Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,341
- 51,907
Habari za Sabato!
Kwa kweli Sisi wengine tulishaweka miiko na mstari kuwa Mwanamke asiyeweza kujilipia nauli wala asiyeweza kujinunulia vocha huyo hatuwezi ku-date naye.
Kwanza hatuamini kabisa kuwa Mwanamke mrembo na mzuri anaweza kukosa nauli au vocha. Hilo siwezi kuamini.
Hiyo imetusaidia Sana kuepukana na Wanawake matapeli, Almaarufu wala nauli, wapiga mizinga ya kitoto toto, Wanawake wenye fikara za kimaskini hivi.
Mtoto yupo Arusha au Mwanza au Nairobi mnawasiliana anakuambia likizo anakuja, anajilipia nauli mwenyewe anakuja.
Hao ndio wasichana na Wanawake ambao Kwa kweli ninaweza kuingia nao kwenye mahusiano. Mnakaa mnajadili na mnapiga Stori za maana, sio unakaa na Mwanamke anawaza akiondoka utampa shilingi ngapi. Hizo sio type za Sisi Watibeli.
Vijana hasa ninyi vijana wadogo ambao mmetoka familia Duni, Vijana mnaojitafuta, chukueni ushauri wangu, utawasaidia pakubwa. Hakikisheni mnachukua Wanawake wanaowahitaji ninyi kimapenzi na kimahusiano. Wenye uwezo wa kujilipia Bills ndogondogo. Achaneni na Kutafuta Kupe na kunguni WA kuwanyonya Damu. Shauri yenu.
Asije Mwanamke Maskini akakuletea mawazo yake ya kimaskini aliyoyarithi Huko kwao, kwamba ati wewe mwanaume ndio unatakiwa umenyeke kumtunza, sijui umtumie nauli, sijui vocha sijui Pesa ya Kula, ukiona demu wako anamawazo ya hivyo jua huyo ni Maskini na atakuletea umaskini nyumbani kwako. Huo unaitwa umaskini wa kurithi. Lazima ufe mapema wewe. Lazima uso wako usiwe na Nuru wewe. Lazima ufubae, yaani huo ndio Utapeli ambao Watibeli hatutauruhusu.
Usije ukakubali kuwa mtumwa WA MTU mwingine Kwa vigezo vya kijinga ATI sijui wewe ni Mwanaume. Tena Kwa MTU ambaye hujamuoa, na hata kama umemuoa lakini ni MTU mbinafsi.
Yaani wewe ndio usulubike? Watibeli hatupo hivyo.
Yaani usulubike Wakati kuna wanawake kibao wanaojiweza, wanaoweza kukupenda na mkaenjoi Maisha Kwa kusaidiana wote pasipo ubinafsi.
Yaani upo na Mwanamke ambaye hata hajawahi kukusaidia chochote zaidi ya wewe ndio kuwa msukule wake kisa akupe ngono. Thubutu!
Vijana, eleweni kuwa Mwanamke akikupenda huwezi kuteseka, eleweni kuwa Mwanamke akikupenda atapata nauli na vocha ya kukutafuta tuu.
Vijana eleweni kuwa ukiona Mwanamke wako ni mbinafsi anataka tuu wewe ndio umhudumie ujue huyo hakupendi, jua wewe ni mtumwa wako.
ATI Mwanamke anakuambia kama usiponipa hiki Mimi na wewe basi, na wewe unaanza kuhangaika. Mpumbavu wewe!
Mbona Sisi hao Wanawake hawathubutu kusema hivyo. Usipende kupelekeshwa kijinga jinga!
ATI Mwanamke anakuambia, mwanaume gani huna Pesa alafu lenyewe linalokuambia kazi halina, Pesa Hana, lakini anatumia maneno yake kukuadhibu wewe ili umtumikie. Nawe Kwa ujinga wako na kutokujiamini kwako unajitutumua ili upate Sifa zake. Aliyekuambia Sifa za Mwanamke Maskini zitakusaidia ni Nani?
Umaskini wa fikra,
Umaskini wa Mali
Umaskini wa Roho.
Vijana wangu, kuweni Wanaume. Na uanaume hautatokana na Maoni ya Wanawake juu yako.
Uanaume ni kujitambua, kujua nafasi yako, kujua nini chakufanya. Kuishi kifalme na sio kutumikishwa kama Lofa. Pumbavu!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kwa kweli Sisi wengine tulishaweka miiko na mstari kuwa Mwanamke asiyeweza kujilipia nauli wala asiyeweza kujinunulia vocha huyo hatuwezi ku-date naye.
Kwanza hatuamini kabisa kuwa Mwanamke mrembo na mzuri anaweza kukosa nauli au vocha. Hilo siwezi kuamini.
Hiyo imetusaidia Sana kuepukana na Wanawake matapeli, Almaarufu wala nauli, wapiga mizinga ya kitoto toto, Wanawake wenye fikara za kimaskini hivi.
Mtoto yupo Arusha au Mwanza au Nairobi mnawasiliana anakuambia likizo anakuja, anajilipia nauli mwenyewe anakuja.
Hao ndio wasichana na Wanawake ambao Kwa kweli ninaweza kuingia nao kwenye mahusiano. Mnakaa mnajadili na mnapiga Stori za maana, sio unakaa na Mwanamke anawaza akiondoka utampa shilingi ngapi. Hizo sio type za Sisi Watibeli.
Vijana hasa ninyi vijana wadogo ambao mmetoka familia Duni, Vijana mnaojitafuta, chukueni ushauri wangu, utawasaidia pakubwa. Hakikisheni mnachukua Wanawake wanaowahitaji ninyi kimapenzi na kimahusiano. Wenye uwezo wa kujilipia Bills ndogondogo. Achaneni na Kutafuta Kupe na kunguni WA kuwanyonya Damu. Shauri yenu.
Asije Mwanamke Maskini akakuletea mawazo yake ya kimaskini aliyoyarithi Huko kwao, kwamba ati wewe mwanaume ndio unatakiwa umenyeke kumtunza, sijui umtumie nauli, sijui vocha sijui Pesa ya Kula, ukiona demu wako anamawazo ya hivyo jua huyo ni Maskini na atakuletea umaskini nyumbani kwako. Huo unaitwa umaskini wa kurithi. Lazima ufe mapema wewe. Lazima uso wako usiwe na Nuru wewe. Lazima ufubae, yaani huo ndio Utapeli ambao Watibeli hatutauruhusu.
Usije ukakubali kuwa mtumwa WA MTU mwingine Kwa vigezo vya kijinga ATI sijui wewe ni Mwanaume. Tena Kwa MTU ambaye hujamuoa, na hata kama umemuoa lakini ni MTU mbinafsi.
Yaani wewe ndio usulubike? Watibeli hatupo hivyo.
Yaani usulubike Wakati kuna wanawake kibao wanaojiweza, wanaoweza kukupenda na mkaenjoi Maisha Kwa kusaidiana wote pasipo ubinafsi.
Yaani upo na Mwanamke ambaye hata hajawahi kukusaidia chochote zaidi ya wewe ndio kuwa msukule wake kisa akupe ngono. Thubutu!
Vijana, eleweni kuwa Mwanamke akikupenda huwezi kuteseka, eleweni kuwa Mwanamke akikupenda atapata nauli na vocha ya kukutafuta tuu.
Vijana eleweni kuwa ukiona Mwanamke wako ni mbinafsi anataka tuu wewe ndio umhudumie ujue huyo hakupendi, jua wewe ni mtumwa wako.
ATI Mwanamke anakuambia kama usiponipa hiki Mimi na wewe basi, na wewe unaanza kuhangaika. Mpumbavu wewe!
Mbona Sisi hao Wanawake hawathubutu kusema hivyo. Usipende kupelekeshwa kijinga jinga!
ATI Mwanamke anakuambia, mwanaume gani huna Pesa alafu lenyewe linalokuambia kazi halina, Pesa Hana, lakini anatumia maneno yake kukuadhibu wewe ili umtumikie. Nawe Kwa ujinga wako na kutokujiamini kwako unajitutumua ili upate Sifa zake. Aliyekuambia Sifa za Mwanamke Maskini zitakusaidia ni Nani?
Umaskini wa fikra,
Umaskini wa Mali
Umaskini wa Roho.
Vijana wangu, kuweni Wanaume. Na uanaume hautatokana na Maoni ya Wanawake juu yako.
Uanaume ni kujitambua, kujua nafasi yako, kujua nini chakufanya. Kuishi kifalme na sio kutumikishwa kama Lofa. Pumbavu!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam