Wakuu, Kuna jamaa yangu anaitwa Michael amefariki jana na habari nimezipata leo kupitia accounts za washkaji zangu za Facebook pamoja na Instagram.
Sasa ninajiuliza, kuna faida gani ya kuwa mtu mwema kwa maana wema wanakufa na wabaya pia wanakufa.
At least labda ingekuwa wema wanaishi muda mrefu hapa duniani, lakini wanakufa tu kama wakufavyo watu waovu.
Kuna faida gani ya kuwa mtu mwema??
Pole kwa msiba wa rafiki yako.
Kuhusu swali lako. Mtu akikufanyia ubaya utafurahi?
Fikiria kwamba upo katika mfumo. Na katika mfumo huo unaweza kuongeza ubaya, wengine wakaona ubaya huo, ukawaambukiza kutenda ubaya, na wao wakafanya ubaya, ikawa dunia ya ubaya ubaya tu.
Au, upo katika mfumo, unaweza kuongeza wema, wengine wakaona wema huowema huo, ukawaambukiza kutenda wema, na wao wakafanya wema, ikawa dunia ya wema wema tu.
Hapo utaamua kufanya ubaya ama wema?
Nitakupa story ilimtokea rafiki yangu mmoja Toronto. Jamaa alikuwa hana tabia ya kutoa pesa kwa ombaomba. Ila siku moja alijisikia tu kutoa pesa, pesa ndogo tu. Sasa, katika purukushani za mjini, mara baada ya kutoa oesa tu ile wallet yake ikadondoka. Sasa kumbe kulikuwa kuna mtu alikuqa kaona kika kitu kuanzia jamaa anatoa pesa kwa ombaomba mpaka wallwt inaanguka. Akaiokota ile wallet, akaanza kumfuatikia rafiki yangu amoe ike wallet. Rafiki yangu alikuwa anatembea haraka huyo jamaa aliyemfuatikia hakuweza kumpata kirahisi. Lakini hatimaye alimpata, akamrudishia ile wallet. Akasema "A guy who gives to the poor should never have to lose his money".
Yule bwana aliyerudisha wallet aliguswa sana nankitendo cha rafiki yangu kumpa ombaomba pesa akasema mtu anayetoa pesa kwa ombaomba hatakiwi kupoteza pesa zake. Akamrudishia wallet.