Wengi tuna 'depression' lakini tunaogopa kuongelea kwa kuhofia kuonekana dhaifu, kutangazwa, kuchekwa na tunaowashirikisha kufurahia tunayopitia

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
Hasa wanaume tunashindwa kusema ukweli kwamba tuna depression kwasababu tunaogopa kuonekana dhaifu kama wanawake, pia namna ambavyo jamii inamchukulia mwanaume inamuona kama kiumbe ambaye anatakiwa awe ngangali muda wote ila kiuhalisia depression haichagui mwanaume wala mwanamke.

Wengi sana tunapitia kwenye lindi la mawazo, stress na depression za kila namna kuanzia kudaiwa madeni, kufilisika, kukosa ajira, misuko suko ya ndoa, magoniwa, n.k.

Hivi ni vitu ambavyo ni ngumu sana kugawana na asiehusika lakini tunaweza kugawana comfort katika kufarijiana, kushauriana, kupeana moyo, n.k.

Kuongea huwa inasaidia kwa kiasi chake lakini sasa inafika kipindi unaona ni bora ukae kimya tu kulingana na uzoefu ulioupata katika maisha yako uliokufanya ujue maana halisi ya "kuwa uyaone" na "ukubwa dawa".

Unakuta una mtu wa karibu kabisa unaemwamini, anapoona una shida anaku hype kabisa "its okay unaweza kuongea na mimi, kuwa huru"

Baada ya muda unakuta mambo yako binafsi yameshasambaa mtaani, anaweza kuwa ni mzazi wako kabisa ama mwanafamilia lakini nae kwa lengo zuri la kupata ushauri wa zaidi akawaambia watu anaowaamini, matokeo yake hakuna siri tena, mtaani huko unaanza kujijua ushatangazwa "msimuone ana gari yule, pale alipo ana mawazo ya kurejesha deni", "msimuone ana mke mzuri vile, kagundulika ana kisukari shughuli hawezi", "msimuone vile anakwenda bar sana, kachapiwa mke yule", n.k. USHATANGAZWA!! hata kupita mitaa ya kati unaona noma.

Wengine unawaambia shida zako ila ndio wanafurahia mpaka wanaweza kukununulia chakula upate nguvu ya kuendelea kuwasimulia taabu zako, kwao ni kama kucheki tamthilia, kushuka kwako ama kuganda pale pale ndio furaha yao kubwa sana.
 
Mwanamke akipata shida ya kifedha anaweza kuitatua kwa kuhongwa.

Moja ya sababu kuu kwanini wanawake ni nadra kujinyonga kuliko Wanaume.
Unaweza honga mpaka kutatua tatizo la mtu? Na hii ni kwa asilimia ngapi ya wanawake huongwa?

Refer post ya malisa insta ndugu alie fungwa kurudi nyumbani mke anasomeshewa watoto,miradi aloacha imekufa na kakuta mtoto mwingine kutoka kwa mfadhili.......hii hutokea kwa asilimia chache sana wengi wa wanawake hufa na tai shingoni
 
Hii ni kweli kabisa. Kwa watu ambao washapitia hali ngumu wanaelewa. Kimsingi miaka ya sasa hatuna ile social security support kutoka kwa ndugu jamaa na rafiki.

Imagine unaweza kuwa na shida ya kukwama kodi ukaamua kumuapproach mzazi au ndugu yako. Jibu la kwanza atalokupa ni "Hali ni ngumu sana, kila mtu hana pesa sasa, pambana tu" sasa haya maneno hayana msaada wowote zaidi ya kumvuruga mtu zaidi.

But kwa watu ambao wapo socially responsible. Amekuja ndugu yako na shida, unatakiwa kupiga simu kadhaa na kutuma sms kadhaa ili upate msaada na kuweza kumtatulia shida yake. Kukosekana kwa social security support kama hii ndio inapelekea watu kuishi namna hii kwa mashaka na kushindwa kushirikiana nyakati za shida.

Mbona kwenye maswala ya ndoa bila aibu huwa tunakutana na kusaidiana tena michango mikubwa na kwa ahadi pia. Why ishindikane kwa mambo ya kawaida tena madogo madogo.
 
Nadhani pia utofauti wa kiuumbwaji na sababu za kijamii zinachangia. Wanaume tuna kiburi kinachofanya tuamini tunatakiwa kujiongoza kwenye mambo yetu binafsi na sio kuongozwa, hivyo hata ushauri huwa tunautafsiri kama ni muongozo kutoka nje.

Wakati wanawake, hicho kiburi hawana na kama sio kimaumbile basi ni jamii imewaaminisha kwamba ni sahihi wao kuongozwa tena na mwanaume. Endapo sio mwanaume basi awe ni mwanamke mwenzao mwenye sifa za kiume.
 
Matokeo yake ni wanaume tukiwa na changamoto tuko tayari kumshirikisha mtu endapo limetukaba sana, na ikifikia hiyo hatua, huwa hatutaki kushauriwa tunataka ufumbuzi wa moja kwa moja, yani kwa mfano mwanaume akiwa na shida ya milioni moja, akija kwako hataki ushauri wa namna ya kuipata anataka umpe ili akulipe baadae.

Wakati mwanamke kwa sababu huwa analizungumza tatizo mapema, huwa yuko tayari kupokea ushauri na akajiona amepata nguvu sana ya kutatua tatizo lake. Na muda mwingine mwanamke hashirikishi mtu tatizo ili asaidiwe, kwake msaada ni kitu cha ziada ila ni ili asikilizwe tu, akimaliza hata bila ya kupewa ufumbuzi, tayari anakuwa amepata amani kubwa.
 
Depression na Anxiety isikie tu mazee.
Ilinifanya niwe master wa Meditation in and out...
Meditation ni jibu kwa stress, anxiety,panic attack and depression.
Unapiga meditation huku mwenye nyumba anangonga hodi kudai kodi yake, huku unadaiwa pesa ya luku, hatari sana
 
Back
Top Bottom