aha,

hiyo ya u-lecturer nilikuwa sijaisikia ila sitashangaa. Waberoya kwake kila kitu kilichoharibika hapo Tanzania kimesababishwa na wapinzani.

Jana ulimbana kisawasawa aliposhindwa akanigeukia mimi akaanza zake za kulia lia nikamwambia kila hoja yako itajibiwa kwa hoja kadri itakavyokuja ana kasumba ya kuwabeza watu waliojitolea kwa hali na mali kuisaidia Tanzania kama kina Lipumba Mbowe Slaa Zitto Seif na wengine ndiyo hatukatai wana weakness zao tukimwambia aje na alternative anasema bora CCM sawa tuambie basi kwa nini iendelee hana jibu
 
Jana ulimbana kisawasawa aliposhindwa akanigeukia mimi akaanza zake za kulia lia nikamwambia kila hoja yako itajibiwa kwa hoja kadri itakavyokuja ana kasumba ya kuwabeza watu waliojitolea kwa mali na hali kuisaidia Tanzania kama kina Lipumba Mbowe Slaa Zitto Seif na wengine ndiyo hatukatai wana weakness zao tukimwambia aje na alternative anasema bora CCM sawa tuambie basi kwa nini iendelee hana jibu

Luteni,

Mimi nina motto yangu hapa JF, watu wenye viroja huwa siwajibu kwa hoja. Mimi huwajibu kwa hoja wale tu wenye kutoa hoja. Watu wenye udaku kama nikitaka kuwajibu namimi nawapatia udaku.

Kwa mfano -- watu kama mkamaP, kanda2 na wenzake huwa hawategemei kupata majibu ya kistaarabu toka kwangu kwa vile wanachoongea huwa ni upupu (kwa standard zangu). Kubwajinga/Waberoya and Co (yaani mamluki wa ccm) hapa pia hukutana na majibu yanayolingana na unafiki wao.

Nimesoma walichoendelea kuandika kwa zamu baada ya mimi kuondoka - (akianza mkamaP anakuja waberoya kabla kubwajinga hajaja kumalizia kabisa) nikacheka kama sina akili nzuri vile.
 
Luteni,

Mimi nina motto yangu hapa JF, watu wenye viroja huwa siwajibu kwa hoja. Mimi huwajibu kwa hoja wale tu wenye kutoa hoja. Watu wenye udaku kama nikitaka kuwajibu namimi nawapatia udaku.

Kwa mfano -- watu kama mkamaP, kanda2 na wenzake huwa hawategemei kupata majibu ya kistaarabu toka kwangu kwa vile wanachoongea huwa ni upupu (kwa standard zangu). Kubwajinga/Waberoya and Co (yaani mamluki wa ccm) hapa pia hukutana na majibu yanayolingana na unafiki wao.

Nimesoma walichoendelea kuandika kwa zamu baada ya mimi kuondoka - (akianza mkamaP anakuja waberoya kabla kubwajinga hajaja kumalizia kabisa) nikacheka kama sina akili nzuri vile.

Asante Mwafrika leo nimejifunza jingine kuwa mtu akija kwa hoja atajibiwa kwa hoja akija kwa udaku atajibiwa kwa udaku sasa mwepesi wa hasira anaondoka mwenyewe imekaa kama jino kwa jino vile anyway ngoja tuendelee kuchangia taifa kwa hoja iliyopo
 
Hivi Msimbazi pake iko chini ya Mbunge wa ilala siyo?
Mzee Mwanakijiji!
It doesn't matter kama msimbazi iko chini ya Mbunge wa Ilala au la hata kama ingekuwa chini ya Pinda au lowasa na hata mwenyewe Jakaya Mrisho Kikwete. I have said it hawa watu ni majambazi pronto.
Solution ni sisi tunaokerwa na uchafu kuinua mafyagio na kuifanya hiyo kazi wenye and no funny tricks. Hapa mataandika mpaka majogoo but the solution is in your hands. Kama unajiona una vijisenti jaribu basi uwalipe mamilioni ya vijana wanoshinda vijiweni wakicheza pool na kungojea kukwapua visimu vya mkononi jua linapozama. And those CCM fools are proud of that kwani those are soft targets wakati wa kununua kura and they don't even care kama wanabwia unga hata hiyo harufu hawasikii Kuanzia Meya and downwards they move in a/c cars of course tinted windows so uchafu in colour appears pleasant!!!! The bottom line is DO IT YOURSELF kama hamtaki kusikia then endeleeni kuzoza hapa JF....
 
Kwa elimu ipi waliyopewa wananchi watathamini usafi na afya zao?? Unajua kama mtu hujafuatilia chanzo utalaumu tu wananchi bure lakini angalia hayo maeneo wakazi wake wengi wana elimu kweli?? Na kama hawana elimu ni nani mwenye wajibu wa kuhakikisha wananchi wake wanakuwa na elimu ya kujua mema na mabaya??
 


Na hii hapa chini maeneo ya Msasani



Hapa ni njia ya kituo cha Polisi cha Msimbazi kama kinavyoonekana kwa mpiga picha. Nimepata picha hii toka kwa Evarist Chahali FB;

Ninajiuliza:
a. Uchafu huu ulianza kujirundika lini hapo? Ni wazi haikutokea siku moja ghafla bin vuup!
b. Ulipoanza kujirundika wahusika walikuwa wanafikiria nini? ni maua yanaota pembeni au mbolea?
c. Je kuna uwezekano wa wataalamu wa biolojia na viumbe hai kufanya utafiti kuona kama kuna jamii mpya ya viumbe hai imeanza kuishi humo na hivyo kutangaza eneo hilo kuwa ni hifadhi ya viumbe hai na kuwa ni "protected area"!?
d.Watu wanaoishi jirani na eneo hilo wanasubiri mwekezaji kutoka nchi gani kuja kuwasaidia kuwaonesha kuwa huo ni uchafu? au wanaamini "somebody's trash is someone's treasure"?
e. Inawezekana sisi ni taifa la watu waliozoea uchafu kiasi kwamba uwepo wake hautushtui tena kwani tumetengeneza some sort of immunity towards uchafu? Yaani hatuoni tatizo kupita na suti zetu, kupaki magari yetu na hata watoto kucheza mbele ya uchafu?
d. Do you see any similarity ya wananchi wa Tanzania na viongozi wabovu?

Mzee Mwanakijiji,

Uchafu ni kitu kinacho onekana kibaya pale tu jamii inayozunguka eneo lenye uchafu inatambua kuwa ni uchafu na hili linategemea elimu ya jamii husika.
Mkuu karibu New Delhi uone uchafu.....
 
Tatizo ni kuwa watu wanasubiri viongozi e.g wa ngazi za mtaa ku-organize usafi otherwise wanasubiri the so called "serikali" ndio wenye kuweza kufanya kila kitu!
 
Inasikitisha sana hii inanikumbusha tulipokuwa High School, shule moja hapa Dar.Kuna siku tuliingia darasani wakati huo tupo Form Six tukiwa busy na kujiandaa na papers akaja mwalimu wetu wa Darasa ambaye naye alikuwa mwalimu wa Chemistry.Sasa basi alipoingia kwa kuona takataka zilizopo Darasani akasema na nina quote " Darasa ili wote amfui chupi halafu shule yenyewe ilikuwa ya mchanganyiko ya wavulana na wasichana watu walishikwa na butwaa, akasema ndio amfui kwa sababu kama mngekuwa mnafua chupi uchafu ambao huko dhahiri mbele yenu amuuondoi je kwa ule usioonekana?.Hiyo imekuwa fundisho kwangu hata nyumbani na ofisini kwangu sipendi taka zizagae au kutosafishwa.Kwa hiyo tuwaulize wakuu je naniiii hawafui?
 
watu waanze kwa kujijengea vyoo! waache kwenda msituni!
 
Sasa mkuu wangu tunawaza kutengeza barabara za juu kabla hata ya miundombinu kama hii ni hatari sana maana sijawahi kuona kitu kama hiki katika maisha yangu,
 
Kwani hakuna "wazungu" wachafu?

sijui kama kuna watu unaweza ukawaambia kule nyumbani kuwa wapo wazungu wachafu, ombaomba, wezi, wabakaji, wauaji n.k.. baadhi ya watu wanachukulia "uzungu" sawa na "ubora".. ndiyo maana wapo ng'ombe wa kizungu, kuku wa kizungu.. wanawake wa kizungu!??
 
Kuna mtangazaji mmoja huwa namsikia mara kwa akisema "DAR KUNUKA". Kwa jinsi jiji lilivyo kwa kweli huwa nakubaliana na hiyo kauli yake, ukipita TANDALE, TANDIKA, MANZESE, YOMBO na kwingineko huwezi ukatofautisha hali ya maeneo hayo.
 
sijui kama kuna watu unaweza ukawaambia kule nyumbani kuwa wapo wazungu wachafu, ombaomba, wezi, wabakaji, wauaji n.k.. baadhi ya watu wanachukulia "uzungu" sawa na "ubora".. ndiyo maana wapo ng'ombe wa kizungu, kuku wa kizungu.. wanawake wa kizungu!??

Kumbe ndio maana kuna sehemu zinaitwa "uzunguni" na zingine zinaitwa "uswahilini". Na kumbe ndio maana ule msemo wa flani ana mambo ya "kiswahili" au flani ni "mswahili"....

Tuna matatizo mengi sana aiseee
 
Kumbe ndio maana kuna sehemu zinaitwa "uzunguni" na zingine zinaitwa "uswahilini". Na kumbe ndio maana ule msemo wa flani ana mambo ya "kiswahili" au flani ni "mswahili"....

Tuna matatizo mengi sana aiseee


kitu pekee ambacho huwezi kukikuta ni kuwa wale nyuki wakali wanaitwa wa Kiafrika, lakini yale mainzi makubwa ya kijani yanayofuata uchafu.. hayaitwi ya "kizungu"!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom