Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,744
Nashukuru sana rafiki yangu kwa haya maombi yako, naamini Mungu atatujalia yote uliyotuombea.... Asante sana
Sijaelewa hiyo mipini ndo nini.... nipe kwanza tafsiri yake ili niweze kujibuMpaka sasa unamipini mingapi?
pacha mimi wakati BAK anajipanga kutuwekea wimbo a shania twain na diana ross naomba mimi nitunge shairi kwa ajili ya dada yetu wa moyoni @fpKutoka kwenye sakafu ya moyo wangu dadaangu FP nakuombea maisha mema ya ndoa..na Mwenyezi Mungu akubariki sana!.....Ushauri wangu: Mti wenye matunda ndio utupiwao mawe..so, be strong as you have been for those 13 years!
Kibao cha kushushia namuomba fundi mitambo BAK akuwekee wimbo wa Diana Ross usemao 'when you tell me that you love me'
Nilikuita kamwali, labda ulikuwa busy. Nalisubiri kwa hamu hilo neno zuri. asante sanakamwali mbona hukuniita mapema!jamani!yani hongera sana mpenzi hebu ngoja nijipange af nikupe neeno zuuuri dadangu mpenzi!mimi love yu sana!
Ubwelili bambu? ufuna kuvemba kwani hasa?Usengwile Namnyangu! Nifuna kuwemba nde...nikuganile mno!
Niwi bahapa. Nikulolakesa tuUbwelili bambu? ufuna kuvemba kwani hasa?
asante mlongo wangu kwa kunigana
Nilikuita kamwali, labda ulikuwa busy. Nalisubiri kwa hamu hilo neno zuri. asante sana
chezeya wangoni walimu wa kiswahili wewe!nimeipenda hii!Kumi na tatu si hoja,kweli unastahili,
Ya kuwa pamoja,ya mgosi na kamwali,
Mmevumilia shida,na iliyokuwa ngumu hali,
Unastahili hongera.
Mwaka ulioolewa,usisahau maishani,
Mwenzio alinogewa,akakuweka ndani,
Mengi ulizushiwa,kuwa si mwema mwandani,
Unastahili hongera.
Itaendelea...
asante sana mlongo wangu.......... mnanipaje raha sasa! wangoni oyeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!Kumi na tatu si hoja,kweli unastahili,
Ya kuwa pamoja,ya mgosi na kamwali,
Mmevumilia shida,na iliyokuwa ngumu hali,
Unastahili hongera.
Mwaka ulioolewa,usisahau maishani,
Mwenzio alinogewa,akakuweka ndani,
Mengi ulizushiwa,kuwa si mwema mwandani,
Unastahili hongera.
Itaendelea...
what would I have done without you mlongo wangu? usengwili sana.Mungu mebariki ndoa ,kwa upendo uso na doa
baraka alowapatia,milele dumu ameitoa
pokeeni kwa mapana ,baraka zake Rabana
MWANZO UKAWE MILELE,TISA OKTOBA ILEILE
Mapenzi mlopeana ,yadumu bila hiyana
leo milele kama jana,mejalia Maulana
nidhamu aloiona,sipindishe akanuna
MWANZO UKAWE MILEL,TISA OCTOBA ILEILE
Kwa busara mlizopewa,mlijenge na kulinda
penzi lataka pepewa,kupendwa kwake kupenda
kulikinga nao chawa ,vya watu wenye kuwinda
MWANZO UKAWE MILELE,TISA OCTOBA ILEILE
Watoto mlojaliwa ,kwao nyie ni vinara
wapeni mahitajiwa,kwao wakawe ishara
upendo wenu wa ndowa,kwao ukawebendera
MWANZO UKAWE MILELE,TISA OCTOBA ILEILE
Rafiki wako kipenzi,hajajuta kuwa nawe
wake mkewe mpenzi,ajivuna kwa wenziwe
litunze na lenu penzi,wengine mu mfanowe
MWANZO UKAWE MILELE,TISA OCTOBA ILEILE.