Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,063
- 136,426
Ndiyo, wewe hapo kwenye hiyo picha.
Wewe siyo rais.
Hujashinda uchaguzi wowote ule na unalijua hilo na kila mtu analijua hilo.
Hujapigiwa kura na watu milioni 31.
Hujapata 97.6% ya kura zilizopigwa kwa sababu hakuna kura zilizopigwa.
Hilo unalijua kabisa hata ujikaushe namna gani.
Huna uzalendo wowte ule wewe.
Huna uwezo wowote ule wa kuwa kiongozi.
Toka lini mshindi wa 97.6% anaogopa kuapishwa hadharani?
Hao watu milioni 31 waliokupigia kura hiyo tarehe 29 Oktoba 2025, picha zao wakiwa wamepanga mistari kusubiri kukupigia kura wewe, ziko wapi?
Wewe na hao vibaraka wako wa tume ya uchaguzi mkajitungia idadi ya ajabu ya watu waliokupigia kura!
Dunia nzima inaucheka huo “ushindi” wako.
Umeandika rekodi mpya duniani ya kuwa mtu wa kwanza kushindana kwenye uchaguzi na nafsi zako wewe mwenyewe: Samia vs Suluhu vs Hassan 😂.
Huna lolote. Huna uhalali
Na endelea kudhani kuwa wewe hugusiki…..halafu tuone utaishia wapi!