Nimekata tamaa, nimechoka! Naona haya maisha hayana faida!

God Forbid

Member
Jan 6, 2024
14
81
Daah nimeandika nikafuta, nikaandika nimefuata., Tokea Wiki nilitaka kuandika hili, nikawa najaribu kusubiri huenda ningepata majibu ila kwa sasa nimeiona niyatoe ya moyoni!

Kwanza nikiri nimekuwa mtumiaji wa hili jukwaa Kwa muda mrefu, zaidi ya miaka 15!

Nimekuwa nikiona nyuzi tofauti za watu kuomba ushauri, wengine husaidia na wengine huishia kudhihaki, so kwenye jamii ndio hivyo!!

Ishu yangu kwa kweli nimekuwa nikipitia kipindi kigumu, hasa kwenye maisha tu ya kawaida ya kila siku!!

Nina familia changa inanitegemea, mke alimaliza chuo hana kazi, ni miaka sasa! Nina kazi ila sina furaha na kazi!

Nilijaribu kuchukua mkopo benki nikampa mke afungue biashara, Ile biashara iliteketea yote katikati ya mwaka Jana, hakuna kilichookolewa!

Na kuanzia hapo ikabidi tuanze upya, nikaingia kwenye madeni ambayo kwa sasa kuyalipa imekuwa tabu, wadeni wananiandama kila kukicha sina cha kuwalipa!

Mshahara umeshakatwa hadi mwisho, sikopesheki popote na hata nikikopa cha kulipa Sina!!

Ndani ya familia kumekuwa na migogoro kila siku isoyoeleweka, watoto hata ada imekuwa kipengele!

Nikiwaangalia watoto na mama yao nawaonea sana huruma, kwa namna nashindwa kuwapa mahitaji yao kwa wakati!!

Hizi sikukuu za mwisho wa mwaka, wife aliniambia marafiki zake wanamcheka kwanini amekuwa so rough ina maana mume ameshindwa hata kukupa 10k ya kusuka?

Daah, yaani hivi juzi yupo ndugu yangu alipata ajali amelezwa, umepitishwa mchango wa familia nimeshindwa kuchangia hata mia, nimeumia sana!!!

Haya maisha yamenikaba kweli kweli. Sijui nachomokaje!

Inakuja roho ya kutaka niache kazi nitokomee, ninakokujua!

Mara nyingine napata mawazo ya kujiangamiza kabisa,(ila nikimtazama mwanangu mdogo anaponitazama pia kwa huruma, ni kama anajua nina masaibu) basi naishia kutoka machozi na kusema yataisha!!

Hivi sasa nina zaidi ya miezi sita nimempiga chenga mwenye nyumba sijamlipa kodi yake!

Yaani nikitoboa huu mwezi, Mungu saidia!

Nipo nimepigwa ganzi tu!

Kuna baadhi ya wanaonidai, wamenipa vitisho kuwa watanifanyia kitu kibaya, kwamba Mimi tapeli mara watanipeleka mahakamani, wengine Kwamba wataenda Kwa waganga kunifanyia unyama, kwamba napewa masala kadhaa yaani, sijielewi Kwa kweli!

Likitokea suala la kijamii mtaani, kazini, n.k hata Kama mchango ni buku imekuwa kipengele Kwa Sasa!

Simu smartphone nimeuza, hata hapa nimeumia kifaa cha rafiki yangu mmoja ambaye ndio kidogo ananipush, ila naona ameshaanza kunichoka!

Bando lenyewe nililotumia nimelipata Kwa kuvuna point!


Haya ninayopitia omba yasikukute!!!

 
Daah nimeandika nikafuta, nikaandika nimefuata., Tokea Wiki nilitaka kuandika hili, nikawa najaribu kusubiri huenda ningepata majibu ila kwa sasa nimeiona niyatoe ya moyoni!

Kwanza nikiri nimekuwa mtumiaji wa hili jukwaa Kwa muda mrefu, zaidi ya miaka 15!

Nimekuwa nikiona nyuzi tofauti za watu kuomba ushauri, wengine husaidia na wengine huishia kudhihaki, so kwenye jamii ndio hivyo!!

Ishu yangu kwa kweli nimekuwa nikipitia kipindi kigumu, hasa kwenye maisha tu ya kawaida ya kila siku!!

Nina familia changa inanitegemea, mke alimaliza chuo hana kazi, ni miaka sasa! Nina kazi ila sina furaha na kazi!

Nilijaribu kuchukua mkopo benki nikampa mke afungue biashara, Ile biashara iliteketea yote katikati ya mwaka Jana, hakuna kilichookolewa!

Na kuanzia hapo ikabidi tuanze upya, nikaingia kwenye madeni ambayo kwa sasa kuyalipa imekuwa tabu, wadeni wananiandama kila kukicha sina cha kuwalipa!

Mshahara umeshakatwa hadi mwisho, sikopesheki popote na hata nikikopa cha kulipa Sina!!

Ndani ya familia kumekuwa na migogoro kila siku isoyoeleweka, watoto hata ada imekuwa kipengele!

Nikiwaangalia watoto na mama yao nawaonea sana huruma, kwa namna nashindwa kuwapa mahitaji yao kwa wakati!!

Hizi sikukuu za mwisho wa mwaka, wife aliniambia marafiki zake wanamcheka kwanini amekuwa so rough ina maana mume ameshindwa hata kukupa 10k ya kusuka?

Daah, yaani hivi juzi yupo ndugu yangu alipata ajali amelezwa, umepitishwa mchango wa familia nimeshindwa kuchangia hata mia, nimeumia sana!!!

Haya maisha yamenikaba kweli kweli. Sijui nachomokaje!

Inakuja roho ya kutaka niache kazi nitokomee, ninakokujua!

Mara nyingine napata mawazo ya kujiangamiza kabisa,(ila nikimtazama mwanangu mdogo anaponitazama pia kwa huruma, ni kama anajua nina masaibu) basi naishia kutoka machozi na kusema yataisha!!

Hivi sasa nina zaidi ya miezi sita nimempiga chenga mwenye nyumba sijamlipa kodi yake!

Yaani nikitoboa huu mwezi, Mungu saidia!

Nipo nimepigwa ganzi tu!

Simu smartphone nimeuza, hata hapa nimeumia kifaa cha rafiki yangu mmoja ambaye ndio kidogo ananipush, ila naona ameshaanza kunichoka!

Haya ninayopitia omba yasikukute!!!
Usiache kazi wala kujidhuru, huo ni upepo tu utapita simama imara!
 
Usiache kazi wala kujidhuru, huo ni upepo tu utapita simama imara!
Wabongo sijui kazi tunaonaga ni maagano manina yani huyu mwalimu anavyoteseka hv unasema asiache kazi atakuja Kula kwako au??? Umeambiwa ana madeni mazito yasiomalizika na mshahara kiduchu wew unasema usiache nyokoo.

Mwalimu mm nakushauri acha kazi nenda kafanye kazi zako za kujiajiri ambazo hata Leo ukikosa kesho utapata kuliko hiyo ya mwisho wa mwez hata laki mbili haifiki ndani ya siku tatu imekwisha na huna tena sehemu ya kujinasua. Ualimu ni pepo

Mpwayungu Village
 
Wabongo sijui kazi tunaonaga ni maagano manina yani huyu mwalimu anavyoteseka hv unasema asiache kazi atakuja Kula kwako au??? Umeambiwa ana madeni mazito yasiomalizika na mshahara kiduchu wew unasema usiache nyokoo.

Mwalimu mm nakushauri acha kazi nenda kafanye kazi zako za kujiajiri ambazo hata Leo ukikosa kesho utapata kuliko hiyo ya mwisho wa mwez hata laki mbili haifiki ndani ya siku tatu imekwisha na huna tena sehemu ya kujinasua. Ualimu ni pepo

Mpwayungu Village
Mkuu kazi za kujiajiri atafanya bila mtaji? Kipindi chote hicho familia inakula nini?.

Kama alivyosema ana madeni maana yake hapo hatapata malipo yoyote hata Nssf kwa vile yatalipia madeni yake.

Asiache kwanza kazi, ila aanze kutafuta biashara ya kufanya, aianze ikikaa sawa kidogo aache kazi na awekeze nguvu zake kwenye hiyo biashara.
Positive mental attitude. ✌️
 
Achana na hayo mawazo ya kujiua
Tatizo lako ni dogo Sana.

Anza na kubadilisha mindset hakikisha Una-Play smart.

Kinachoisumbua familia yako negativity na mkiwa na negativity itakuwa ngumu kufanikiwa na kusimama upya tena.

Anza na haya maeneo kuyafanyia kazi.

@ negative emotions
@ Financial management
@ Spiritual
@ Restoration of Mindset

Baada ya hapo kitu kitarudi mahala pake. na mtaanza kula ,kuvaa na kunywa Kama walivyo watu wengine.

all the best .
 
shukuru Mungu hata ww unakazi,mm hapa nina familia mke na mtoto 1 sina kaz toka nmetoka job muda sasa mambo ni magum muda mwingin kwel unawaza bora ufe tu,

Lkn ukikumbuka kufa sio njia sahihi mtoto wako atalelewa na nan!?acha tu ndugu yang ila pole sana na ushukuru Mungu kwa yote kuwa na imani fanya ibada unayopitia mm ni juzi tu nimetoka na uzi wang hapa jf kuelezea lkn muda mwingine inabid tu ufocus na maisha usikate tamaa

Mm hapa bado sina kaz lkn najipa matumain ipo siku yataisha huku najitafuta japo madeni eeeeeeh acha tu

MUNGU ATUSAIDIE, ACHA MAWAZO YA KUFA KUFAA HATA MM YANAKUJA ILA NAYAKATAA SASA KIMTINDO KUJICHANGANYA NA WATU NA KUCHEZA PLAYSTATION KDG

Sent from my SM-J337W using JamiiForums mobile app
 
Inakuja roho ya kutaka niache kazi nitokomee, ninakokujua!
Mkuu pole sana. Kuacha kazi bila kuwa na kazi au biashara sikushauri, utazidisha tatizo. Pia ukitokomea maana yake unaikimbia familia na watateseka zaidi. Pia wewe huna uhakika wa huko unakoenda kama utafanikiwa, na kama uifanikiwa nafsi bado itakusuta kwa kuwa uliwakimbia wapendwa wako.
Mara nyingine napata mawazo ya kujiangamiza kabisa,(ila nikimtazama mwanangu mdogo anaponitazama pia kwa huruma, ni kama anajua nina masaibu) basi naishia kutoka machozi na kusema yataisha!!
Kujiangamiza hakutamaliza tatizo kwa wale unaowapenda ila kutamaliza tatuzo kwako tu. Je uko tayari wewe usiwepo lakini wale unaowapenda wateseke zaidi?. Don't give up, kila siku ni siku mpya yeye mambo mapya.
 
Daah nimeandika nikafuta, nikaandika nimefuata., Tokea Wiki nilitaka kuandika hili, nikawa najaribu kusubiri huenda ningepata majibu ila kwa sasa nimeiona niyatoe ya moyoni!

Kwanza nikiri nimekuwa mtumiaji wa hili jukwaa Kwa muda mrefu, zaidi ya miaka 15!

Nimekuwa nikiona nyuzi tofauti za watu kuomba ushauri, wengine husaidia na wengine huishia kudhihaki, so kwenye jamii ndio hivyo!!

Ishu yangu kwa kweli nimekuwa nikipitia kipindi kigumu, hasa kwenye maisha tu ya kawaida ya kila siku!!

Nina familia changa inanitegemea, mke alimaliza chuo hana kazi, ni miaka sasa! Nina kazi ila sina furaha na kazi!

Nilijaribu kuchukua mkopo benki nikampa mke afungue biashara, Ile biashara iliteketea yote katikati ya mwaka Jana, hakuna kilichookolewa!

Na kuanzia hapo ikabidi tuanze upya, nikaingia kwenye madeni ambayo kwa sasa kuyalipa imekuwa tabu, wadeni wananiandama kila kukicha sina cha kuwalipa!

Mshahara umeshakatwa hadi mwisho, sikopesheki popote na hata nikikopa cha kulipa Sina!!

Ndani ya familia kumekuwa na migogoro kila siku isoyoeleweka, watoto hata ada imekuwa kipengele!

Nikiwaangalia watoto na mama yao nawaonea sana huruma, kwa namna nashindwa kuwapa mahitaji yao kwa wakati!!

Hizi sikukuu za mwisho wa mwaka, wife aliniambia marafiki zake wanamcheka kwanini amekuwa so rough ina maana mume ameshindwa hata kukupa 10k ya kusuka?

Daah, yaani hivi juzi yupo ndugu yangu alipata ajali amelezwa, umepitishwa mchango wa familia nimeshindwa kuchangia hata mia, nimeumia sana!!!

Haya maisha yamenikaba kweli kweli. Sijui nachomokaje!

Inakuja roho ya kutaka niache kazi nitokomee, ninakokujua!

Mara nyingine napata mawazo ya kujiangamiza kabisa,(ila nikimtazama mwanangu mdogo anaponitazama pia kwa huruma, ni kama anajua nina masaibu) basi naishia kutoka machozi na kusema yataisha!!

Hivi sasa nina zaidi ya miezi sita nimempiga chenga mwenye nyumba sijamlipa kodi yake!

Yaani nikitoboa huu mwezi, Mungu saidia!

Nipo nimepigwa ganzi tu!

Simu smartphone nimeuza, hata hapa nimeumia kifaa cha rafiki yangu mmoja ambaye ndio kidogo ananipush, ila naona ameshaanza kunichoka!

Haya ninayopitia omba yasikukute!!!
Mkuu haupo peka yako na ukumbuke tu hii DUNIA SIO YETU mzee wangu.

Wapo baadhi yetu humu unatafuta buku tano kwa siku lakini bado haipatikani.

Daah badae watoto wetu wanakuja kudhihaki wenzao kwamba wao maskini wakati sasa hivi mshua wao anapitia kipindi kigumu asee inakera sana.

Sema nini kaka tuskate tamaa. MUNGU WETU SOTE na maisha yetu ya nyuma ni matokeo ya sasa.

APECHE ALOLO
 
Niseme tu ukwel kuna watu watanikashfu ila ukweli kuna mambo yanakuwa hayaendi hadi unamkosea mungu, na kuona shetani ni mkarimu na mwenye huruma kuliko mungu.

Kwa mungu huwa tunajikomba ila kiukweli tu hatujali hadi siku ambayo tutashtuka kuwa tunatumia nguvu sana kuamini mtu asiye na mda na sisi tunaamini ametupatia pumzi na uhai ndilo la kujivunia ila kuna maana gan mtu akupe uhai na uzima na kisha kukuterekeza jangwani bila kukujali na yule ambae tunaamini ni mbaya ni adui yeye ndio akuokote na akupe unafuu wa maisha?

Wanasema shetani anamasharti na marejesho magumu ila kuna raha gani ya kuteseka,?

Mbona sasa mungu hatupi nafasi walau kutupa bila kutukopesha?

Aliekuokota mavumbini na kukufuta na kukuonyesha njia na kukuheshimisha hata akitaka malipo au marejesho sioni kama ananinyanyasa bali anataka nilipe fadhira kwa kile alichonipa.

Ndugu acheni woga maisha mazuri yapo na wapo wanaoyaishi wekeni namba hapa za Waganga wa kwel wanaotoa ndagu za uhakika tuzamie huko dunia haihitaji huruma.
 
Sijui imani yako ila niamini mimi Mungu hujibu maombi.

Jaribu kukaa chini na kulia kidhati na Mungu wako. Palipo na Mungu hakuna linaloshindikana.

Baadhi ya mapito huja ili kukuandaa na kukuimarisha na neema zilzo mbele.

Dua yangu kubwa siku zote ni Mungu kunipa ustahmilivu katika kila gumu, kunipa moyo wa kukubali kila lile nisiloweza kubadilisha, kunisogeza karibu na kila lenye heri na mimi na kuniepusha kila lililo na shari na mimi.

Narudia tena muombe sana Mungu wako mambo yatafunguka bila hata kutarajia.
 
Back
Top Bottom