mzalendo91
JF-Expert Member
- Sep 10, 2010
- 430
- 138
Salaam wana jf,Mwaka 2015 iwe isiwe lazima na mimi nipate kibanda changu cha kujisitiri na familia yangu maana tusio na nyumba sometimes naona kama tunyanyasika!!Hivi juzi juzi jobmate mwenzangu alipoteza mke na mtoto katika ajali ya bus huko Musoma,na mmoja ya waliokuwepo kwenye msiba huo ni baba mwenye nyumba anapoishi.Jamaa alienda kumzika mkewe upareni na alirudi jana na leo amekuja job.Wakati tunaendelea kumpa pole za hapa na pale!! .Simu yake iliita na alikwenda kuongelea pembeni.Aliporudi alitueleza mzee mwenye nyumba anataka kodi yake siku ya tarehe 01 saa mbili sharp bila kukosa na awali alikuwa alikuwa analipa kwa miezi sita sita but mzee kamwambia kwa tarehe hiyo alipe ya mwaka na kama hataweza tarehe 2 January ahame!My take: sikatai jamaa kulipa kodi kwa kipindi hicho but ni vema wenye nyumba mkawa na busara ya kumvumilia kidogo mtu hata apumzike kidogo then ndo umweleze.Kufiwa na mke na mtoto mara moja si jambo dogo na pia kitendo cha kupandisha miezi ya kulipia bila taarifa ya miezi mitatu pia si ustaarabu.Tiririkeni waungwana.
Mwambie jamaa yako kama anaweza utata afanye hivi.
1. Asifanye fujo yeyote na ajaribu kumwambia mwenye nyumba wake amwandikie notisi ambayo itaonyesha kuwa anatakiwa kuhama hiyo nyumba ndani ya mwezi mmoja. Akishapewa hiyo notisi aitunze vizuri.
2. Pindi itakapofika hiyo siku ya notisi atoe japo hata pesa ya mwezi mmoja halafu amsihi huyo mzee aipokee na waandikishiane kuwa nyingine atamlipa kesho yake kwa kuwa kuna pesa anaitegemea.
3. Huyo mzee mwenye nyumba akikubali hicho nilichosema hapo juu. Jamaa hasijitese tena kuhusu suala la kodi bali aendee tu kuitafuta pasipo pressure maana mwenye nyumba akifanya jambo lolote la kipuuzi kama vile kutoa vyombo vya jamaa nje.
4. Huyo msela wako akimbilie mahakamani kufungua kesi akienda na vithibitisho vyote kama mkataba wa awali, notisi aliyopewa chini ya mwezi 1 na yale makubaliano ya mkataba mpya ambapo alitoa pesa ya mwezi mmoja na mzee akaichukua.
5. Kesi ikishafunguliwa mahakaman na stop order ikatolewa, mpaka hiyo kesi isikilizwe na mahakimu kutoa hukumu huyo msela wako anaweza kujikuta kakaa kwa huyo mzee hata miaka 5 bure bila kulipia kitu chochote.
6. Mahakama nyingi nchini zina kesi zinazohusiana na masuala hayo ndio maana shauri likifunguliwa leo mpaka kuja kutolewa maamuzi ya mwisho uchukua miaka mingi.
NINATUMAINI USHAURI WANGU UTAKUSAIDIA SANA KAMA UKIUFANYIA KAZI