Ngalikihinja
JF-Expert Member
- Sep 1, 2009
- 31,244
- 31,338
Wewe ungeamua nini
???
Kuna jamaa kaoa lakini pamoja na hayo ana kimada nje ya ndoa yake. Mkewe alishatonywa lakini aliamua aanze na uchunguzi. Sasa kuna siku baba aliamua ku-surprise kimada wake kwa kumnunulia simu, lakini risiti iliandikwa jina lake (la baba). Alipofika nyumbani risiti akaisahau kwenye suruali, kama kawaida mama katika harakati ya kufua akiona. Baada ya kuisoma, akafahamu aina ya simu iliyonunuliwa. Cha kwanza akaamchunguza Yule kimada wa mumewe kama ana simu ya aina hiyo. Baada ya kupata uhakika huo, akaenda polisi kushitaki kuwa kaibiwa simu aliyonunuliwa na mumewe na mwizi wake anamfahamu. Kama kawa polisi wakaenda kumkamata kimada na baada ya kuulizwa akadai simu kanunuliwa na mpenzi wake. Akatumwa akamwite huyo mpenzi wake. Baada ya kutinga polisi, mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo;
Polisi: huyu unamfahamu..??
Baba: ndiyo ni mke wangu.
Polisi: hii risiti na hii simu unavifahamu..??
Baba: ndiyo.
Polisi: vya nani ??
Baba: mke wangu.
Polisi: we dada (kimada) hii simu si yako ni ya huyu mama, hivyo unawekwa ndani kwa kosa la wizi.
Baada ya mume na mke kuondoka, mume alirudi tena kuweka mambo sawa na kimada akatoka.
Swali
kwa wanawake, kama ungekuwa kwenye nafasi ya mke, ungefanya nini ??? Na kama ungekuwa ndo huyo kimada ungechukuwa hatua gani baada ya hapo ???
Kwa wanaume, ungefanya nini kwenye nafasi ile ya mume..???
Kuna jamaa kaoa lakini pamoja na hayo ana kimada nje ya ndoa yake. Mkewe alishatonywa lakini aliamua aanze na uchunguzi. Sasa kuna siku baba aliamua ku-surprise kimada wake kwa kumnunulia simu, lakini risiti iliandikwa jina lake (la baba). Alipofika nyumbani risiti akaisahau kwenye suruali, kama kawaida mama katika harakati ya kufua akiona. Baada ya kuisoma, akafahamu aina ya simu iliyonunuliwa. Cha kwanza akaamchunguza Yule kimada wa mumewe kama ana simu ya aina hiyo. Baada ya kupata uhakika huo, akaenda polisi kushitaki kuwa kaibiwa simu aliyonunuliwa na mumewe na mwizi wake anamfahamu. Kama kawa polisi wakaenda kumkamata kimada na baada ya kuulizwa akadai simu kanunuliwa na mpenzi wake. Akatumwa akamwite huyo mpenzi wake. Baada ya kutinga polisi, mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo;
Polisi: huyu unamfahamu..??
Baba: ndiyo ni mke wangu.
Polisi: hii risiti na hii simu unavifahamu..??
Baba: ndiyo.
Polisi: vya nani ??
Baba: mke wangu.
Polisi: we dada (kimada) hii simu si yako ni ya huyu mama, hivyo unawekwa ndani kwa kosa la wizi.
Baada ya mume na mke kuondoka, mume alirudi tena kuweka mambo sawa na kimada akatoka.
Swali
kwa wanawake, kama ungekuwa kwenye nafasi ya mke, ungefanya nini ??? Na kama ungekuwa ndo huyo kimada ungechukuwa hatua gani baada ya hapo ???
Kwa wanaume, ungefanya nini kwenye nafasi ile ya mume..???